Fatma Ferej: Ni Faraja Kwetu Serikali Kupitia ATCL Kwenda Kuwachukua Watanzania Wenzetu

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
609
1,540
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa faraja hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwanusuru Watanzania walioko nchini Ukraine nchi ambayo iko vitani na Urusi.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema Serikali inachukua hatua za haraka kunusuru maisha ya Watanzania wapatao 300 pamoja na wanafunzi waliopo Ukraine.

Inakumbukwa kwamba likuwa ni ACT WAZALENDO iliyoibua hadharani haja na umuhimu wa Serikali kuchukua uongozi katika suala hilo la kuwachukua watanzania waliopo nchini Ukraine kwa kupitia nchi jirani.

Taarifa ya Naibu Msemaji Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Dahlia Majid iliyotolewa tarehe 25,Februari/ 2022 iliitaka Serikali ivae wajibu wake wa kulinda usalama wa raia wake kwa kuwaokoa Watanzania hao kwa sababu wajibu mkuu na wa kwanza kwa Serikali yoyote ni kulinda raia wake na mali zao popote walipo.

Baada ya Juhudi kubwa za Chama cha ACT Wazalendo kupitia Msemaji Wa Kisekta wa Mambo ya Nje, kuitaka Serikali ichukue hatua za makusudi kuwasaidia Watanzania Walioko Ukraine, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa taarifa na Muongozo wa namna unavyo shughulikia jambo Hilo!

Kuna taarifa kwamba kutakuwa na ndege ya ATCL itakayo kwenda kuwachukua watanzania wenzetu nchi ya Poland ,Romania na nchi zingine zinazopakana na Ukraine ambazo watanzania wapo Siku ya Tarehe 03.03. 2022.Na kuna mawasiliano yametolewa na Shirika la Ndege la Tanzania kupitia namba 0800110045 kwa mawasiliano zaidi ,hii kwetu sisi ni hatua njema.

Ila kuna changamoto ambayo ipo na tunaitaka Serikali kupitia Wizara ya mambo ya nje na Ubalozi wa Tanzania wa Poland uliopo Berlin kuchukua hatua za haraka ili kutatua changamoto hii.

Nchi ya Poland sasa inapokea watu wengi sana kutoka Ukraine,uwezo wao wa kuhudumia wote ni mgumu sana ingawa wanajitahidi sana .Na kwa kurahisisha hili ndio maana yeyoye anayeingia Poland anaulizwa mpakani kama ana ndugu wa kumpokea na atakayemsaidia na kumpa hifadhi na mahitaji.

Jambo la kuumiza watanzania wenzetu wanaoingia Poland na Romania mpakani hakuna utaratibu wowote uliowekwa na serikali yetu ya Tanzania ili kuwapokea hawa ndugu zetu aidha kuwapakia katika usafiri na kuwapa sehemu ya hifadhi na mahitaji yote hakuna utaratibu, watanzania wenzetu wanaoingia mpakani wanateseka hakuna utaratibu wowote uliowekwa.

Hivyo basi,tunashauri serikali ya Tanzania kupitia wizara ya mambo ya nje na Ubalozi wa Tanzania Poland uliopo Berlin iweke utaratibu wa haraka wa kuwapokea watanzania wanaoingia Poland na nchi zingine kama Romania ili kuwapa usafiri, hifadhi ya malazi,chakula na mahitaji ya msingi katika kipindi hiki ambacho serikali inajiandaa kwenda kuwachukua.

Lakini pia serikali iwasiliane na nchi za Afrika Mashariki na nchi kadhaa za Afrika ambazo nazo zinapokea watu wao ili pia wawapokee Watanzania popote wawaonapo na kuwapa hifadhi watanzania watakaopokelewa hapo mpakani kabla ya kuchukuliwa na kuletwa Tanzania.

ACT Wazalendo itaendelea kuwa sauti mbadala kwa kuwasema Watanzania katika masuala mbali mbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi

Fatma Fereji

Msemaji wa Kisekta wa Mambo wa Nje.

