Fedha mpya haziendani na mfumo wa muamala wa TANZANIA

asante nguli kwa taarifa. hapo lazima kuna biashara imeishafanyika. OMG, hivi sasa mwisho wa haya ma-minyororo ya ufisadi utakuwa lini? jamani mie nimechoka hata kusikia sasa sitaki tena, khaaa! ujinga gani huu? halafu waziri mwenyewe wa fedha karudishwa yuleyule ili akamilishe kazi aliyoianza! gavana utasikia kesho kabomoa nyumba yake anajenga nyingine ya mabilioni!! jamani TZ tunatia huruma jamani mpaka basi!
 
Well inawezekana kukawa kuna uzembe. Lakini tatizo ni kuwa hawakuwataarifu wenye mabenki au wametengeneza size tofauti na za zamani? Kwanini unadhani BOT ndio inawajibika kununua au kutengeneza mashine ili ziendane na hiyo pesa? Wenye mabenki wanahitaji kufuata hitajio la nchi au nchi inahitaji kufuata hitajio la mabenki? Naomba nieleweke nahitaji nguvu katika sekta binafsi lakini maswali haya niliyouliza yanatufanya tufikiri responsibly zaidi.

ATM machines zinatumika nchini kwa miaka mingi sasa. Kwa maoni yangu ni wajibu wa BoT kila wanapotaka kuchapisha noti mpya kuhakikisha noti hizo mpya zitaweza kutumia hizo ATM machines zilizokuwepo na siyo kuwataka mabenki wabadilishe ATM machines zao kila mara kunapokuwa na mabadiliko ya pesa.

 
ATM machines zinatumika nchini kwa miaka mingi sasa. Kwa maoni yangu ni wajibu wa BoT kila wanapotaka kuchapisha noti mpya kuhakikisha noti hizo mpya zitaweza kutumia hizo ATM machines zilizokuwepo na siyo kuwataka mabenki wabadilishe ATM machines zao kila mara kunapokuwa na mabadiliko ya pesa.

Kuna mchangiaji hapo juu kaeleza clearly kabisa kwamba wachapisha notes woote wanajua size ya ATM zote duniani maana ni kama simcard vile. Kwahiyo taarifa hii tuitazame kwa makini.
 
Kuna mchangiaji hapo juu kaeleza clearly kabisa kwamba wachapisha notes woote wanajua size ya ATM zote duniani maana ni kama simcard vile. Kwahiyo taarifa hii tuitazame kwa makini.

Basi kama ni wao wabebeshwe gharama za kufanya adjustments za aina yoyote ile maana ni makosa yao. Tusubiri kusikia zaidi kilichojiri kwenye hili sakata.
 
Huu ni wizi, watatuambia noti ndogo inaenda kurekebisha halafu wajanja wanaiingiza iliyopo, muda si mwingi tutakuta pesa tofauti kwenye mzunguko. Hii haina tofauti na watengenezaji pesa bandia halafu wanaziingiza benki.
 
swala ni gharama ya kubadili cash canisters,ili noti ndogo zikae sawa,hili ni dili la mtu,kwani kumbuka noti mpya zina size sawa na dola. itabidi benki zote zinunue kwa supplier mmoja wa hizo canisterthen gharama ya benki will be passed on to mtanzania,same cost like LUKU with richmond dowanz or euwra ktk bili ya petrol+luku so tarajia gharama za kutumia ATM zitaongeka from 300 kuwa kitu kama 600 au hata 1000 per transaction
 
Jamani hebu tuache uzushi! Ukiangalia noti zetu zote haziko kwenye kipimo kimoja yaani angalia ukubwa wa noti ya shilingi 1000, ya 2000, ya 5000 na 10,000 zote zinatofautiana lakini zote zinatolewa na mashine hiyo moja. Hebu tuambie ni wapi ulienda ukakuta kila noti inatolewa na mashine tofauti tofauti? Wana-JF hivi kweli tunakazana kuwalaumu BOT kwa ajili ya thread ya kizushi kama hiyo? Au kuna mtu gani hajawahi kuchukua shilingi 1,000 au 2,000 kwenye ATM? Mimi sitaki kuamini kwamba safari hii BOT wametengeneza noti ndogo kama stemp (hapo litakuwa jambo jingine litakalohitaji maelezo ya kina)!!

Na suala la kubadili noti safari hii mimi sioni kama ni jambo la uzembe! Nawaunga mkono kwa asilimia zote, hivi hatuoni ajabu kuendelea kutumia noti zenye saini za watu kama akina B.P. Mramba na D. Balali? Watu wanaweza kuuliza sasa tutakuwa tunatengeneza noti kila tunapobadili magavana na mawaziri wa fedha? Labda huu ndo uwe mjadala wa kuona nini kifanyike ili kuzuia hali hiyo isiendelee kutokea. Pengine tunaweza kuwa na Saini ya mtu mmoja maalum (sema kama vile Mwl. Nyerere) ambaye hata akifa iendelee kuwepo kwenye noti zetu na hili linapaswa kuzungumzwa kwenye Katiba yetu mpya ili kuzuia utengenezaji holela wa fedha zetu. Hivyo wana-JF nasema tena naunga mkono wazo hili la kubadili noti ili tusiendelee kuona saini za akina Mramba na Balali (Zinatuchefua bure).

