Fatuma Karume aambiwe sheria za Asili (za Mungu) hazipitwi na wakati

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,864
FATUMA KARUME LAZIMA UJUE SHERIA ZA ASILI(ZA MUNGU) HAZIPITWI NA WAKATI.

Kwa Mkono wa, Robert Heriel.

Tahadhari; Andiko hili huenda likawa limetumia lugha Kali. Ikiwa unatatizo na Lugha Kali na zinakudhuru Kwa namna moja ama nyingine basi nakusihi ishia hapahapa kusoma. Na endapo umekaidi, ukasoma basi nisihusike na madhara yoyote kwani umeona utayamudu.

Niite Taikon wa Fasihi, Kuhani katika Hekalu Jeusi.

Mimi sio mwanasheria lakini sheria ipo damuni. Ipo damuni kwa sababu ninapenda haki. Yeyote apendaye haki sheria imo damuni mwake. Hata hivyo haki asili yake ni ipi. Bila Shaka haki asili yake ni Kwa MUNGU Mkuu muumba wa vyote katika yote. Yeyote Yule apendaye haki yu ampenda Mungu. Na yeyote ampendaye MUNGU yu apenda Haki.
Haki na Mungu havitenganishiki.
Ili haki ifanyike sharti iwepo sheria, hata hivyo tunafahamu kuwa sheria yafaa mtu au vitu zaidi ya mmoja/kimoja ili kujenga mahusiano MAZURI.

Haki sharti iandane na wajibu, na wajibu upo chini ya sheria. Kila kimoja chamtegemea mwenziwe.

Zipo haki jumuishi,
Zipo haki za makundi,
Halikadhalika zipo sheria jumuishi na sheria za makundi.

Zipo sheria za wakati Fulani,
Zipo sheria za milele.

Zipo sheria za Asili (sheria za Mungu)
Zipo sheria za binadamu kutengeneza.

Mwanasheria yeyote ili awe bingwa WA kiwango cha juu kabisa cha kimataifa ni lazima awe anaujuzi mkubwa wa sheria za ASILI (sheria za MUNGU) ambazo ndizo sheria Mama.

Hata mahakamani, mwanasheria au wakili au hakimu, au Jaji, Kama hajabobea katika sheria za Asili(sheria za MUNGU) hawezi kuwa mzuri au mbobevu katika sheria za kidunia.

Siri kubwa ya wanasheria WA ngazi za kimataifa ni hiyo. Huwezi ijua sheria za kibinadamu kabla hujaijua sheria ya Asili(Sheria mama).
Mahakamani ni rahisi kushindwa na mtu anayejua sheria ya Asili(sheria za Mungu) kuliko mtu anayejua sheria hizi walizotunga maprofesa wa Kerege.

Profesa mi mtu Kama watu wengine, tena wengine uwezo wao unaweza ukawa juu Kwa Zama zao lakini Kwa Zama zinazokuja wakaonekana walikuwa vilaza.

Sishangai kusikia sheria zinapitwa na wakati, ni kweli sheria za maprofesa wa Kerege lazima zipitwe na wakati Kwa sababu ni Binadamu, wao huwa vipanga Kwa wakati wao lakini nyakati zikipita zikaja nyakati zingine huonekana walikuwa vilaza tuu.

Katika Dini sheria za binadamu huitwa MAPOKEO Ambayo hutokana na Mila, desturi, miiko na maadili ya jamii moja kwenda nyingine.

Tatizo kubwa linalotokea katika Zama hizi na huenda lilishawahi kutokea ni baadhi ya wanasheria kuchanganyikiwa Kwa Uelewa mdogo au kuchanganywa na mambo waliyoyasoma ambayo yamewapumbaza mpaka wameshindwa kutofautisha mambo ya Asili Vs Man-made Things.

Fatma Karume lazima urudi shule ufundishwe kutofautisha Natural Vs Artificial. Sheria unazofundishwa Kwenye vyuo vya kidunia zote ni Artificial Laws ambazo baadhi yake zimerudufiwa na kuboreshwa kutoka katika Natural laws.

Sheria za Asili hazibadiliki sijui hujui hili au unafanya ukaidi.

Ndio maana Dada yangu Fatma huwezi kulala na mtoto wako WA kumzaa, au kulala na Mzazi wako ati Kwa sababu kuna haki ya Faradha iliyobainishwa kwenye Artificial Laws zilizotengenezwa na binadamu.

Ishu ya ushoga na usagaji kumsingi hata angekuja Profesa wa Harvard akashusha utafiti kuwa haina madhara na inafaida, Kwa Sisi tunaojua sheria halisi, tutamuona profesa huyo kajikoroga na kachanganyikiwa kitaaluma.

