Fastjet: Kwa wale mlikuwa mnadhani itakuwa msaada kwa watanzania, someni hapa.

Wabongo kwa majungu, hamtaki walalahoi wapande ndege jamani?
Na mleta mada anaongea bila ushahidi wowote, huenda hajui hata ladha ya pipa ikoje. By the way low cost airlines ndio mkombozi wa nchi nyingi za Ulaya, hapa tunaongelea kampuni kama Easy Jet, Ryanair, Cimber Airlines na kadhalika. Humo hata maji hupewi, wanachotoa wao ni usafiri tu.
 
Ukiacha ushabiki wa kibiashara na ushabiki kama wa waumini wa huduma moja. Mimi naona usafiri kwa Fast jet ni ukombozi, tunaomba isifanyiwe hujuma kama waleeeee, tunawakumbuka.

- bei ni sh 32000
- Bei yao ukiongeza na VAT (kwa wale wasiorudishiwa) ni kama 45000 au chini ya hapo,
- kama unataka chakula, menu ba bei utapewa
- kama una mzigo 8000 kwa 20kg za kwanza
- kama una zaidi 8000 kwa kila kilo ya ziada

kuna siri gani kuficha haya? Lazima tujue hizo breakdowns

pima mwenyewe, wenzio tumekata ticket za familia kwa bei ya ticket ya mtu mmoja ya precision.
Tunaipenda preciosion ila lazima wakubali changamoto, wasianze kujisifia kwa kuwakashifu wenzao, soko sasa ni lao, inabidi wagawane. Wajenge imani kwa kazi yao,


Wawaue mende kwenye ndege zao, tunaogopa kula mikate kwa uwezekano kuwa imetembelewa na mende jamani hawana hela ya Expell

Hakika na mende tena???
Ila leo kwenye magazeti nimeskia huko duniani kuna abilia amegongwa na nyoka ndani ya pipa
 
Last edited by a moderator:
Na mleta mada anaongea bila ushahidi wowote, huenda hajui hata ladha ya pipa ikoje. By the way low cost airlines ndio mkombozi wa nchi nyingi za Ulaya, hapa tunaongelea kampuni kama Easy Jet, Ryanair, Cimber Airlines na kadhalika. Humo hata maji hupewi, wanachotoa wao ni usafiri tu.

Idimi hizo kampun ndo nazipenda
 
Last edited by a moderator:
Idimi hizo kampun ndo nazipenda

We cha tu. Nimepiga sana boksi za deiwaka toka nchi moja na nyingine kwa usafiri huo, hasa Cimber Airlines (enzi hizo ikiitwa Sterling Airlines) na SAS, halafu mwingine anakuja anaponda Fastjet bila kufanya upembuzi kwamba wengine nao wamepita njia hizo hizo.
Nimependa mfano wa mmojawetu hapo juu, aliyeongelea gharama kubwa za simu enzi hizo ndio zinaingia. Kupiga na kupigiwa ilikuwa lazima ulipe kwa dola, lkn makampuni yalipoongezeka kupokea simu ikawa bure na gharama sasa zimeshuka sana. Hata kwenye ndege, yakija makampuni mengi zaidi gharama zitashuka tu.
 
We cha tu. Nimepiga sana boksi za deiwaka toka nchi moja na nyingine kwa usafiri huo, hasa Cimber Airlines (enzi hizo ikiitwa Sterling Airlines) na SAS, halafu mwingine anakuja anaponda Fastjet bila kufanya upembuzi kwamba wengine nao wamepita njia hizo hizo.
Nimependa mfano wa mmojawetu hapo juu, aliyeongelea gharama kubwa za simu enzi hizo ndio zinaingia. Kupiga na kupigiwa ilikuwa lazima ulipe kwa dola, lkn makampuni yalipoongezeka kupokea simu ikawa bure na gharama sasa zimeshuka sana. Hata kwenye ndege, yakija makampuni mengi zaidi gharama zitashuka tu.
hapa ndio watz wengi na baadhi ya waafrika tunashindwa kusonga mbele kwa ile kitu inaitwa 'resistance to change'. Unajua mkuu kuna watu wameangaika sana, wameloga sana nk wakipigania kubakiza ajira zao RTC, Halmashauri, TRA, URAFIKI, ATC, Mawizarani and the like wakiamini kabisa kuwa hakuna maisha sehemu nyingine yoyote bila kuajiriwa katika hizo taasisi.
Laiti hawa wangelijua kuwa nje ya huo mfumo wa kifikra wangetokea mamilionea wa kuendesha hii nchi kwa kipato halali na kutoa ajira kwa watanzania wenzao (namaanisha wajasiriamali wanaolipa kodi leo)

 
kaka mchanganuo wao unafahamika tuu sio mpaka uon tiketi ya mtu wewe nenda ktk website yao kwenye booking then we can talk. hivi kwa watz ambao asili yao lazima abebe mzigo akisafiri utamsaidia kweli ktk hili? pili nachid kama inavyofahamika hapo hakuna kitu inaitwa VAT sasa subiri waiweke then utakuja tena humu humu kukiri kuwa hakuna jipya.