Wazo la nani agharamie hayo marekebisho ya ATMs (kama kweli kuna haja ya kurekebisha), hiyo itakuwa gharama ya mwenye biashara na wala hauwezi ukawa mzigo wa BOT. Ni wewe mwenyewe ndo unataka biashara yako iende vizuri na kwa ufanisi hivyo lazima uingie gharama. Endapo watatudanganya kwamba BOT imegharamia marekebisho hayo tutajua ni aina nyingine ya ufisadi!!!!!!
 
Job K shukran mi napenda wajengaji hasa katika maswala ya msingi yanayo leteleza chuki na hasira kwa wenyenchi.
 
I think this is true!
Jamani hebu tuache uzushi! Ukiangalia noti zetu zote haziko kwenye kipimo kimoja yaani angalia ukubwa wa noti ya shilingi 1000, ya 2000, ya 5000 na 10,000 zote zinatofautiana lakini zote zinatolewa na mashine hiyo moja. Hebu tuambie ni wapi ulienda ukakuta kila noti inatolewa na mashine tofauti tofauti? Wana-JF hivi kweli tunakazana kuwalaumu BOT kwa ajili ya thread ya kizushi kama hiyo? Au kuna mtu gani hajawahi kuchukua shilingi 1,000 au 2,000 kwenye ATM? Mimi sitaki kuamini kwamba safari hii BOT wametengeneza noti ndogo kama stemp (hapo litakuwa jambo jingine litakalohitaji maelezo ya kina)!!

Na suala la kubadili noti safari hii mimi sioni kama ni jambo la uzembe! Nawaunga mkono kwa asilimia zote, hivi hatuoni ajabu kuendelea kutumia noti zenye saini za watu kama akina B.P. Mramba na D. Balali? Watu wanaweza kuuliza sasa tutakuwa tunatengeneza noti kila tunapobadili magavana na mawaziri wa fedha? Labda huu ndo uwe mjadala wa kuona nini kifanyike ili kuzuia hali hiyo isiendelee kutokea. Pengine tunaweza kuwa na Saini ya mtu mmoja maalum (sema kama vile Mwl. Nyerere) ambaye hata akifa iendelee kuwepo kwenye noti zetu na hili linapaswa kuzungumzwa kwenye Katiba yetu mpya ili kuzuia utengenezaji holela wa fedha zetu. Hivyo wana-JF nasema tena naunga mkono wazo hili la kubadili noti ili tusiendelee kuona saini za akina Mramba na Balali (Zinatuchefua bure).

Wazo la nani agharamie hayo marekebisho ya ATMs (kama kweli kuna haja ya kurekebisha), hiyo itakuwa gharama ya mwenye biashara na wala hauwezi ukawa mzigo wa BOT. Ni wewe mwenyewe ndo unataka biashara yako iende vizuri na kwa ufanisi hivyo lazima uingie gharama. Endapo watatudanganya kwamba BOT imegharamia marekebisho hayo tutajua ni aina nyingine ya ufisadi!!!!!!
 
swala ni gharama ya kubadili cash canisters,ili noti ndogo zikae sawa,hili ni dili la mtu,kwani kumbuka noti mpya zina size sawa na dola. itabidi benki zote zinunue kwa supplier mmoja wa hizo canisterthen gharama ya benki will be passed on to mtanzania,same cost like LUKU with richmond dowanz or euwra ktk bili ya petrol+luku so tarajia gharama za kutumia ATM zitaongeka from 300 kuwa kitu kama 600 au hata 1000 per transaction

Asante kwa maelezo ndg yangu wewe unaonekana unaelewa,.
 
Jamani hebu tuache uzushi! Ukiangalia noti zetu zote haziko kwenye kipimo kimoja yaani angalia ukubwa wa noti ya shilingi 1000, ya 2000, ya 5000 na 10,000 zote zinatofautiana lakini zote zinatolewa na mashine hiyo moja. Hebu tuambie ni wapi ulienda ukakuta kila noti inatolewa na mashine tofauti tofauti? Wana-JF hivi kweli tunakazana kuwalaumu BOT kwa ajili ya thread ya kizushi kama hiyo? Au kuna mtu gani hajawahi kuchukua shilingi 1,000 au 2,000 kwenye ATM? Mimi sitaki kuamini kwamba safari hii BOT wametengeneza noti ndogo kama stemp (hapo litakuwa jambo jingine litakalohitaji maelezo ya kina)!!

