Familia za watuhumiwa ni sababu kubwa ya watu kushikiliwa na Polisi bila dhamana

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Sijui wangapi mna ‘personal experiences’ za kushikiliwa na Polisi kwa kosa lolote lile.

Ni kweli Watanzania wengi ni wanyonge sana hasa wanapokuwa mbele ya dola. Hata wenye hela huwa ghafla wanageuka wanyonge hata haki zao zinapogandamizwa.

Kwa mazingira na mazoea ya Kitanzania, bado wengi wetu, si wenye nchi, si Polisi na hata si Mahakama wanaoelewa na kuheshimu dhana ya ‘innocent until proven guilty’.

Mfano, wengi hawaheshimu haki ya mtuhumiwa ya kwamba hata ukishakuwa katika mikono yao, una haki ya kutozungumza chochote mpaka wakili wako awepo.

Familia inachotaka ni kuona uko huru. Wakifika kituo cha polisi, wataanza kuwapa polisi hela za chai, watazungumza kinyongenyonge, wakati huo huo maafande wanazidi kukaza kwa kauli zao. Na hapo ukute kesi yako inahusisha wasiojulikana, kesi yako kimsingi haiko polisi.

Masaa 24 yanapita, 48, 72, unakuja kugundua wiki 2, mtu wenu hajafikishwa mahakamani wala hajaachiwa. Wakili wenu yupo yupo tu na ndiyo kwanza familia inamwambia atulie, yatakwisha tu haya, hawataki kushindana na dola.

Mara nyingi familia zetu ndiyo zinalea tabia hii ya kushikilia watu hovyo hovyo bila kufuata sheria.

Myonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, ni rahisi kusema lakini siyo kutenda.
 
Bongo / africa hamna haki, kuna watu kibao wameishia kuumia kwa kupambania haki.
kama unaweza jinasua kwa namna yoyote iwe kwa pesa au kingine ni heri kuliko kupambana na watu wasio na huruma.
 
Bongo / africa hamna haki, kuna watu kibao wameishia kuumia kwa kupambania haki.
kama unaweza jinasua kwa namna yoyote iwe kwa pesa au kingine ni heri kuliko kupambana na watu wasio na huruma.
Ila mambo haya wakati mwingine yanalipika hapa hapa. Nakumbuka Hassan Al Bashir alipotupwa ndani alilalamika mbona mnaniweka kwenye gereza ambalo halina hadhi ya kumuweka binadamu?
Lakini yeye ndilo aliwafungia wapinzani wake tena kwa uonevu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mbali na kusali kwa ajiri ya kuombea njia salama uendako hakikisha unasali kuepukana na matatizo na serikali,mtu mwingine,au hata watu wengine.

bro kwanza nikukosoe unapotaja unyonge kama sababu ya kutoa hela.si hivyo watu hawapendi mlolongo.fikiria umepigana na konda asubuhi wakati unaenda zako mihangaiko ukawekwa polisi,hata kama polisi ni ndugu zako lazima ufikirie kuingia mfukoni usafishe njia maisha yaendelee.maana huo mlolongo wa mahakamani kusikilizwa na kutafuta ushahidi,utakula wiki kadhaa,wakati huo mambo yako yanasimama.

haya mambo ukitaka uyaelewe,yapo sana barabarani kwa watu wenye vyombo vya usafiri,unavunja bumper,unatoa laki 3,wakati mahakamani mambo yangekiwa mteremko.
 
Ila mambo haya wakati mwingine yanalipika hapa hapa. Nakumbuka Hassan Al Bashir alipotupwa ndani alilalamika mbona mnaniweka kwenye gereza ambalo halina hadhi ya kumuweka binadamu?
Lakini yeye ndilo aliwafungia wapinzani wake tena kwa uonevu

Sent using Jamii Forums mobile app
usikariri pambana upate msuli,vinginevyo utaonewa kila siku na usishuhudie mtesi wako akifikwa na chochote.
 
hawa jamaa hawana utu

nobody wanna mess with them.

KISA:jamaa yangu ni fundi simu yy na msaidizi wake walikamatwa na simu ya wizi aliyoletewa kutengenezaa,nilienda kuwawekea mdhamana na nilikidhi matakwa yao...

hata baada ya kukidhi vigezo hao ndugu waliendelea kushikiliwa kwa siku mbili zaidi:lakini ilipotolewa 20k waliachwa muda huo huo;japo awali tulishakubaliana kulipa simu na gharama za wao kuifuatilia

usiwalaumu ndugu;tuko bongo ndani ya Afrika:wakati mwingine INABIDI


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii tabia imeota mizizi kwa sababu inaanzia juu na kushuka chini,Africa hakuna utu wala haki ,visa,visasi na ubabe ndio vimetawala ndio Mana wanasema police kuingia ni bure ila kutoka ni hela hata kama huna hatia, wananyanyaswa watu wenye wanasheria nguli na mpunga, sembuse akina pangu pakavu,
Alieshika mpini ndio anaamua cha kumfanya aliyeshika makali
 
Back
Top Bottom