+255 777 424 390

28/03/2022

IMG-20220228-WA0014.jpg
 
Si mlipinga Magufuli aliponunua ndege?
Wapiiii kila ndege Alipiga panga 20%. Mbona akutuma msaada kwa watanzania waliotimuliwa msumbiji hapo jirani tu akabaki kuwatukana. Na cha ajabu msumbiji ilipopigwa na kimbunga akatafuta sifa za kijinga kumtuma kabudi kuwapa msaada haohao misumbiji iliyowatimua watanzania wenzake.

Pongez kwa mama kwa kuwasaidia watanzania wenzetu Ukraine.
 
Hiyo ndege itakwenda kuwachukulia mji gani? Anga yote ya UKRAINE ni no fly zone Hivyo pengine wajikusanye waende Poland ndio wakachukuliwe!!
 
Watawachukulia wapi
Hizi siasa hizi dah
Haya ngoja tuone ikirudi kama itarudi
 
Upinzani Tanzania hauhitaji kwenda Ulaya au Marekani kujifunza nini maana upinzani waende Zanzibar

Ulaya na Marekani likifika swala la national interest wanakuwa wamoja

Mfano swala la vita ya Russia na Ukraine wote wako kitu kimoja against Russia

Tanzania bara vyama vya upinzani pumbafu zao

Vyama vikuu upinzani Zanzibar vinajielewa kwenye national interest ya nchi ya Zanzib ar wanakuwa United kama wazanzibari bila kujali itikadi

Raisi Mwinyi alisema Serikali ya Zanzibar itafanya Juhudi kubeba walio Ukraine nk

Act wazalendo Zanzibar kupitia huyu mama wameunga mkono Juhudi hizo za serikali

Mipinzani bara iko kama mibwege hata tamko hamna wapo wapo tu wakati kule wako watoto na ndugu wa watu wa vyama vyote

Hopeless kabisa

Zanzibar hongereni CCM na upinzani kuwa united kwenye issue ya kitaifa inayohusu nchi yenu
 
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa faraja hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwanusuru Watanzania walioko nchini Ukraine nchi ambayo iko vitani na Urusi.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema Serikali inachukua hatua za haraka kunusuru maisha ya Watanzania wapatao 300 pamoja na wanafunzi waliopo Ukraine.

Inakumbukwa kwamba likuwa ni ACT WAZALENDO iliyoibua hadharani haja na umuhimu wa Serikali kuchukua uongozi katika suala hilo la kuwachukua watanzania waliopo nchini Ukraine kwa kupitia nchi jirani.

Taarifa ya Naibu Msemaji Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ndugu Dahlia Majid iliyotolewa tarehe 25,Februari/ 2022 iliitaka Serikali ivae wajibu wake wa kulinda usalama wa raia wake kwa kuwaokoa Watanzania hao kwa sababu wajibu mkuu na wa kwanza kwa Serikali yoyote ni kulinda raia wake na mali zao popote walipo.

Baada ya Juhudi kubwa za Chama cha ACT Wazalendo kupitia Msemaji Wa Kisekta wa Mambo ya Nje, kuitaka Serikali ichukue hatua za makusudi kuwasaidia Watanzania Walioko Ukraine, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa taarifa na Muongozo wa namna unavyo shughulikia jambo Hilo!

Kuna taarifa kwamba kutakuwa na ndege ya ATCL itakayo kwenda kuwachukua watanzania wenzetu nchi ya Poland ,Romania na nchi zingine zinazopakana na Ukraine ambazo watanzania wapo Siku ya Tarehe 03.03. 2022.Na kuna mawasiliano yametolewa na Shirika la Ndege la Tanzania kupitia namba 0800110045 kwa mawasiliano zaidi ,hii kwetu sisi ni hatua njema.

Ila kuna changamoto ambayo ipo na tunaitaka Serikali kupitia Wizara ya mambo ya nje na Ubalozi wa Tanzania wa Poland uliopo Berlin kuchukua hatua za haraka ili kutatua changamoto hii.

