Kituko
JF-Expert Member
- Jan 12, 2009
- 9,555
- 9,330
Akijibu swali la Mwanachama mfu wa CCM (A, Lwaitama), Dr Slaa alisema, kisaikolojia hiyo ni hulka ya binadamu kuogopa asipokujua,
lakini ni kweli watu hawakujuhi huko?
Miongoni mwa sifa kuu za binadamu ni usahaurifu, na hiyo ndio inayompa matumaini makubwa sana binadamu ile hali ya kusahahu ikitokea basi kila kitu kinaonekana ni kawaida tu, na binadamu anaendelea kupambana na maisha yake mapya bila kumbukumbu ya yale ya zamani. sifa nyingine kuu ni hofu, na hii hofu yaweza kuwa ni yako mwenyewe (personal) ama ya kupandikizwa (kutiwa hofu)
Swali ni wapi huko kusikojulikana?
Asilimia karibu ya hamsini ya Watanzania wanakujua huko Dr Slaa anapopazungumzia ila wamesahau na kuona hali iliyopo ni ya kawaida tu, namaanisha wamekusahahu kule kulikokuwa na Elimu ya Bure, Matibabu ya Bure, Heshima kwa UTU wa mtu, utawala wa kuheshimu katiba, kuheshimu mali za umma pamoja na rasilimali zake, kule kulikokuwa na Miiko ya uongozi na kule kulikokuwa na Watanzania waliokuwa tayari kuitetea nchi yao (Kimichezo, sanaa na hata kijeshi) ni usahaurifu tu. lakini Dr Slaa anawakumbusha na yupo tayari kuwarudisha kule kwenye nchi ile ya Asali na Maziwa (Tanzania), keshajitoa muhanga na kisha onyesha nia na njia ya kupitia kurudi kule, hauna haja ya kupigana wala kumwaga damu ili Dr Slaa akurudishe kule, anachohitaji kwako ni wewe kuweka (√) tu kwenda kwake
Lakini pia kuna karibu ya aslimia hamsini ya Watanzania hawakujuhi kule anapopazungamzia Dr Slaa, hawajawahi kuiona ile Tanzania, wako tayari kwenda kule lakini wanatatizo la Hofu, wanaogopa kwa sababu wametiwa uoga nafsini mwao kuwa hicho kitu akiwezekani, Dr Slaa atapata wapi Pesa? Na wameambiwa hiyo nchi anayoizungumzia Dr ni ya kufikirika tu, haipo, yaani wanaambiwa na Viongozi waliopo kwamba Utawala bora (usio wa kirafiki, Kindugu, Kikabila, Kidini) hauwezekani Tanzania, Ndugu zanguni hakuna vita itakayotokea kwa wewe kuibadilisha hii serikali iliyopo, kama una hofu na hayo waulize wale waliokuwepo kwenye nchi ile watakwambia inawezekana na wao wameshawahi kushuhudia
Nchi ilikuwa na watu wachache na rasilimali chache na zilitumika kwa faida ya Watanzania wote, sasa nchi ina watu wengi na ina rasilimali nyingi mno lakini zinatumiwa na watu wachache,
Dr Slaa anataka hizo rasilimali (keki) ya Taifa tugawane wote (katika uduma muhimu za kibinadamu) na kila raia awe katika hali ya kiutu
Wakati naendelea kuandika nasikia sauti ya Nyerere ikitukumbusha it can be done-play your part
Kwa kuweka √ kwenda kwa Dr Slaa hiyo 31 October 2010, na utakuwa umeweka historia katika nchi hii, utakuwa umeshiriki katika ukombozi wa kuirudisha Tanzania kwa Watanzania na kwa faida ya Watanzania wa sasa na wale wajao
lakini ni kweli watu hawakujuhi huko?
Miongoni mwa sifa kuu za binadamu ni usahaurifu, na hiyo ndio inayompa matumaini makubwa sana binadamu ile hali ya kusahahu ikitokea basi kila kitu kinaonekana ni kawaida tu, na binadamu anaendelea kupambana na maisha yake mapya bila kumbukumbu ya yale ya zamani. sifa nyingine kuu ni hofu, na hii hofu yaweza kuwa ni yako mwenyewe (personal) ama ya kupandikizwa (kutiwa hofu)
Swali ni wapi huko kusikojulikana?
Asilimia karibu ya hamsini ya Watanzania wanakujua huko Dr Slaa anapopazungumzia ila wamesahau na kuona hali iliyopo ni ya kawaida tu, namaanisha wamekusahahu kule kulikokuwa na Elimu ya Bure, Matibabu ya Bure, Heshima kwa UTU wa mtu, utawala wa kuheshimu katiba, kuheshimu mali za umma pamoja na rasilimali zake, kule kulikokuwa na Miiko ya uongozi na kule kulikokuwa na Watanzania waliokuwa tayari kuitetea nchi yao (Kimichezo, sanaa na hata kijeshi) ni usahaurifu tu. lakini Dr Slaa anawakumbusha na yupo tayari kuwarudisha kule kwenye nchi ile ya Asali na Maziwa (Tanzania), keshajitoa muhanga na kisha onyesha nia na njia ya kupitia kurudi kule, hauna haja ya kupigana wala kumwaga damu ili Dr Slaa akurudishe kule, anachohitaji kwako ni wewe kuweka (√) tu kwenda kwake
Lakini pia kuna karibu ya aslimia hamsini ya Watanzania hawakujuhi kule anapopazungamzia Dr Slaa, hawajawahi kuiona ile Tanzania, wako tayari kwenda kule lakini wanatatizo la Hofu, wanaogopa kwa sababu wametiwa uoga nafsini mwao kuwa hicho kitu akiwezekani, Dr Slaa atapata wapi Pesa? Na wameambiwa hiyo nchi anayoizungumzia Dr ni ya kufikirika tu, haipo, yaani wanaambiwa na Viongozi waliopo kwamba Utawala bora (usio wa kirafiki, Kindugu, Kikabila, Kidini) hauwezekani Tanzania, Ndugu zanguni hakuna vita itakayotokea kwa wewe kuibadilisha hii serikali iliyopo, kama una hofu na hayo waulize wale waliokuwepo kwenye nchi ile watakwambia inawezekana na wao wameshawahi kushuhudia
Nchi ilikuwa na watu wachache na rasilimali chache na zilitumika kwa faida ya Watanzania wote, sasa nchi ina watu wengi na ina rasilimali nyingi mno lakini zinatumiwa na watu wachache,
Dr Slaa anataka hizo rasilimali (keki) ya Taifa tugawane wote (katika uduma muhimu za kibinadamu) na kila raia awe katika hali ya kiutu
Wakati naendelea kuandika nasikia sauti ya Nyerere ikitukumbusha it can be done-play your part
Kwa kuweka √ kwenda kwa Dr Slaa hiyo 31 October 2010, na utakuwa umeweka historia katika nchi hii, utakuwa umeshiriki katika ukombozi wa kuirudisha Tanzania kwa Watanzania na kwa faida ya Watanzania wa sasa na wale wajao