mkuu kilo 20 ni standard, mkuu unataka upande hadi na viroba vya ndizi au unapeleka mchele kilo 50 moshi ambao tofauti ya bei kwa kilo moja dar na moshi ni Tsh 100! acha kuishi kwa mazoea boss. hawa jamaa ni wakombozi kwetu
 
Wateja wa PW wanalalamiiika, wao wenyewe wenye ndege wanajua ndo maana wameshusha bei. Wameshusha ya nn kama hawaogopi? Wamezoea monopoly na kunyanyasa abiria, check in ya domestic flight wanafanya sawa na international flight kisa kwa sababu wako peke yao. Wanafanya fitna na travel agent kuwaumiza competitors hasa TC. Nadhani muda umefika wabadilike, there is more to come. Karibu fast Jet the economy airline utukomboe na ubeberu wa PW.
 
kwa wate wanaoujua marketing strategy kunakitu kinachoitwa Introductory Marketing unanaza bishara yuko kwa kujiendesha kihasara for short time kwa mantik kuwa ukamate wateja na kuteka akiri zao,na wakishaingia katika bishara yako wakishakuwa aware na biashara yako unapandisha bei chini au zaidi ya competitors wako unaanza kujiendesha kifaida zaidi..kipindi hicho utakuwa na wateja wengi zaidi..na wanapofanya hivyo wamekwisha kuona..kuwa ni ngumu penetration(marketing penetration) into air market with the some the price with other competitors..

Faida ambayo wangeweza kuipata kwa 5 yrs wataipata for 2 or 3 yrs.

Makampuni makubwa duniani yaliyofanikiwa yanianza kwa strategy hii baadaye yakajiendesha kifaida zaidi.


Kunakitu kinaitwa S.W.O.T--nondo nyingine nitafute...
 
Wateja wa PW wanalalamiiika, wao wenyewe wenye ndege wanajua ndo maana wameshusha bei. Wameshusha ya nn kama hawaogopi? Wamezoea monopoly na kunyanyasa abiria, check in ya domestic flight wanafanya sawa na international flight kisa kwa sababu wako peke yao. Wanafanya fitna na travel agent kuwaumiza competitors hasa TC. Nadhani muda umefika wabadilike, there is more to come. Karibu fast Jet the economy airline utukomboe na ubeberu wa PW.

Mkuu nilikuwa bongo last year! nilishangaa, yaani PW ni kampuni ya ajabu, inajifanyia inavyotaka kwa abiria wake!!! Nikasema bado tunahitanji "low cos airlines" ili wapate adabu. I am happy FastJet have led the way!!!

Nasikia wameshusha bei ya DR-MWZ-DAR to 199,000 inclusive of all taxes! I am saying they are still high!!!

Go go go FastJet, let them feel the pinch!!:A S angry:
 
wewe mtoa mada nakushauri uachane na mambo ya vitabu na notisi za shuleni na vyuoni na pia story za mtaani,, nenda kanunue ticket ukirudi utajua kuwa ulikuwa chaka mbaaya,,, me nimemchukulia ticket m2 mmoja juz juz hapa from mwanza to dar then to mwanza,(yaan to and fro au go & return) total ikaja elfu 90, yupo dar sa hivi na amekubali fast jet iko poa........ sasa huo mchanganuo wako umeutoa wapi???


au we ni presicision/ air tanzania???
 
Huwa natoka dar - mwanza na Atc kwa 398,000 na precission kwa 368,000 jaani trip moja kwa 198,000 mkp 200,000 hawa jamaa hata wangesema 100,000 bado wangekuwa cheap, hayo mahesabu uliyotoa hapo hayaeleweki kajipange tena
 
Huwa natoka dar - mwanza na Atc kwa 398,000 na precission kwa 368,000 jaani trip moja kwa 198,000 mkp 200,000 hawa jamaa hata wangesema 100,000 bado wangekuwa cheap, hayo mahesabu uliyotoa hapo hayaeleweki kajipange tena
Achana na vibaraka wa Precision wanawewe hao. Taarifa nilizo nazo hawa jamaa Fast Jet muda wowote kuanzia sasa wanaingiza Air bus mbili na ATR moja.

Kuna madai kwamba hii ni kuwavuta wateja ila baada ya miezi 3 bei itapanda na kuwa sawa na wengine, na mimi nasema hivi wakipandisha bei na kuwa sawa na wengine na sisi tunarudi kwenye mabasi yetu kama zamani.
 
