Fedha mpya haziendani na mfumo wa muamala wa TANZANIA

Kuna vikao kati vya ma-CEOO wa mabenki na uongozi wa BOT nini kifanyike ili fedha walizotengeneza ziweze kutumika katika miamala yetu yaani ATM machines. Fedha hizi mpya ni tofauti kwa size na za zamani. Swali ni Je kama hizo fedha hazita fit kutumika/wa na ATMs zetu zitarudiwa kuchapishwa? au watang'oa ATMs zote na kuweka mpya?

Nitajitahidi kuwapa update za noti mpya kadiri nitakavyozipata.

UPDATE

BOT walikubaliana na mabenki nchini kutoa chip maalumu zitakazo fungwa kwenye ATM ili ziendane na size ya noti mpya. Kampuni inayosambaza na kufunga hizo chip tutaifahamu hivi punde.

napenda kuamini kuwa BOT wakati wanatengeza noti mpya walitakiwa kujua noti lazima ziwe compatible na ATM, hivyo nahizi kuna kamchezo makusudi kamefanywa na watu fulani wakijua watanufaika baadae. chunguza kwa undani pia kampuni itakayotoa hizo chip, nani atagharamikia
 
Mimi hili la kutoa chipi bado siliamini, mi nachojua , Tufanye ukitaka kuweka fedha zenye size mpya kwenye ATM unachotakiwa kufanya kuset kwenye software ya ATM, na kubadilisha size ya ndani ya CASSETI tu, ndo huo utaratibu Hakuna kingine chochote kitakochofanywa cause Kama size ya noti inafanana ya USD, Na ATM hizi ndizo pia zinatumiwa MAREKANI ,sasa kwa nini ATM zetu ndo zifungwe hiyo chipi.?
 
NCR.jpg

Hiyo hapo juu ni ATM ilioyetengenezwa na NCR, kampuni ambayo inatengeneza asilimia zaidi ya 70% ya atm zinazotumika duniani, sasa swali kama hiyo ATM hapo juu inatumika marekani kutoa usd, kwa nini ishindikane tanzania kwa hizo noti zetu mpya ambazo ni sawa na size ya DOLLA? au ATM za marekani nazo zimefungwa hiyo CHIPI?
 
crap! Crap!! Crap!! Crap!!

ni ufinyu tu wa mawazo ya kiufundi tatizo wabongo tumekariri,
linawezekana na limefanyika bila cost yeyote labda bot waseme wanataka kuingiza ulaji sawa ila linawezekana bila ubishi wowote!
 
Back
Top Bottom