FAO yaishauri Tanzania kuweka kipaumbele katika zao moja la kilimo litakaloitambulisha nchi soko la Kimataifa

Shirika la Chakula duniani FAO limeishauri Tanzania kuweka kipaumbele katika zao moja la kilimo litakaloitambulisha nchi yetu kwenye soko la kimataifa.

Chanzo: Radio One

My take; Pendekeza zao, binafsi Napendekeza Korosho

=======

View attachment 1966827

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limeishauri Tanzania kuweka kipaumbele katika zao moja la kilimo litakaloitambulisha Tanzania Kimataifa ili kuweza kupenya kirahisi katika soko la Kimataifa la mazao ya Kilimo.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Qu Dongyu alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula(Mb) mazungumzo yaliyofanyika katika makao makuu ya Shirika hilo Roma, Italia.

Dkt. Qu Dongyu ameongeza kuwa Tanzania ina mazao muhimu na mengi ya kilimo ambayo yanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza pato la Taifa lakini changamoto kubwa ni namna ya kupenya katika soko la kimataifa kutokana na kukosa zao la utambulisho na kwamba Shirika hilo FAO iko tayari kusaidia ujuzi na kuijengea uwezo Tanzania kufikia lengo hilo.

View attachment 1966828

Dkt. Qu Dongyu ameongeza kuwa kwa sasa FAO imeanzisha jukwaa maalum la kuwawezesha wanawake na vijana kunufaika na sekta ya kilimo kutokana na utafiti kuonesha kuwa wanawake wengi katika nchi zinazoendelea wanajihusisha na kilimo.

Katika mazungumzo hayo Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Libearata Mulamula amesema Tanzania imeupokea ushauri wa FAO na kwamba itaufanyia kazi ili kuiwezesha Tanzania kutambulika na kunufaika katika soko la Kimataifa la mazao ya kilimo ili kuwawezesha wakulima kujikomboa kiuchumi kwa kuongeza pato la kaya na hivyo kuinua uchumi wa Tanzania.

Ameongeza kuwa Tanzania imejipanga kikamilifu kunufaika na mpango wa Shirika la chakula na Kilimo la Umoja wa Matiafa (FAO) wa kuanzisha jukwaa maalum la kuwawezesha wanawake na vijana kunufaika na sekta ya kilimo kutokana na utafiti kuonesha kuwa wanawake wengi katika nchi zinazoendelea wanajihusisha na kilimo

View attachment 1966829

Balozi Mulamula yuko Roma, Italia kushiriki Mkutano wa tatu wa Mawaziri wa Mambo ya Nje kutoka nchi za Afrika na Italia pamoja na kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa amani.
Huu ni ukweli ambao sijui kwa nini wataalamu wetu hawaoni mpaka tuambiwe na FAO? The fact is that we spread yourself too narrowly. Tunalima mahindi, mpunga, ngano, viazi , maharagwe, kunde, ndizi, alizeti , michikichi, n.k, lakini siyo hata zao moja tunapeleka nje kama finished product. Ukienda Muheza utakuta malori mengi toka Kenya yanapakia machungwa, wanaenda kukamua juice halafu wanairudisha hapa kama finished product, hakuna mtu anayefikiria kuweka kiwanda Muheza au Tanga cha kukamua juice ya matunda.
 
Ardhi ya Tz Inakubali aina zote za mazao isipokuwa ya arabuni kama tende

Kikubwa fursa
 
Ni kweli, Ni wazo jema kabisa.

Tuwe na alama ya utambulisho kimataifa kupitia zao la aina moja ya kilimo.

Lakini haimaanishi kwamba tubweteke na tusitie nguvu katika kulima mazao mengine.
 
... mahindi yao kwa ajili ya kulishia nguruwe na cattle! Dah; this world is not fair.
Ndo ivo mkuu lakini ndo tayari maalufu kwa hilo na kuna wakati nilisikia kuwa hicho chakula cha wanyama kililetwa Africa kama msaada wakati wa njaa
 
Siwezi kukubaliana na ushauri huu. Diversity ya ardhi, hali ya hewa hapa nchini inatoa furusa ya kulima mazao mbali mbali. Kwenye masuala ya nishati tunahimiza energy consumption mix ili kupunguza risks. Ni strategy hii pia inatakiwa itumike kwenye kilimo.
Umenena vyema.
 
Shirika la Chakula duniani FAO limeishauri Tanzania kuweka kipaumbele katika zao moja la kilimo litakaloitambulisha nchi yetu kwenye soko la kimataifa.

Chanzo: Radio One

My take; Pendekeza zao, binafsi Napendekeza Korosho

=======

View attachment 1966827

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limeishauri Tanzania kuweka kipaumbele katika zao moja la kilimo litakaloitambulisha Tanzania Kimataifa ili kuweza kupenya kirahisi katika soko la Kimataifa la mazao ya Kilimo.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Qu Dongyu alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula(Mb) mazungumzo yaliyofanyika katika makao makuu ya Shirika hilo Roma, Italia.

Dkt. Qu Dongyu ameongeza kuwa Tanzania ina mazao muhimu na mengi ya kilimo ambayo yanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza pato la Taifa lakini changamoto kubwa ni namna ya kupenya katika soko la kimataifa kutokana na kukosa zao la utambulisho na kwamba Shirika hilo FAO iko tayari kusaidia ujuzi na kuijengea uwezo Tanzania kufikia lengo hilo.

