Zuia Sayayi
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 841
- 133
Baada ya miezi ya kujaribu kufungua (bila kufuta taarifa) simu mbili aina ya iPhone [ iPhone 5 na iPhone 7 ] zilizokua zikitumiwa na gaidi aitwaye Syed Farook (21),
Hatimaye FBI yafanikiwa kuingia kwenye iPhone iliyokuwa ikitumiwa na Syed Farook aliyehusika na tukio la kuwamiminia risasi na kuwaua watu 14 na kujeruhi wengine 22 pale Pensacola Naval mnamo Desemba 2019 akiwa yeye na mkewe (Tashfeen Malik ), Wataalam wa computer wa FBI walifanikiwa kufanya hivyo bila msaada wa Apple, lakini Wakili Mkuu wa Serikali William Barr na mkurugenzi wa FBI Christopher Wray wote walionyesha kufadhaishwa sana na kampuni ya Apple kwenye mkutano na waandishi wa habari Jumatatu asubuhi.
FBI inadai alikuwa na uhusiano na shirika la kigaidi al-Qaeda. Ma engineer wa FBI
Bado, maafisa wote wawili wanasema kwamba usimbuaji wa vifaa alivyotumia gaidi Huyo ulizuia uchunguzi. "Shukrani kwa kazi kubwa ya FBI - na hakuna shukrani kwa Apple - tuliweza kufungua simu za Alshamrani," alisema Barr, ambaye alilalamika miezi hiyo na "pesa nyingi za walipa kodi" zilizotumika kufungua vifaa hivyo
FBI ilitumia mbinu mbali mbai kupata data kwenye iPhone zilizokua zikitumiwa na gaidi huyo (Syed Farook), ambaye alikufa na mkewe katika vita vya bunduki na polisi baada ya kuwauwa watu 14 huko San Bernardino, California, mnamo Desemba.
NOTE: Katika majibizano ya Tukio lile kati ya Polisi na magaidi hao, polisi waliokota simu hizo eneo la tukio ambapo FBI waliwaomba kampuni ya apple kuzifungua simu hizo kwa sababu zilikua zimefungua kwa namba za siri, lakini Apple walikataa kufungua simu zile na kusema ni kinyume cha sheria za usiri na faragha za mteja(mtumiaji),
Syed Farook aliwahi kuwaua wanamaji watatu wa Amerika katika KISIWA cha Naval Air Station Pensacola huko California mnamo Desemba na kujeruhi wengine wanane. Alikuwa mwanachama wa jeshi la Saudi na alikuwa kwenye uwanja wa mafunzo huko Amerika.
SOURCE
foxnews
theVerge