Fedha za Mfuko wa Jimbo kwa Jimbo la Hai Kilimanjaro hazionekani Jimboni tangu 2020 hadi 2022

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,818
21,419
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.

Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.

CCM ni janga la kitaifa.


######

Mbunge atoa ufafanuzi kuhusu madai hayo[/B]

Akijibu taarifa hizo, Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe amekanusha uwepo wa madai hayo ya matumizi mabaya ya Fedha za Mfuko wa Jimbo akieleza hakuna ukweli katika suala hilo.

Anasema “Fedha hizo zipo kwa mujibu wa Sheria, haziingii kwenye akaunti ya Mbunge kama wengi wanavyodhani, zinaingia katika akaunti ya Mkurugenzi wa Halmashauri.

"Zikiingia Mkurugenzi anamtaarifu Mbunge kama Mwenyekiti wa Mfuko wa Jimbo ambaye anaitisha kikao kwa ajili ya maelekezo, fedha hizo zinaenda kwenye miradi ya Serikali.

“Mimi huwa huwa ninaita Madiwani tunajadili kuhusu miradi na kuidhinisha, lakini wanaonunua, wanaosambaza, wanaosimamia ni Halmashauri na siyo mimi Mbunge.”

Amesema Mkurugenzi wa Halmashauri anaweza elezea zaidi kuhusu fedha hizo kwa kuwa ndiye anayezipokea kupita akaunti yake.

Ametaja Wajumbe wa Mfuko wa Jimbo kuwa ni:

1. Saashisha E Mafuwe (Mb)- Mwenyekiti
2. Leonard Luhwavi - Mkuu wa Idara ya Mipango, Takwimu na uratibu -Katibu.
3. Judica J. Munisi - Diwani wa Machane Kaskazin -Mjumbe
4. Zanika A. Mushi Diwani V/Maalum-Mjumbe.
5. Hellen J. Munuo- Mtendaji Kata ya Muungano-Mjumbe.
6. Andrew E. Msuya - Mtendaji Kata ya Masama Mashar - Mjumbe.
7. Asifiwe James Malya - Mwakilishi kutoka NGO
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.
Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.
CCM ni janga la kitaifa.
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.
Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.
CCM ni janga la kitaifa.
Anaweza kuwa jamaa anatumia kumlipia wakili Sabaya
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.
Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.
CCM ni janga la kitaifa.
UGAWAJI NI KESHO: VIFAA VYA UJENZI VILIVYONUNULIWA KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO

Kesho, Ijumaa, 10.6.2022, Halmashauri yetu (Musoma DC) ITAGAWA vifaa vya ujenzi vilivyonunuliwa kwa kutumia FEDHA za MFUKO wa JIMBO la MUSOMA VIJIJINI.

Sekondari zilikaribishwa kutuma maombi ya kusaidiwa vifaa vya ujenzi, hasa za ukamilishaji wa ujenzi wa Maabara zao 3 (Physics, Chemistry and Biology).

Maombi yalitumwa kwa Afisa Mipango wa Halmashauri yetu (Musoma DC).

Kamati ya Mfuko wa Jimbo, chini ya Mwenyekiti wake, Mbunge wa Jimbo (Prof Sospeter Muhongo) ilifanya KIKAO na kupitia maombi yaliyotumwa na hatimae kugawa vifaa vya ujenzi vitakavyonunuliwa kwa kutumia Fedha za Mfuko wa Jimbo la Musoma Vijijini.

Orodha iliyoambatanishwa hapa inaonesha undani wa ugawaji wa vifaa hivyo vya ujenzi.

Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Alhamisi, 9.6.2022
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.
Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.
CCM ni janga la kitaifa.
Fanyeni utafiti, sijui kama mnajua Uhifadhi na taratibu za matumizi ya fedha za mfuko wa jimbo. Fedha hii haipo kwenye akaunti au mfukoni mwa Mbunge bali wakurugenzi wa halmashauri.

Ni madiwani wanaoibua miradi na Mbunge atoa aproval kwa matumizi akizingatia kilio cha wapiga kura wake.
 
CCM Jimbo la Hai pitieni uzi huu mtagundua Hakuna mbunge kwenye hilo jimbo.
 
Fanyeni utafiti, sijui kama mnajua Uhifadhi na taratibu za matumizi ya fedha za mfuko wa jimbo. Fedha hii haipo kwenye akaunti au mfukoni mwa Mbunge bali wakurugenzi wa halmashauri. Ni madiwani wanaoibua miradi na Mbunge atoa aproval kwa matumizi akizingatia kilio cha wapiga kura wake.
Diwani wa darasa la saba tangu Lini wakaibua mradi? Mbunge amekula fedha zote anazingizia madiwani.
Mbunge ni graduate madiwani la saba.
 
Kwa Hali ya mbunge wa Hai ilivyo tumegundua chadema tulifanya mengi kuliko ccm .
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, unaulizwa Fedha Za mfuko wa jimbo kwa Jimbo la Hai zimeweza kusaidia shughuli gani tangu 2020 hadi 2022?

