MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,734
1. Penda Kujichanganya nao kupiga stori ukiwa na muda
2. Ukibakiza vichenji chenji wape
3. Ukijua wanavuta Bangi au Pombe siku ukiwa nazo mfukoni wanunulie
4. Ukisikia Mmoja wao kakamatwa onyesha hata kinafiki tu kuwa unampambania Kumtoa
5. Wakosoe kwa kuwajenga na siyo kwa Kuwadhalilisha na kama ukisikia kuna Kazi yoyote (hasa za Kawaida tu) waunganishe / watafutie
6. Usiwe na Kiherehere Kingi cha Kuwachomesha kwa Polisi mpaka labda itokee sana na imebidi
7. Ukiwa nao Maskani unapiga Story Mbili Tatu penda mara kwa mara kuingizia Mambo ya Kiimani ( hasa ya Mwenyezi Mungu ) na jinsi ya kuwa Mwema hapa duniani na kutubu ili kuyaanza Maisha mapya na mema
Ukiyafanya haya mambo Makuu Saba (7) Tajwa hapa nakuhakikishia kuwa hata ukiwa unaishi nao Mtaani unaweza hata Kukaa miaka 20 wasikufanye lolote lile na ukashangaa.
Kwa KEROZENE kuandika haya (hivi) sisemi kuwa nawapenda au nawaunga mkono hawa Wahalifu bali nimejaribu tu kuwapeni Mbinu ya Kisaikolojia ya kuweza Kuishi nao na Kuwakabili pia bila ya wao Kukudhuru kwa lolote / chochote.
Nina Mtu hapa Majuzi kati Usiku mida ya Saa 7 Gari yake ilimsumbua na alikuwa Safarini hivyo akabidi aje Kulala Ghettoni Kwangu na akiwa njiani na Kukutana nao akiwa na Simu zake Mbili za thamani na Hela mfukoni walipomuweka Mtu kati ili Kumdhuru huku wakimhoji akasema anakuja kwangu KEROZENE na kilichofuatia wakaachana na Mpango wao huo na kumsindikiza hadi Ghettoni Kwangu na Kunigongea kisha nikaamka na wakanikabidhi Mgeni wangu huku Wawili wakisema watalilinda Gari lake mpaka Asubuhi hivyo asiwe na Wasiwasi.
Tulipoamka Asubuhi na kuanza harakati za Kushughulikia Gari lake Jamaa yangu alipowaona akatoa Tsh 10,000/= kama Asante yake Kwao na kwa Mshangao Jamaa waliikataa na kumwambia wakiipokea hiyo Hela itakuwa ni kama vile wananilipisha Mimi Kaka yao wa Mtaa kwani huwa nawasaidia mno wakiwa na Shida.
Baada ya Jamaa yangu kuona Tukio lile na nikamuelezea Mishe zao zote za Kimatukio Mtaani (Mitaani) ameshawatafutia Watatu kati yao Kazi katika DalaDala zake na sasa wamebaki kama Wanne baada ya wengine pia Kuwaunganisha katika Mishe za Ujenzi, Uvuvi na Ulinzi.
Tuwasaidie na kamwe tusiwadidimize!
2. Ukibakiza vichenji chenji wape
3. Ukijua wanavuta Bangi au Pombe siku ukiwa nazo mfukoni wanunulie
4. Ukisikia Mmoja wao kakamatwa onyesha hata kinafiki tu kuwa unampambania Kumtoa
5. Wakosoe kwa kuwajenga na siyo kwa Kuwadhalilisha na kama ukisikia kuna Kazi yoyote (hasa za Kawaida tu) waunganishe / watafutie
6. Usiwe na Kiherehere Kingi cha Kuwachomesha kwa Polisi mpaka labda itokee sana na imebidi
7. Ukiwa nao Maskani unapiga Story Mbili Tatu penda mara kwa mara kuingizia Mambo ya Kiimani ( hasa ya Mwenyezi Mungu ) na jinsi ya kuwa Mwema hapa duniani na kutubu ili kuyaanza Maisha mapya na mema
Ukiyafanya haya mambo Makuu Saba (7) Tajwa hapa nakuhakikishia kuwa hata ukiwa unaishi nao Mtaani unaweza hata Kukaa miaka 20 wasikufanye lolote lile na ukashangaa.
Kwa KEROZENE kuandika haya (hivi) sisemi kuwa nawapenda au nawaunga mkono hawa Wahalifu bali nimejaribu tu kuwapeni Mbinu ya Kisaikolojia ya kuweza Kuishi nao na Kuwakabili pia bila ya wao Kukudhuru kwa lolote / chochote.
Nina Mtu hapa Majuzi kati Usiku mida ya Saa 7 Gari yake ilimsumbua na alikuwa Safarini hivyo akabidi aje Kulala Ghettoni Kwangu na akiwa njiani na Kukutana nao akiwa na Simu zake Mbili za thamani na Hela mfukoni walipomuweka Mtu kati ili Kumdhuru huku wakimhoji akasema anakuja kwangu KEROZENE na kilichofuatia wakaachana na Mpango wao huo na kumsindikiza hadi Ghettoni Kwangu na Kunigongea kisha nikaamka na wakanikabidhi Mgeni wangu huku Wawili wakisema watalilinda Gari lake mpaka Asubuhi hivyo asiwe na Wasiwasi.
Tulipoamka Asubuhi na kuanza harakati za Kushughulikia Gari lake Jamaa yangu alipowaona akatoa Tsh 10,000/= kama Asante yake Kwao na kwa Mshangao Jamaa waliikataa na kumwambia wakiipokea hiyo Hela itakuwa ni kama vile wananilipisha Mimi Kaka yao wa Mtaa kwani huwa nawasaidia mno wakiwa na Shida.
Baada ya Jamaa yangu kuona Tukio lile na nikamuelezea Mishe zao zote za Kimatukio Mtaani (Mitaani) ameshawatafutia Watatu kati yao Kazi katika DalaDala zake na sasa wamebaki kama Wanne baada ya wengine pia Kuwaunganisha katika Mishe za Ujenzi, Uvuvi na Ulinzi.
Tuwasaidie na kamwe tusiwadidimize!