Boramaisha
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 820
- 18
Baadhi ya watumishi wa Serikali wamekuwa wakilalamika kwamba wamepoteza muda mwingi kufanya mazoezi ya kujitayarisha na mashindano ya kila mwaka ya Wizara na Idara za Serikali - SHIMIWI lakini ghafla wametangaziwa kwamba SHIMIWI haipo mwaka huu.
Je, kuna sababu gani ya kutofanyika mashindano hayo mwaka huu? Je, yawezekana fedha za kuendesha mashindano hayo hazipo kwa kuwa zimeingizwa kwenye matumizi ya Uchaguzi? Kama hivyo ndivyo watumishi hawa wa Serikali na Idara zake wategemee nini baada ya uchaguzi kwisha? Ni dhahiri kuna hatari kwamba hata mishahara wataweza kuikosa maana fedha zitakuwa zimetumika kwenye gharama za kuitafutia Serikali iliyo madarakani ushindi kwenye Uchaguzi mwezi ujao!
Wenye kujua sababu za kutokuwepo SHIMIWI mwaka huu tunaomba watueleze.
Je, kuna sababu gani ya kutofanyika mashindano hayo mwaka huu? Je, yawezekana fedha za kuendesha mashindano hayo hazipo kwa kuwa zimeingizwa kwenye matumizi ya Uchaguzi? Kama hivyo ndivyo watumishi hawa wa Serikali na Idara zake wategemee nini baada ya uchaguzi kwisha? Ni dhahiri kuna hatari kwamba hata mishahara wataweza kuikosa maana fedha zitakuwa zimetumika kwenye gharama za kuitafutia Serikali iliyo madarakani ushindi kwenye Uchaguzi mwezi ujao!
Wenye kujua sababu za kutokuwepo SHIMIWI mwaka huu tunaomba watueleze.