Mwanasheria ili aheshimike, popote pale Duniani lazima ajikite katika kuzitetea na kuzifasiri sheria za Asili(Sheria za Mungu),
Lakini ili Mwanasheria awe hopeless na useless anapaswa aende kinyume na sheria za Asili. Ataonekana kachanganyikiwa na Hana maana Yeyote.

Sheria za Asili zinazohusu matumizi ya miili yetu zinakataza mwanaume kulala na Mwanaume mwenzake(kufirana) Kama anavyolala na Mwanamke, pia zinakataza mwanamke kulala na Mwanamke mwenzake(kusagana) Kama anavyolala na Mwanaume.

Pia sheria za Asili zinakata mwanaume(mume) kutumia uchi wa nyuma(mkundu) Kwa mkewe.
Hata sheria za kibinadamu hata hapa nchini zinakataza mume kumfira mkewe, na adhabu yake ni kubwa.

Sheria za Asili zinakataza, mtu kutokulala na mnyama Kama alalavyo na binadamu mwenzake.

Sheria za Asili zinakataza, mtu kutumia kiumbe kingine kujifanyisha mapenzi, mathalani kutumia sex machine, matango, Ndizo, Vibomba.

Sheria za Asili zinakataza, mtu kulala na Mama au Baba yake, kulala na Mkwe WA kiume na wakike, kulala na ndugu wa damu moja, kulala na Mke au mume wa ndugu yako wa damu, Kulala na Mke au mume wa Baba au mama Yako. Miongoni mwa sheria nyingi.

Sheria hizi ni Mama.
Mtu Yeyote aendaye kinyume na sheria hizi mara nyingi ni Mpumbavu.

Sheria za Mungu hazipitwi na wakati Kwa maana ni Asili. Asili tumeikuta na tutaiacha.

Dada Fatuma Karume asije akajichanganya kuwa kusoma vielimu vyake vya maprofesa wa Kerege akadhani atadhani atamzidi maarifa Mungu aliyeweka Sheria za ASILI ambazo hazibadiliki.

Asije akadhani na kufikiria kuwa kuwa msomi au kuiga Wazungu ndio ati kuendana na wakati huo ni upumbavu.

Kwanza Neno lenyewe wakati ni neno linalotawaliwa na sheria za Asili na wala sio Artificial laws.

Dada Fatuma Karume nakusihi usijidharau watu wakakudharau, elimu yako haina maana yoyote Kama utakuwa mweupe kwenye masuala ya elimu ya kiroho, na utajichoresha Kwa watu ambao hata hawajafika Darasa la pili Kwa elimu dunia.

Kuzikataa sheria za Asili na kuziona zimepotwa na wakati ilhali wakati ni Asili ya sheria hizo ni Dalili ya upumbavu na kuzidiwa akili mpaka na wanyama.

Mwisho;
Niwasihi wanasheria, mahakimu, majaji, mawakili, makadhi, watoa maamuzi wote, waalimu na watu wote wenye nafasi ya kufundisha jamii kuwa Lazima tuzingatie elimu ya Asili na sheria za Asili ndipo tuzingatie hizi zetu za Profesa wa Kerege.

Ati Mimi Taikon miaka kumi ijayo nimemaliza kusoma uprofesa wa sheria, ati nawaambia sheria inayomzuia mtu kumuoa Mama yake imepitwa na wakati nanyi mnaniunga Mkono kisa ni profesa 😃😃 huo si ufala na ninyi ni mafala.

Iwe Mimi au wewe au Yule bila kujali nafasi yake, hata asome mpaka apate kibiyongo, hata asome mpaka macho yazibe Avae miwani ya darubini, Kama atavunja kanuni za Asili jua ni MPUMBAVU TUU.

NAa watu wote wamuite Mpumbavu.

Ati kisa Taikon nimeenda Kusoma Ulaya, au nimekuwa Rais wa nchi hii au ni mtoto wa Rais ndio nivunje kanuni za Mungu(Asili) nanyi mnifuate kisa ninasifa tajwa hapo, ninyi mtakuwa wapumbavu na Mimi nitakuwa Mpumbavu tuu.

Hakuna mtu anayeweza kuvunja sheria za Asili akabaki SALAMA.

Nipumzike sasa

Ni Yule Mtibeli kutoka Nyota ya Tibeli yenye mbawa mbili irukayo huku na Huku.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kerege.
 
DINI: Kuhusu ushoga, Yesu Kristo angelikujibu hivi "Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe."

