Fedha za safari za JK zaibwa na watendaji

Hivyo ni vijisenti wanavyochukua kila siku hapa labda walidhulumiana mgawo ndiyo kadili kakajulikana na sisi vipofu
 
Fedha za safari za JK zaibwa

MAOFISA watano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuiba fedha zilizotengwa "kwa ajili ya safari za rais," MwanaHALISI limeelezwa"

........................................................................

Source: Gazeti la Mwanahalisi:

Lakini kwa kuwasimamisha hawa Dagaa haitasaidia, kwa nini Ofisi ya Ikulu isiwafanyie kazi Sangara!!!

Au hizi pesa kwa sababu ni za safari ya Raisi ndio maana imewauma sana, mbona ubadhirifu mwingine wanaufumbia macho.

SERIKALI AMKENI, WIZI HADI CHINI YA KITANDA. BALAA HILI!!!!!!!!!!!!!!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Ndio maaana huko ikulu kila mtu anapatakaeee, pesa zote hizo ni kwasafari tuu au na kwa mambo mengine?. Kwautashi wangu wa haraka bila kufanya utafiti akinifu, tunakoelekea kubaya na tena kubaya sana, halii hii inatisha kwa mtu anaye tafakari kwa kina na kibinaadamu. Hii kwa mfano naweza kusema watoto waingie kwenye chumba cha baba yao na kufungua kabati la kuifadhia pesa za baba yao na kuchukua fedha bila kupata ridhaa kutoka kwa mzazi, hiii ni mbaya machoni na kusikia. Kama wazazi wetu walio aminika nakupewa madaraka makubwa namna hii tena wenye kuhitaji uzalendo wa hali ya juu zaidi wanaweza kufanya hivyo sijui miaka ishirini ijayo kutakua na haligani Tanzania, nafikiri udhalimu wote utafanyika katika nchi hii, itakua zaidi ya pango la wanyang'anyi, fanya utakavyo hakuna wakukuuliza! INASIKITISHA KWELI KWELI!
 
Labda tu nikukumbushe ndugu yangu, hizi ni zama za Chukua Chako mapema ili mradi usibabwe!
 
Hawa wezi ... kama kweli wameiba - basi nimewapenda! .... walikuwa wapi hawa siku zote? - wamefanya jambo la maana ila jamaa aache U-Vasco da Gama wake!

Walitakiwa waanze mwanzo tu jamaa baada ya kuingia madarakani ... aingekuwa anasafiri kwenda kubembea huko nje!
 
hivi ikulu na mambo ya nje ni wizara moja? huu wizi umetokea ikulu au mambo ya nje? (KAMA KWELI UMETOKEA)
 
NAsikia zilikuwa za safari yake aliyoipanga kwenda Papua New Guinea!
 
Fedha za safari za JK zaibwa

MAOFISA watano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuiba fedha zilizotengwa “kwa ajili ya safari za rais,” MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa za uhakika zilizopatikana ndani ya ikulu na wizara hiyo, zimesema kwamba maofisa hao, akiwemo Mkuu wa Itifaki, walifanikiwa kuchota Sh. 3 bilioni “kutoka benki moja nchini.”


........................................................................

Source: Gazeti la Mwanahalisi:

inawezekana ni mchezo wa muda mrefu tu.ila kwa sasa wanamhofia CAG
 
Hazijaibwa Ikulu zimeibwa mambo ya nje na Maafisa ambao sio wa Ikulu bali ni wa wizara hiyo.... mwanahalisi wametumia Ikulu kuuza gazeti lao. Fedha zilikuwa mikononi mwa wizara hiyo na ndio walikuwa walinzi wa fedha hizo sio Ikulu. Let be fair
 
Taarifa zinasema walisimamishwa kazi wiki mbili zilizopita, but kati ya hao waliosimamishwa kuna ambao wapo Nje ya nchi (Brazil) kikazi mpaka sasa. Kuna haja ya kujua namna transaction ya kutoa fedha za matumizi serikalini inavyofanyika coz haiwezekani Katibu wa wizara asijue dili kama hilo! Si ajabu hata TAKUKURU wamepata taarifa hizi kupitia Mwanahalisi!

hapo kwenye kala,,,hao TAKUKURU ndo washehereshaj wa rushwa bongo
 
Hii ni hatari wezi wameamua sasa kutafuna hicho hicho kidogo kinacho tengwa kwa ajili ya Ikulu. Sasa inabidi rais ashtuke hapa tafsiri yake ni kwamba rais ameng'atwa alikuwa amesinzia sasa inabidi aamke kukabiliana na hawa panya.
 
Hii ni hatari wezi wameamua sasa kutafuna hicho hicho kidogo kinacho tengwa kwa ajili ya Ikulu. Sasa inabidi rais ashtuke hapa tafsiri yake ni kwamba rais ameng'atwa alikuwa amesinzia sasa inabidi aamke kukabiliana na hawa panya.

ye kang'atwa sie tunatafunwa
 
Back
Top Bottom