Fast & Furious 9: Umeionaje?

Hahaha nimeicheki jana hii ni bonge la muvi..

Contract killers mama na mtoto!
Mama baada ya kufanya mauaji sana akawa most wanted na makundi ya wakora ikabidi apotee(go dark)
Huku akimwacha mwanae SAMI akichukuliwa na kundi mamaake alokuwa anafanyia kazi ya kuua!

Mtoto baada ya kuwa well trained akawa anapewa mission zile zile kama za mamaake! Za kuua.....

Utamu ulianzia pale sami alipofanya mauaji kimakosa na akamuua mtoto wa tycoon gaidi mbaya kabisa....

Huku sami akipewa tenda ingine ya kwenda kumuua jamaa alieiba hela za kampuni yao na kuzirudisha..
Baada kumpiga yule mwizi risasi mwizi akamwambia sami kwamba zile fedha aliiba ili amkomboe mwanae ambae alitekwa hivyo anaomba amsaidie kumuokoa mwanae!!

Hapo ndio muvi inanoga zaidi..
Sami katumwa aue kisha arudishe ela za kampuni yeye akazipeleka kwa magaidi ili amkomboe mtoto wa yule mwizi!!

Ikabidi kampuni itume wakora wengine wamuue sami kwa kukiuka au kukengeuka na kuvunja uaminifu..
Hapo hapo kampuni ikampigia simu yule tycoon alieliwa mtoto wake a kupewa location ya sami ili wammalize...

Kwahiyo hapo sami inabidi apambane na wakora waliemteka mtoto hapohapo watu waliotumwa na kampuni yake vilevile yule tycoon ambae mwanae aliuwawa na sami....

Ni hatari na nusu hapo..
Hii muvi naipa rate 7/8
Umetisha mzigo wa maana sana huo..
Mzigo mwingine ulionifanya nicheke sana ni huu hitman's wife bodyguard
 
Nimeangalia movie nyingi naona siku izi movie zimeisha story wanachofanya ni ku change character tuu ila content za movie aisee ni hakuna kitu kabisa , ebu nambie movie gani ni mpya kuanzia kwenye story ?niishie kusema production ya movie kwenye story imeeshia ukomo ndio maana saa hii movie moja ma star kumi
 
Hiyo movie niliacha kuangalia pale diesel na mdada flani wakiwa ndani ya gari wamerukia mlima mwingine kwa kutumia kamba na Gari likaharibika sana lakini wao hawakuumia hata kidogo.
 
Tayari movie ya FF9 imeachiwa clean version, wazee wa kudownload kazi kwenu! Kama ushaoiona njoo utupe maoni yako, tumepigwa au laa?

View attachment 1872922
iko vizuri,yaani jamaa wanakulazimisha kukudanganya mpaka unaingia line๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚,ila nilicheka zaidi mbongo mwenzetu Tyrese alivoanza kujihisi yeye si binadamu wa kawaida maana karushiwa risasi nyingi na hata moja haijampata ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†
 
Nimeangalia movie nyingi naona siku izi movie zimeisha story wanachofanya ni ku change character tuu ila content za movie aisee ni hakuna kitu kabisa , ebu nambie movie gani ni mpya kuanzia kwenye story ?niishie kusema production ya movie kwenye story imeeshia ukomo ndio maana saa hii movie moja ma star kumi

Hollywood sku hizi wameishiwa new materials kazi yao ni Kutoa Sequels, Pre-sequel, remakes, reboots au live actions za animation hawana mpya kupata original story kwa sasa ni nadra, labda icheki Ice road ya Liam Neeson japo sina uhakika kama ni adaptation kutoka mahali au la
 
Nlishatoaga review mwanzo pale hamna kitu, Probably watu waliniona hater kwa vile wengi walikuwa hawajaiangalia

Movie Reviews
Ikitoka army of thieves unistue
 
Back
Top Bottom