Nchi ya Poland sasa inapokea watu wengi sana kutoka Ukraine,uwezo wao wa kuhudumia wote ni mgumu sana ingawa wanajitahidi sana .Na kwa kurahisisha hili ndio maana yeyoye anayeingia Poland anaulizwa mpakani kama ana ndugu wa kumpokea na atakayemsaidia na kumpa hifadhi na mahitaji.

Jambo la kuumiza watanzania wenzetu wanaoingia Poland na Romania mpakani hakuna utaratibu wowote uliowekwa na serikali yetu ya Tanzania ili kuwapokea hawa ndugu zetu aidha kuwapakia katika usafiri na kuwapa sehemu ya hifadhi na mahitaji yote hakuna utaratibu, watanzania wenzetu wanaoingia mpakani wanateseka hakuna utaratibu wowote uliowekwa.

Hivyo basi,tunashauri serikali ya Tanzania kupitia wizara ya mambo ya nje na Ubalozi wa Tanzania Poland uliopo Berlin iweke utaratibu wa haraka wa kuwapokea watanzania wanaoingia Poland na nchi zingine kama Romania ili kuwapa usafiri, hifadhi ya malazi,chakula na mahitaji ya msingi katika kipindi hiki ambacho serikali inajiandaa kwenda kuwachukua.

Lakini pia serikali iwasiliane na nchi za Afrika Mashariki na nchi kadhaa za Afrika ambazo nazo zinapokea watu wao ili pia wawapokee Watanzania popote wawaonapo na kuwapa hifadhi watanzania watakaopokelewa hapo mpakani kabla ya kuchukuliwa na kuletwa Tanzania.

ACT Wazalendo itaendelea kuwa sauti mbadala kwa kuwasema Watanzania katika masuala mbali mbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi

Fatma Fereji

Msemaji wa Kisekta wa Mambo wa Nje.

+255 777 424 390

28/03/2022

View attachment 2134193
Wataingilia Anga lipi,
 
Rais wa Ukraine amechaguliwa kidemokrasia kupitia tume huru ya uchaguzi.
Upinzani Tanzania hauhitaji kwenda Ulaya au Marekani kujifunza nini maana upinzani waende Zanzibar

Ulaya na Marekani likifika swala la national interest wanakuwa wamoja

Mfano swala la vita ya Russia na Ukraine wote wako kitu kimoja against Russia

Tanzania bara vyama vyaupinzani pumbafu zao

Vyama vikuu upinzani Zanzibar vinajielewa kwenye national interest ya nchi ya Zanzib wanakuwa United kama wazanzibari bila kujali itikadi

Raisi Mwinyi alisema Serikali ya Zanzibar itafanya Juhudi kubeba walio Ukraine nk

Act wazalendo Zanzibar kupitia huyu mama wameunga mkono Juhudi hizo za serikali

Mipinzani bara iko kama mibwege hata tamko hamna wapo wapo tu wakati kule wako watoto na ndugu wa watu wa vyama vyote

Hopeless kabisa

Zanzibar hongereni CCM na upinzani kuwa united kwenye issue ya kitaifa inayohusu nchi yenu
 
P
Wapiiii kila ndege Alipiga panga 20%. Mbona akutuma msaada kwa watanzania waliotimuliwa msumbiji hapo jirani tu akabaki kuwatukana. Na cha ajabu msumbiji ilipopigwa na kimbunga akatafuta sifa za kijinga kumtuma kabudi kuwapa msaada haohao misumbiji iliyowatimua watanzania wenzake.

Pongez kwa mama kwa kuwasaidia watanzania wenzetu Ukraine.
Jambo kama hulijui kaa kimya ebu uliza wenyej mikoa ya mpakani na msumbiji ni malori mangap ya jeshi yalikwenda kubeba watanzania toka msumbiji kuwarudisha nyumban uliza watu wa ruvuma na mtwara
 
Back
Top Bottom