View attachment 1966828

Dkt. Qu Dongyu ameongeza kuwa kwa sasa FAO imeanzisha jukwaa maalum la kuwawezesha wanawake na vijana kunufaika na sekta ya kilimo kutokana na utafiti kuonesha kuwa wanawake wengi katika nchi zinazoendelea wanajihusisha na kilimo.

Katika mazungumzo hayo Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Libearata Mulamula amesema Tanzania imeupokea ushauri wa FAO na kwamba itaufanyia kazi ili kuiwezesha Tanzania kutambulika na kunufaika katika soko la Kimataifa la mazao ya kilimo ili kuwawezesha wakulima kujikomboa kiuchumi kwa kuongeza pato la kaya na hivyo kuinua uchumi wa Tanzania.

Ameongeza kuwa Tanzania imejipanga kikamilifu kunufaika na mpango wa Shirika la chakula na Kilimo la Umoja wa Matiafa (FAO) wa kuanzisha jukwaa maalum la kuwawezesha wanawake na vijana kunufaika na sekta ya kilimo kutokana na utafiti kuonesha kuwa wanawake wengi katika nchi zinazoendelea wanajihusisha na kilimo

View attachment 1966829

Balozi Mulamula yuko Roma, Italia kushiriki Mkutano wa tatu wa Mawaziri wa Mambo ya Nje kutoka nchi za Afrika na Italia pamoja na kushiriki Mkutano wa Kimataifa wa amani.
Nchi kama Tzn haiwezi kuwa na zao moja tuu,binafsi napendekeza tuwe na Mazao 5..

Happy tuwe na korosho,parachichi,mchele,chai na pareto.
 
Waende zao hapa!! Enzi za Mwalimu Nyerere tulikuwa na Pamba,Kahawa,Mkonge ,Chai na Muhogo kama Exports.Na tulikuwa Vizuri sana .Sasa hivi Wanaotuangusha ni Wanasiasa .Kama wakiwa makini Tanzania tutarudi no 1 kwenye export za mazao ya Kilimo
Swma hivi tuyape kipaombele Mazao machache sio tunaenda jumla jumla tuu..

Tuchague Mazao maalum for exports kama 5 na Mazao ya food security for domestic and exports when needed.
 
Akitoa mzungu ndio linakuwa wazo zuri ila tukisema wananzengo haina maana?

Mawazo yamezungumzwa Sana hata saizi ukienda story of change kuna mawazo mazuri mengi tuu ila mnasubilia aje mzungu ndio aseme .
ndio mfumo tulio rithiswa na wakoloni shekh ndio maana hadi leo ni zaidi ya miaka 70 bado tunaitumia Katiba yao
 
Ndo ivo mkuu lakini ndo tayari maalufu kwa hilo na kuna wakati nilisikia kuwa hicho chakula cha wanyama kililetwa Africa kama msaada wakati wa njaa
Mahindi ya Yanga wazee wanasimulia.
 
Wazo la Kijasusi. Hatulitaki. Tumekataa. Shenzi kabisa. Hivi wanatuonaje hao?
 
Kilimo Cha karanga KONGWA
Ha ha ha mzee mwenzangu mitaala ya elimu tuliyokuwa nayo ni ya kijinga sana. Eti rais wa kwanza wa Mali aliitwa nani? Wakati wenzetu huko walikuwa wanasoma mambo ya teknolojia na kadhalika, sisi tumebaki kuwasifu kina Kwame Nkurumah.
 
My take; Pendekeza zao, binafsi Napendekeza Korosho
Una sababu zipi, kwa nini isiwe soya, ukiniuliza ntakupa sababu kikamilifu.

Hata hivyo sikubaliani na wazo hilo la zao moja. Nchi yetu ina maeneo yenye kubeba aina tofauti za mazao. Kupeleka korosho Kilimanjaro haitasaidia sana wananchi wa huko. Brazil ina Kahawa na Soya na mifugo, kama kuku n.k. Kwani Kenya kuwa na zao la chai ni kipi kimeongezeka kwao? Mbona wanahangaika na Avocado, Maua, mbogamboga, n.k.

Zao moja likibuma kutokana na sababu mbalimbali, hali ya hewa, au hata kushuka kwa bei duniani, ndiyo mmekwisha kazi msimu huo!

Hilo ni pendekezo la hovyo. Huyo mtu kakosa jambo la muhimu la kujadili na waziri wetu, akaona heri apoteze muda akipiga soga.

Lakini sikusoma sababu yake kushauri hivyo, Bado sidhani kuwa ni ushauri wa kuwekwa maanani.

Pendekezo la maana sana angesema MIKOA iwe na zao moja la nguvu sana. Kwa mfano, Kigoma yote ile ingeenezwa na michikichi sehemu zote za mkoa.
Kagera ikajichimbia kwenye NDIZI na Kahawa

SIMIYU PAMBA

SIngida na Dodoma usiwaambie chochote zaidi ya ALIZETI, n.k., n.k..
 
Wamesema zao la kipaumbele!
EeenHeeee!

Kweli umekengeuka kwenye hili. Akili imegota kabisa!
Heri ubaki kwenye siasa za CCM na vimistari vyako viwili viwili.

"Kipaumbele" maana yake nini,...kama michikichi inastawi vyema Kigoma, tuamue hilo zao ndio liwe wakilishi wa nchi nzima, kwa kulipa "kipaumbele", kama ndilo zao tunaloweza kuchagua kuwa litutambulishe?
 
Back
Top Bottom