mimi kama mmoja wa watu wanaosafiri sana niliposikia huduma mpya za fastjet tanzania kwa gharama nafuu ya Tsh 32000 nikasema mkombozi kafika Tanzania kwa watu wa Dar-Mwanza na KLM. Nikasema hvi kama napanda dar express dar to arusha kwa Tsh 28000 kwa masaa karibu kumi, leo naambiwa natumia Tsh32000 tu kwa muda wa saa 1 na dk kama 20 hv, kwanza nilistaajabu ktk hali iliyonifanya nijaribu kufanya utafiti wa hiyo fare yao.nilianza kwa kutembelea website yao ktk booking category.nilipoona jinsi mchanganuo wa cost yao ulivyo nikasema jamaa wameshajua kuwa watanzania ni watu wasiojua kufatilia jambo. Iko hivi fare exclusive vat and other cost ni Tsh 32000, ukibeba kabag kadogo utakalipia Tsh 8000, bag lisilozidi Kg 20(sport bag) utalilipia Tsh 32000. sasa hapa acha hiyo VAT ambayo ikianza kulipwa utalipa wewe, airport charge ambayo ni Tsh 10000.fanya sum utaona how much you should pay. kwa mantki hiyo watanzania hapa tumejidanganya wenyewe kwani kilichotumika ni busness tricks ktk kuvuta mind za clients. ndo mana kama mtafatilia gazeti la The Citizen la ijumaa iliyopita kama sikosei kuna mwakilishi toka precision airline kaelezea sana ktk hili na mwisho akasema hivi " Haitachukua muda kwa Watanzania kuelewa gharama halisi watakayolipa kwani ktk biashara hii ya usafiri utagundua gharama za uendeshaji zipo sawa na 40% ya mapato hutumika ktk oil" akaendelea kwa kusema hajaona drop down yoyote ktk booking yao kwa maana kuwa hawajaathiriwa vyovyote vile na ujio wa Fastjet zaidi ya kupata changamoto zaidi ktk uboreshaji wa huduma zao.
My take:
Ni wazi kuwa wenye ufahamu zaidi ktk huduma za usafiri wa anga wamegundua kuwa kama kuna diffence basi itakuwa ndogo na si kama inavyotamkwa na watu ktk vyombo vya habari. so tuwe tunasoma angalau watanzania wenzangu maana kila jambo ni sisi tu watanzania tunadanganywa thats too sad kusema kuwa hata wawekezaji wamegundua watanzania wengi ni mbumbumbu ktk masuala yanayowahusu wenyewe.

Hiyo gharama bado ni chini sana kulinganisha na Precision Air. Hizi ndege ni kwa ajili ya watu wanaofanya biashara au safari za muda mfupi. Ni mtindo huo huo wa kulipisha mizigo wanafanya EasyJet na Rynair. Mtu kama unakwenda Mwanza kwa mkutano na kurudi Dar, unahitaji mabegi ya nini. Kama unaenda Holiday Mwanza kwa siku nne mabegi mazito ya nini. Wenzetu ndo wanavyofanya. Kwa EasyJet and Ryanair hakuna kupangiwa seat, unawahi kupata seat, ukitaka chai au kahawa unanunua, lakini bado ni usafiri wa bei nafuu na watu wanautumia sana.
 
Ukiacha ushabiki wa kibiashara na ushabiki kama wa waumini wa huduma moja. Mimi naona usafiri kwa Fast jet ni ukombozi, tunaomba isifanyiwe hujuma kama waleeeee, tunawakumbuka.

- bei ni sh 32000
- Bei yao ukiongeza na VAT (kwa wale wasiorudishiwa) ni kama 45000 au chini ya hapo,
- kama unataka chakula, menu ba bei utapewa
- kama una mzigo 8000 kwa 20kg za kwanza
- kama una zaidi 8000 kwa kila kilo ya ziada

kuna siri gani kuficha haya? Lazima tujue hizo breakdowns

pima mwenyewe, wenzio tumekata ticket za familia kwa bei ya ticket ya mtu mmoja ya precision.
Tunaipenda preciosion ila lazima wakubali changamoto, wasianze kujisifia kwa kuwakashifu wenzao, soko sasa ni lao, inabidi wagawane. Wajenge imani kwa kazi yao,


Wawaue mende kwenye ndege zao, tunaogopa kula mikate kwa uwezekano kuwa imetembelewa na mende jamani hawana hela ya Expell

Tutaanza kushika mabomba kwenye ndege muda si mrefu. hahahaha kweli watanzania mnapenda vya bure!
 
kwa wate wanaoujua marketing strategy kunakitu kinachoitwa Introductory Marketing unanaza bishara yuko kwa kujiendesha kihasara for short time kwa mantik kuwa ukamate wateja na kuteka akiri zao,na wakishaingia katika bishara yako wakishakuwa aware na biashara yako unapandisha bei chini au zaidi ya competitors wako unaanza kujiendesha kifaida zaidi..kipindi hicho utakuwa na wateja wengi zaidi..na wanapofanya hivyo wamekwisha kuona..kuwa ni ngumu penetration(marketing penetration) into air market with the some the price with other competitors..

Faida ambayo wangeweza kuipata kwa 5 yrs wataipata for 2 or 3 yrs.

Makampuni makubwa duniani yaliyofanikiwa yanianza kwa strategy hii baadaye yakajiendesha kifaida zaidi.


Kunakitu kinaitwa S.W.O.T--nondo nyingine nitafute...


Fastjet ni 'no-frills/low -cost carrier. Hizo marketing rhetoric unazoongea na mambo ya 1st year. Jaribu kutafiti low-cost carriers zinafanye kazi.
 
Back
Top Bottom