MILA NA DESTURI: Lakini pia mtazamo wa kitamaduni, Tanzania tumekuwa na mashoga hata kabla ya wazungu ama waarabu kuja, tunaishi nao, wengi wamekuwa wakijificha, na wengi hulazimika kuoa ili kuificha jamii uhalisia wao.

PIA KUNA WATU WENGI TU, Huwaingilia wake zao kinyume na maumbile.

MWACHENI MUNGU MWENYEWE AHUKUMU.
 
Ulaya na Marekani hawana hizo sheria za asili ulizosema na ndiyo wanapigania haki za mapenzi ya jinsia moja na wao ndiyo walikuambia kuwa kuna MUNGU
Ulaya ipo hiyo Sheikhe?

😃😃

Unafikiri Kabla ya wao kuja Sisi Waafrika hatukuwa na Mungu??

Au unataka elimu ya historia kidogo
 
DINI: Kuhusu ushoga, Yesu Kristo angelikujibu hivi "Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe."

MILA NA DESTURI: Lakini pia mtazamo wa kitamaduni, Tanzania tumekuwa na mashoga hata kabla ya wazungu ama waarabu kuja, tunaishi nao, wengi wamekuwa wakijificha, na wengi hulazimika kuoa ili kuificha jamii uhalisia wao.

PIA KUNA WATU WENGI TU, Huwaingilia wake zao kinyume na maumbile.

MWACHENI MUNGU MWENYEWE AHUKUMU.

Unaweza nambia shoga Kwa kilugha chenu anaitwaje??

Kama hujui nafikiri utajua kuwa kabla ya Mzungu kuja hapakuwa na ushoga hapa Afrika.

Yesu alifuata sheria za Asili,
Yesu kusema hivyo hayo ni maoni yake hatabadilishi hata kifungu kimoja cha sheria za Asili.

Lazima ujue kutofautisha sheria na Mafunzo, na maoni
 
Vyovyote iwavyo, Ila sheria za Asili hazituruhusu
Wote wanaojadili mambo ya faragha huwa nawaona kama mapunguani.

Ushoga, ulawiti na lesbianism vilikuwepo, vipo na vitaendelea kuwepo haijalishi ni halali au ni haramu.

Kilichobadilika sasa hivi ni hawa watu kutafuta recognition.

Ila siku mapaa ya nyumba yakifunuliwa ghafla, ninyi mnoajifanya mnaandika naneno LAKI 5 kupinga haya mambo mtabaki na aibu.

Na kibaya zaidi wanahukumiwa mashoga wenyewe, wanaowafir*** hawaguswi, wao ni watakatifu.

Nchi hii unafiki umejita mizizi.
 
Simamia imani yako na fuata kile unachokiamini.Hili suala la ushoga kuna wakati naona kama linathibitisha unafiki wetu waswahili.
Madam tunaishi katika nchi ambayo haiendeshwi kidini basi hoja za wanaopigania uhuru wamashoga na wasagaji zitapata nguvu na kushinda muda si mrefu. Ni suala la muda tu! Leo mashoga wanajulikana wazi mpaka vijijini, vijiwe vyao vinajulikana, wanunuzi wa mashga wanajulikana.

Ukimwi ulivyoanza marehemu Dr.Remmy aliimba "mambo kwa sox)"akihimiza matumizi ya condom,wombo ulipigwa marufuku lakini baada ya muda tuligawa condom bure!

Simama na imani yako!
 
Wote wanaojadili mambo ya faragha huwa nawaona kama mapunguani.

Ushoga, ulawiti na lesbianism vilikuwepo, vipo na vitaendelea kuwepo haijalishi ni halali au ni haramu...
Kama yapo na yanakatazwa tunachokataza ni kuwazuia wanayotaka yawe Recognised na sheria za kidunia.

Kuhusu unafiki unaweza kuwa Sawa
 
Kama yapo na yanakatazwa tunachokataza ni kuwazuia wanayotaka yawe Recognised na sheria za kidunia.

Kuhusu unafiki unaweza kuwa Sawa
Mimi nadhani muhimu kulinda watoto na wanawake wanabakwa au kuingiliwa kinyume na maumbile bila ridhaa yao.

Ila kukaa kukaza shingo, unalingana na kitu amnacho hakina athari kwenye maisha yako ni kupoteza energy bure.

Jitu zima na akili zake timami limeamua kupelekewa moto.

Halifanyii kitandani kwako, chumbani kwako wala halikuombi pesa.

Unaumia nini wewe?
 
Back
Top Bottom