Fani zote tugomee, saa ya ukombozi ndio hii unasemaje

fikirikwanza

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
7,452
3,065
Baada ya kuona namna serikali ilivyoboronga kushughulikia suala la mishahara na posho za madaktari, japo siwaungi mkono madaktari kuacha wagonjwa wafe wakidai posho, nimefikiri na kuona ni kama kwamba mungu anataka kutusaidia WaTZ, napendekeza fani zote tuweke dhana za kufanyia kazi chini, serikali ndo itatafuta ufumbuzi wa mambo mengi yanayofanyika vibaya bila hata kujali malalamiko ya wananchi.
 
pesa ya kutafuna wao wanayo ila ya wafanyakazi hawana . Jeuri ni wafanyakazi wote silaha chini tuone ..................
 
nape leo hajaingia humu?
kakimbia kambi?
kama ananisikia naomba aje japo tumsikie ana makapi gani leo?
 
Kama serikali imeshindwa kujua namna ya kuumaliza mgomo huo, wakati watu wanakufa labda ndo wakae pembeni watu wengine ambao pia ni Watz kama wao walijaribu kuongoza na kutatua matatizo ya watz
 
Inshu ni kumgomesha mwl wa primary school mwnye div.four ya points 28! Hawa ndo tatizo kubwa! Thts y kenya walimu wa primary wana chama chao na wa sec.na lecturers wana chama chao pia! Sasa hapa cwt occupants wengi ni walimu wa primary! Kutakua na mgomo hapo? Akifukuzwa na four yake ataajiriwa wapi?? Bado kaz ya ku pressurize walim wagome wakiwa kama ndo watumwa wa serikali tena wengi in number(about 47 pcnt of all gvnt workers) bado ni ngumu!
 
Inshu ni kumgomesha mwl wa primary school mwnye div.four ya points 28! Hawa ndo tatizo kubwa! Thts y kenya walimu wa primary wana chama chao na wa sec.na lecturers wana chama chao pia! Sasa hapa cwt occupants wengi ni walimu wa primary! Kutakua na mgomo hapo? Akifukuzwa na four yake ataajiriwa wapi?? Bado kaz ya ku pressurize walim wagome wakiwa kama ndo watumwa wa serikali tena wengi in numhber(about 47 pcnt of all gvnt workers) bado ni ngumu!
Hapo umenena mkuu,hawa walimu wa primary n tatizo,na wanachangia sana hata kwenye mambo ya
Uchaguzi,cjui wakoje na vi 4 vyao
 
Hapo umenena mkuu,hawa walimu wa primary n tatizo,na wanachangia sana hata kwenye mambo ya
Uchaguzi,cjui wakoje na vi 4 vyao

wana njaa kweli hawa lkn ndo wenye shida kuliko mtu yeyote hapa nchini.yaan njaa mbaya kweli manake mtu unaweza ukaambiwa vua nguo mbele za watu upewe pesa mtu akakubali acha kabisa njaa inaumbua
 
Acheni mawazo yenu ya ajabuajabu. Dhiki kuu haina budi kuja ni Mapenzi ya Mungu.


Madoctor kugoma siwaungi mkono hata nimewekewa shoka shingoni. Na hamtambui hakuna tumaini kwa yeyote hapa duniani maana kila mnaedhani atatatua matatizo yenu hata mridhike nae anamatatizo yake.



Serikali muikubali kama ilivyo na mridhike na mishahara yenu, imeandikwa umasikini hautakoma kamwe katika nchi na suluhu ya kutotawaliwa na matajiri na kutatua matatizo yetu nikufanya kazi kazi kwa bidii, je sio sisi tutawaliwao na matajiri?



unapogoma doctor ni sawa nakuua kwa upanga, na unajua ukiua kwa upanga kinachofuata, Mungu amewabariki kwa neema ya karama hii(maarifa ya udoctor) ili mumtukuze kupitia kazi za mikono yenu amini inakuja siku kwakuwa mliomba kwa tamaa zenu naye (MUNGU) ATAWALIPA MNACHOKIDAI kwa maana enzi yake imezungukwa na haki na hukumu. Nanyi mwawahukumu viumbe wake wapate tabu hata kufikwa mauti kwa kuzitimizia roho zenu tamaa zake.


Tumaini peke ni Kwa Mungu hata kama unalipwa sh.100 mambo yako yote yatafanikiwa. Ila mmelitamani Joho la babeli na kulivaa(tabia)
hata matokeo yake mmelewa mvinyo wake, mmesahau maadili ya kazi na AMri YA MUNGU "USIUE, USITAMANI," Serikali yetu ni masikini.



Tamaa zenu za starehe na anasa zinaifanya nchi kuwa mtumwa wa nchi tajiri.


*ANGALIZO, YEYOTE AFANYAE KAZI ILI KUTATUA MATATIZO YAKE TU NI MTUMWA, ILA AFANYAE KAZI KUJIKOMBOA YEYE NA WENGINE NI MTU HURU*
 
Acheni matusi, nyie primary mlifundishwa na wenye degree?? Mgomo unawezekana kwa yeyote tukiamua, asiyetaka analazimishwa!
 
Mgomo !
Migomo yenu yakuwaimbia wafu wasiojua lolote wamelala kaburini.
Huwa mnashangaza watu wazima mmebeba mabango eti "kama sio juhudi zako Nyerere....." huimbwa sana na wagomaji wanaopingana na mamlaka kwakuwa tumaini lenu mmeliweka kwa wafu akina Plato, aristotle, abrahamu, luther king.
Lakini nasema ikiwa tumaini lako li Katika kristo Yesu aliye hai kamwe hutotetereka hata kama unalipwa mia imeandika iheshimuni mamlaka na msibishane nayo ila omben kwa Mungu mtapewa.
 
Misimamo ya kidini daima ni ya kihafidhina na hudumaza harakati za ukombozi. Mwenyezi MUNGU hataki uonevu hivyo chonde pembeni na udini wenu wa kinafiki sie twasonga mbele.
 
Pia tuwagomee na Tanesco kulipa ongezeko la bei ya kununulia umeme halafu tuandamane pale Jangwani ,Jangwani iwe ndio kitovu cha maandamano yote
 
Hata mkiandamana miaka mia asubuhi na mchana HAKUNA TUMAINI DUNIA HII na usidhani CCM hawjui walitendalo CHADEMA na CHADEMA WAJUA CCM ILITENDALO HIVYO WOTE WANAJUANA NA WANAUELEWA MCHEZO WAO wakuchanganye wewe. Hao wote ni wanasiasa nasi twajua siasa ni mbaya na imeandikw hakuna amani kwa wabaya amkeni. Jesus coming soon.
 
Back
Top Bottom