Elections 2010 Fanya uamuzi sasa fanya kwa umakini piga kura katika uchaguzi mkuu ujao

Maluo

Member
Feb 29, 2008
58
3
Ndugu wana jamii forams

ni muhimu sana kujitolea ile kuweza kuleta mabadiliko ya kisiasa ili uchumi wetu uweze kuonguzwa na watu wenye mtizamo chanya hivyo basi wewe ukiwa ni mwanachama ama momaji wa jamii forums naomba sana sana uhakikishe unakuwa mpiga kura kwa kuwa kura yako ni sehemu ya kuweka mtazamo wako kushirikishwa katika uamuzi wa mustakabali wa taifa hili

nasema hivyo kwa sababu zifuatao
1. Kujiandikisha na kupiga kura ni kuonyesha uzalendo uliotukuka kwa kuwa nyakati zinaonyesha kwamba kama wewe una uwezo wa kutambua mabaya na mazuri na pia una uwezo wa kushiriki katika kuweka viongozi wenye upeo wa dunia ya sasa kwa kupiga kura na endapo wewe unao huo uwezo na hutaki kupiga kura INASIKITISHA SANA KWA KUWA UNAACHA JUKUMU MUHIMU NA LA MAANA KUFANYWA NA WACHECHE NA PENGINE WASIOELEWA MAMBO. Kwa kuwa endapo una uwezo wa kuchanganua maswala mbali mbali kutokushiriki katika kupiga kura ni sawa na kuendelea kuwaruhusu viongozi wasiotufaa kutuongoza kwa kuwa wewe ujuae mabaya hushiriki katika kuyakataa

Hivyo wana Jamii Forums jiandae kupiga kura kwa kuwa watanzania tunasadikika kuwepo takribani milioni arobaini kwa sasa hivyo tuhakikishe angalao kura za uraisi zinafikia angalao watu millioni 20 kupiga kura tuache hao millioni ishirini ambao wanaweza kuwa watoto ama vinginevyo takwimu zetu siyo makini sana na wale waliohama baada ya daftari la kudumu la wapiga kura kuandikishwa

2. Jambo la pili hakikisha unapata muda wa kusoma vitabu muhimu kama katiba ya Nchi yetu, kupata taarifa mbali mbali pamoja na kuhakikisha taarifa hizi zinakuwa ni sahihi pia zinawafikia wengi kwa kuwa ni vyema jamani hadi leo hii kweli tunaenda kitua cha polisi unaambiwa balozi wako ni nani Jamani zinduka ofisi ya serikali ama mamlaka za kisheria za chini ni viongozi tunawachagua ambao ni wa aserikali za mitaa ambapo tunao wenyeviti wa mitaa kwa maeneo ya mijini na wenyeviti wa vitongoji kwa maeneo ya vijijini jamani tuelimishane kujua haki zetu kwa kuwa utaratibu kwa ubalozi ni wa chama cha ccm na siyo kwa ajili ya watu wote na mimi kwa kweli hili ni moja ya mabadiliko ambayo tunayahitaji kwa jamii yetu kwani
 
hili ni jambo la muhimu sana, watanzania jueni kwamba, bakora kubwa kuliko zote mnayoweza kuwapiga mafisadi, ni through kura yako moja tu. tukumbuke ya kwamba, kwa kura zetu ndo tunawaajiri hawa viongozi, sisi ndo mabosi wao na wanatakiwa wafanye kile tunachowatuma, kwa kura zetu wanaendesha mashangingi, bila sisi hawangeweza, hivyo lazima watutumikie. just think about it, chukua uamzi kuwashawishi hata watu wengine wenye moyo wa kuto kupiga kura, siku hiyo wajitokeze kuchagua kiongozi atakaye tufaa. tusipende kuchaguliwa kiongozi na mtu mwingine, tutakosa sauti wakati tukiibiwa kodi zetu.
 
Back
Top Bottom