Kuna kila dalili fedha hizo wanalamba asali wachache.
Miaka ya 2015-2020 fedha hizo zilioneka jimboni na Kufanya shughuli muhimu ila kwa sasa mbunge anajengea nyumba yake ya kuishi.
CCM ni janga la kitaifa.
Matunda ya kuongozwa na Rais mpumbavu ndiyo yanakuwaga hivi.
 
Part 2:
BARABARA ZINAZOJENGWA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

A - FEDHA ZA BAJETI YA MAENDELEO (ROAD FUND DEVELOPMENT BUDGET) 2021/2022

(1) Mkirira - Kwangwa Hospital (Gharama: Tsh Milioni 350). Limekamilika kwa 90%

(2) Bukima-Bulinga- Bwasi (Gharama: Tsh Milioni 300). Ujenzi umekamilika

B - Fedha za Jimbo
Masinono - Kinyang'erere (Gharama: Tsh Milioni 500). Likiwemo Daraja la Jitirola na mengine mawili. Hatua za kumpata Mkandarasi zinakamilishwa

C - FEDHA ZA TOZO
(Jumla: Tsh bilioni 2)
Barabara zinazojengwa na utekelezaji umeanza:

(1) Mmahare-Etaro-Nyasaungu
(2) Mugango-Bwai Kwitururu- Kwikuba
(3) Bwai Kwitururu- Bwai Kumsoma
(4) Maneke-Mayani- Kyawazaru
(5) Nyaminya-Kataryo- Kyawazaru
(6) Rwanga-Seka-Mikuyu
(7) Saragana- Nyambono- Chumwi
(8) Kaburabura-Masinono-Bugwema
(9) Bukima-Bulinga- Bwasi
(10) Busekera-Burungu
(11) Chitare-Kurugee-Buraga (Kivukoni)
(12) Kome - Buira
(13) Kigera Etuma-Ekungu
(14) Nyakatende-Kamguruk- Kigera Etuma
(15) Mkirira-Nyegina-Esira
(16) Kurukerege-Nyegina

TAARIFA kutoka:
*Ofisi ya TARURA (W)
*Ofisi ya Mbunge
Mbunge wa ccm Hai soma taarifa ya mbunge mwenzako ujifunze utendaji kazi na upunguze maneno uzidishe matendo vinginevyo chadema tunakutoa madarakani 2025 asubuhi
 
Ukitaka kumtuhumu kiongozi au mtu yeyote basi uwe na uelewa na kitu unachokisema, inaonekana hujui hata unachomtuhumu mbunge wa Hai ni kitu gani wala hujui mfuko wa jimbo ni nini!!

Ngoja nikusaidie kidogo labda itakusaidia kupata ufahamu wa CDF.

Mfuko wa kuchochea Maendeleo ya jimbo (CDF) upo kisheria, umeazishwa kwa Sheria namba 16 ya mwaka 2019.

Kazi ya mfuko wa kuchochea Maendeleo ya jimbo ni kusaidia kuendeleza au kuazisha miradi ya Maendeleo katika jimbo husika.

Mfuko wa kuchochea Maendeleo ya jimbo unaongozwa na Kamati ya Mfuko wa kuchochea Maendeleo ya jimbo, ambayo Mwenye kiti wa kamati hii ni Mbunge husika wa jimbo na Katibu wake ni Afisa Mipango wa Halmashauri husika.
Wajumbe wengine wa mfuko huu ni madiwani 2, Watendaji wa kata 2, Muwakilishi wa Ngo 1, na wawakilishi wa Wananchi.

Mfuko unaendeshwa na kamati, Kamati imepewa majukumu ya kupitia miradi na kuchambua miradi yote inayofadhiliwa na mfuko huu.

Sheria inataka miradi inayofadhiliwa na mfuko huu iibuliwe toka ngazi ya chini( Wananchi), Wananchi wanaibua miradi wanayotaka kutekeleza then inawasilishwa kwenye kamati kupitia kwa katibu wa mfuko.

Kamati inapitia maombi yote yaliyowasilishwa na kufanya maamuzi ni miradi ipi itekelezwe. Hakuna mradi unaotekelezwa bila kuidhinishwa na kamati.

Mbunge hawezi kuchukua hela ya mfuko wa kuchochea Maendeleo ya jimbo kwa kuwa fedha hizi ni za Serikali, zinakaguliwa kama fedha nyingine za Serikali.

Fedha za mfuko wa jimbo hazipitii kwenye account ya Mbunge wala hazipiti ofisi ya mbunge. Fedha hizi zinakuwa incorporated kwenye bajeti ya Halmashauri wakati wa kuanda mpango na bajeti wa Halmashauri husika, fedha hizi zinasimamiwa na Mkurugenzi wa Halamashauri husika. Malipo ya fedha hizi yanapita kwenye mfumo wa malipo wa Serikali ( MUSE) .

Hakuna namna mbunge anaweza kaenda kwa Mkurugenz akachukua fedha na kwenda kujengea nyumba yake..

#Mungu ibariki Tanzania
# Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
# #Tujiandae kuhesabiwa, Sensa ni kwa Maendeleo yetu
 
Back
Top Bottom