Opportunity Cost
JF-Expert Member
- Dec 10, 2020
- 9,035
- 6,904
Uzalendo kwanza.
Kichwa cha habari kinahusika, miaka ya nyuma mtu ulikuwa ukifeli au kupata ufaulu hafifu unaambiwa hata ualimu umeshindwa? Lakini kwa miaka ya hivi karibuni naona trend imehamia kwenye fani ya Afya na Tiba.
Just imagine fani nyeti kama afya ila pass mark za udahili ni kuwa na D D D kwenye masomo yanayoitwa ya sayansi. Kuna watu watesema eti hiyo ni minimum pass mark lakini wanasahau kwamba wanafunzi wengi wanaangukia kwenye ufaulu huo na kudahiliwa ngazi ya Diploma alafu baadae wanakuwa Medical Doctor baada ya kujiendeleza.
Binafsi naamini mtu mwenye uelewa mdogo au ufaulu finyu hata ajiendeleze ataishia kuwa mtaalam wa average tuu. Bahati mbaya watu wa hivi ndio wamejaa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, na hii kazi saizi imevamiwa na kila mtu sio kazi ya wito na kujitoa bali kazi ya kusaka pesa.
Watu wenye uelewa finyu ndio tunategemea wagundue chanjo ya corona na kufanya operation complex, huu ni utani na kuchezea afya zetu. Hawa ndio mara nyingi unakuta wanagombana na kutoleana maneneo machafu na wagonjwa. Pia kwa watu wa hivi pesa mbele huduma inafuata. Binafsi nikienda hospital au dukani nikakuta vile vitoto vyenye D 3, huwa siko tayari vinihudumie kwenye ishu za msingi labda kupima pressure na maabara ila prescriptions hapana, huwa niko tayari kughairi huduma na kutafuta kwingine au nimpigie simu daktari naemfahamu hakupitia huu utaratibu wa D 3.
Kana kwamba haitoshi saizi kumezuka vyuo uchwara kila kona vinavyotoa haya mafunzo ya fani za afya almaarufu Health and Allied Sciences, sayansi zipi na pass mark za D? Hii fani inaonekana ni simple sana kuliko fani zingine tofauti na tulivyokuwa tunatishwa zamani kwamba fani za afya ni ngumu na zinahitaji watu wenye akili. Kwa sasa fani hii ni kama shamba la bibi na fani ya vilaza na zoa zoa.
Please regulatory authorities tunaomba mliangalie hili maana afya zetu ni muhimu sana.
Kichwa cha habari kinahusika, miaka ya nyuma mtu ulikuwa ukifeli au kupata ufaulu hafifu unaambiwa hata ualimu umeshindwa? Lakini kwa miaka ya hivi karibuni naona trend imehamia kwenye fani ya Afya na Tiba.
Just imagine fani nyeti kama afya ila pass mark za udahili ni kuwa na D D D kwenye masomo yanayoitwa ya sayansi. Kuna watu watesema eti hiyo ni minimum pass mark lakini wanasahau kwamba wanafunzi wengi wanaangukia kwenye ufaulu huo na kudahiliwa ngazi ya Diploma alafu baadae wanakuwa Medical Doctor baada ya kujiendeleza.
Binafsi naamini mtu mwenye uelewa mdogo au ufaulu finyu hata ajiendeleze ataishia kuwa mtaalam wa average tuu. Bahati mbaya watu wa hivi ndio wamejaa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, na hii kazi saizi imevamiwa na kila mtu sio kazi ya wito na kujitoa bali kazi ya kusaka pesa.
Watu wenye uelewa finyu ndio tunategemea wagundue chanjo ya corona na kufanya operation complex, huu ni utani na kuchezea afya zetu. Hawa ndio mara nyingi unakuta wanagombana na kutoleana maneneo machafu na wagonjwa. Pia kwa watu wa hivi pesa mbele huduma inafuata. Binafsi nikienda hospital au dukani nikakuta vile vitoto vyenye D 3, huwa siko tayari vinihudumie kwenye ishu za msingi labda kupima pressure na maabara ila prescriptions hapana, huwa niko tayari kughairi huduma na kutafuta kwingine au nimpigie simu daktari naemfahamu hakupitia huu utaratibu wa D 3.
Kana kwamba haitoshi saizi kumezuka vyuo uchwara kila kona vinavyotoa haya mafunzo ya fani za afya almaarufu Health and Allied Sciences, sayansi zipi na pass mark za D? Hii fani inaonekana ni simple sana kuliko fani zingine tofauti na tulivyokuwa tunatishwa zamani kwamba fani za afya ni ngumu na zinahitaji watu wenye akili. Kwa sasa fani hii ni kama shamba la bibi na fani ya vilaza na zoa zoa.
Please regulatory authorities tunaomba mliangalie hili maana afya zetu ni muhimu sana.