Maxence Melo
JF Founder
- Feb 10, 2006
- 4,230
- 13,415
Serikali kwa mara nyingi imekuwa inakiri kuwepo kwa matumizi yasiyo ya lazima na kuahidi kuyapunguza.
"Serikali itaendelea na jitihada zake za kudhibiti matumizi kwa kuahirisha ununuzi wa kila aina ya magari [...]; kupunguza malipo ya posho mbalimbali, kukata gharama za mafuta kwa magari ya serikali, kupunguza idadi ya safari za ndani na nje, [...] na kuendelea kuhakikisha kwamba semina na warsha zinaondolewa na kama ni za muhimu basi ni lazima ziidhinishwe na Ofisi ya Waziri Mkuu, "alisema Waziri wa Fedha, Mheshimiwa M. Mkulo, tarehe 8 Juni 2011
Leo hii, jumla ya makadirio ya matumizi ya vitu visivyo vya lazima ni shilingi za kitanzania bilioni 568 ingawa wadau wa ndani na wahisani wamekuwa wakionyeshawasiwasi wao kuhusu kuendelea kwa tatizo la matumizi yasiyo ya lazima.
Kwa hisani ya SIKIKA
Zaidi download attachment hii ndogo yenye mapendekezo ya wapi papunguzwe fedha, kiasi gani n.k