samaki2011
JF-Expert Member
- Dec 17, 2013
- 1,775
- 468
Bajeti ya Sh50 bilioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya safari za Rais Jakaya Kikwete katika mwaka ujao wa fedha ni miongoni mwa mafungu ya fedha yaliyopigwa panga ili kuwezesha kupatikana kwa fedha za kugharimia miradi ya maendeleo. Habari kutoka ndani ya kikao cha majadiliano baina ya Serikali na Kamati ya Bunge ya Bajeti zinasema, Sh11 bilioni zimepunguzwa katika fungu hilo na kubakiza Sh39 bilioni.
Hata hivyo, kiasi kilichobakishwa ni ongezeko la asilimia 260 la Sh15 bilioni zilizopitishwa na Bunge mwaka jana kwa ajili ya safari za Rais katika mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30 mwaka huu.
Katika bajeti ya 2013/14 safari za Rais zilitengewa Sh15 bilioni lakini inaonekana fedha zilizotumika ni nyingi zaidi maana ndani ya miezi miwili tu zote zilikuwa zimemalizika, kilisema chanzo chetu na kuongeza:
Kwa hiyo kwa mwaka 2014/15 Serikali ilimtengea Rais Sh50 bilioni za safari, ila tumekata Sh11bilioni ili kupelekwa katika shughuli nyingine za maendeleo. Kwa hiyo kwa mwaka ujao wa fedha, safari za Rais zitatengewa Sh39 bilioni.
source: Mwananchi newspaper
Wadau nimewachomolea hii habari kutoka gazeti la mwananchi. Swali langu ni kwamba bajeti ya safari za raisi ni sawa au zaidi ya bajeti ya wizara moja nyeti, huko nje kunaliingizia taifa kiasi gani? na mbona siwaoni marais wa nchi nyingine wakisafiri sana kama marais wetu? na kama kweli safari hizi zina tija mbona hatuwi matajiri kuliko nchi nyingine ambazo maraisi wake hawasafiri kama hawa wetu?
Hata hivyo, kiasi kilichobakishwa ni ongezeko la asilimia 260 la Sh15 bilioni zilizopitishwa na Bunge mwaka jana kwa ajili ya safari za Rais katika mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30 mwaka huu.
Katika bajeti ya 2013/14 safari za Rais zilitengewa Sh15 bilioni lakini inaonekana fedha zilizotumika ni nyingi zaidi maana ndani ya miezi miwili tu zote zilikuwa zimemalizika, kilisema chanzo chetu na kuongeza:
Kwa hiyo kwa mwaka 2014/15 Serikali ilimtengea Rais Sh50 bilioni za safari, ila tumekata Sh11bilioni ili kupelekwa katika shughuli nyingine za maendeleo. Kwa hiyo kwa mwaka ujao wa fedha, safari za Rais zitatengewa Sh39 bilioni.
source: Mwananchi newspaper
Wadau nimewachomolea hii habari kutoka gazeti la mwananchi. Swali langu ni kwamba bajeti ya safari za raisi ni sawa au zaidi ya bajeti ya wizara moja nyeti, huko nje kunaliingizia taifa kiasi gani? na mbona siwaoni marais wa nchi nyingine wakisafiri sana kama marais wetu? na kama kweli safari hizi zina tija mbona hatuwi matajiri kuliko nchi nyingine ambazo maraisi wake hawasafiri kama hawa wetu?