Na suala la kubadili noti safari hii mimi sioni kama ni jambo la uzembe! Nawaunga mkono kwa asilimia zote, hivi hatuoni ajabu kuendelea kutumia noti zenye saini za watu kama akina B.P. Mramba na D. Balali? Watu wanaweza kuuliza sasa tutakuwa tunatengeneza noti kila tunapobadili magavana na mawaziri wa fedha? Labda huu ndo uwe mjadala wa kuona nini kifanyike ili kuzuia hali hiyo isiendelee kutokea. Pengine tunaweza kuwa na Saini ya mtu mmoja maalum (sema kama vile Mwl. Nyerere) ambaye hata akifa iendelee kuwepo kwenye noti zetu na hili linapaswa kuzungumzwa kwenye Katiba yetu mpya ili kuzuia utengenezaji holela wa fedha zetu. Hivyo wana-JF nasema tena naunga mkono wazo hili la kubadili noti ili tusiendelee kuona saini za akina Mramba na Balali (Zinatuchefua bure).

Wazo la nani agharamie hayo marekebisho ya ATMs (kama kweli kuna haja ya kurekebisha), hiyo itakuwa gharama ya mwenye biashara na wala hauwezi ukawa mzigo wa BOT. Ni wewe mwenyewe ndo unataka biashara yako iende vizuri na kwa ufanisi hivyo lazima uingie gharama. Endapo watatudanganya kwamba BOT imegharamia marekebisho hayo tutajua ni aina nyingine ya ufisadi!!!!!!

Mtiririko mzuri ila mzee kuhusu vikao vya noti mpya usibishe kabisa ni ukweli mtupu naokueleza na kama unataka kuamini nacho kwambia ukienda kwenye ATM kwa sasa haza zilizoko dsm utaona inayotoa noti mpya ni 1 tu kutokana na adjustment ambayo mafundi wamefanya
 
Hii inanikumbusha wakati wa Celtel kuja Zain walipaka rangi magari alafu hatiame wakasema rangi imekosewa ikabidi warudie.
Miradi ya watu iyo jamani.
Initially lengo ilikuwa kuphase out noti fake ambazo zilitengenezwa wakati wa uchaguzi so wakakurupuka na huo mradi,wahusika wa project watakuwa very myopic ila siwalaumu ni sababu ya haraka ya kulifanya ilo esp political pressure
 
Mkuu nadhani si lazima watengeze pesa upya. hapo ni kuangalia cost-benefit analysis. Kwani Tanzania kuna ATM ngapi? Gharama ya kuadjust hizo ATM zinafanana na kuchapisha notes? Wanaweza kuziadjust na kazi ikaendelea.

At whose cost?
 
Wala hakuna tatizo la fedha mpya kutumika katika ATM, kwani unapopata fedha yenye size tofouti, ni kubadilisha saizi tu ya casseti, na kuweka software mpya kwenye ATM, ni hilo tu na wala HAITASUMBUA SANA.
 
Duniani kote, ni kweli wanatumia ATM kutoa pesa za aina mbalimbali. Lakini je, kuna ATM gani bongo inatoa fedha za kigeni? Maana wageni wamekuwa wakilalamika kuwa ukifika Tanzania kama unahitaji foreign currency lazima ubadili kwenda kwenye Tshs. Nchi nyingine machine za sehem za kusafiria kama airport zina options za currency tofauti.
Ukweli ni kwamba BOT wamebadili size ya note ili ziweze kuhifadhika zaidi na kuachana na size zile za zamani. Lengo lao lilikuwa jema ila walitakiwa wawataarifu wenye mabenki juu ya hili na huenda wangekuwa wamejiandaa zaidi. Kwa nchi yetu sekta binafsi imekuwa ikidharaulika lakini ingepewa nafasi inayostahili huenda uchumi wetu ungefika mbali zaidi.
Kuhusu ubwege wa serikali sina wasiwasi nao, wamezowea na wameshatuzowea, lakini hili la kuwa kuna nchi ambazo zina "option" za "currency" tofauti nina wasiwasi nalo. Nimewahi kuona hata mashine unazoweza kununua dhahabu moja kwa moja, lakini hilo la currency bado ingawa sipingi.
Ninavyoelewa ni kuwa katika nchi nyingi (siwezi kusema zote, sina hakika) kubadilisha fedha za kigeni ni benki na vituo vyengine vya ubadilishaji, ambako mgeni hutakiwa kutoa passport yake ili kudhibiti uvushaji wa pesa haramu. Mgeni halazimishwi kubadilisha fedha za nchi husika bali hufanya hivyo kwa hiari yao (ni faida kwao kwa sababu pesa zao zina thamani kubwa kuliko zetu za madafu).
 
Wala hakuna tatizo la fedha mpya kutumika katika ATM, kwani unapopata fedha yenye size tofouti, ni kubadilisha saizi tu ya casseti, na kuweka software mpya kwenye ATM, ni hilo tu na wala HAITASUMBUA SANA.

soma update yangu huaamni fwatilia mwenyewe
 
wakuu si naskia mzigo wa noti mpya ulipigwa pale airport? tena mzigo wa kutosha
 
Back
Top Bottom