kopites
JF-Expert Member
- Jan 28, 2015
- 8,371
- 10,010
Sass mlitaka wakasome chini ya mti au?Mimi na mwenza wangu,na watoto wangu wawili tumeshajiunga chuo kikuu cha Dodoma ili tuweze kupata PhD za Voda fasta
Wana ccm wenzangu hii ni fursa, Bahati hazipatikani kirahisi, Jiungeni na chuo kikuu cha Udom mapema kujipatia PhD
Udom ni chuo Kikuu pekee ambacho kinatoa nafasi na PhD za haraka haraka kwa wanasiasa kama mimi
Tunatumia nafasi hii vizuri kabla mambo hayajageuka hapo mbeleni
Shule ni shule tu, Huku mtaani uwe umesoma Oxford, Harvard au Cambridge kinachotakiwa ni CONNECTION TU
Siungi mkono PhD uchwara kama hizi lakini kuna muda inabidi ucheze na mdundo au Beat linavyotaka
Kama DJ ameruhusu kuruka ruka ukimbuni, Mimi nani nikatae PhD ya bure toka Udom
Udom ni sehemu pekee kwa watu sasa kujipatia PhD
karibuni Udom sana
Mpaka mwaka 2025 kila mwanasiasa atakuwa anaitwa Dokta
Hapo mwakani nitaitwa Mheshimiwa, Dokta Gussie (PhD udom 2022)