Familia ya Nyerere yaikana CHADEMA

habari zilizoripotiwa na gazeti la habari leo ni kuwa mmoja wa wanafamilia ya Nyerere ametoa tamko la kuikana chadema na kusema kwamba chama hicho kisitumie jina na kaburi la hayati Nyerere kujipatia umaharufu wa kisiasa! pia amesisitiza kwamba wao kama familia hawaungi mkono maandamano ya chadema na hawana uhusino wowote na chadema.
TAHARIFA RASMI NI HII;

WAKATI Watanzania wakizidi kujitokeza kulaani maandamano ya kichochezi ya Chadema, familia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, imeelezea kushangazwa na uongo wa viongozi wa chama hicho, kwamba familia hiyo inakiunga mkono.

Mbali na kuelezea kilichotokea wakati viongozi wa chama hicho walipotembelea familia hiyo hivi karibuni, pia imekemea mbinu za kutumia kaburi la Baba wa Taifa kujipatia umaarufu.

Kwa mujibu wa taarifa ya familia hiyo, tofauti na ilivyotangazwa na vyombo vya habari vinavyoshabikia maandamano hayo, familia hiyo haikuunga mkono maandamano hayo na badala yake ilisisitiza umuhimu wa kuzingatia utaratibu wa Serikali na kudumisha utulivu.

Akitoa taarifa hiyo jana, mmoja wa wanafamilia hiyo, Makongoro Nyerere, aliweka bayana kwamba familia hiyo haijaunga mkono Chadema kwa mambo inayoendelea nayo sasa, ikiwamo maandamano yaliyoendeshwa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kwamba chama hicho kimepata baraka na kuombewa dua yenye lengo la kuungwa mkono na mjane wa Mwalimu Nyerere, Mama Maria na familia yake kwa lengo la kukitabiria ushindi.

Makongoro, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mara, akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM ya Mkoa kilichoshirikisha wajumbe na wabunge wa CCM wa mkoa huo, alisema kilichofanyika Butiama ni utaratibu wa kawaida wa kupokea wageni wanaotembelea kaburi la Mwalimu.

Source: Habari leo. Hilo ni gazeti la mafisadi kazi yao ni kuandika pumba tu. Tulishaona kwenye TV (ITV) na vyombo mbalimbali vya habari siku CHADEMA walipoenda kutembelea kaburi la hayati baba wa taifa, JK Nyerere, mpaka mmoja wa watoto wa Nyerere akatabiri kuwa 2015 CHADEMA watashinda uchaguzi, sasa hizo habari za habari leo ni udaku mtupu na hazina mashiko! Kutembela kaburi la baba wa Taifa ni heshima tu CHADEMA hawakufanya hivyo kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa kwasababu wao sio wa kwanza kufanya hivyo!!
 
Huyu Makongoro Nyerere ndiye aliyeanza kuonyesha kuwa inawezekana kabisa kwa familia ya Nyerere kupokea mabadiliko ya kisiasa pale alipojiunga NCCR mwaka 95!Kwa hiyo ingawa kwa sasa kweli yupo ccm na ana cheo kikubwa tu,asipingane na kauli ya mwanafamilia mwenzake badala yake aiheshimu!Vilevile cdm kama chama hakijawahi kutoa tamko linaloonekana kama kinatumia kaburi au jina la Nyerere vibaya.Chama pekee kwa sasa ambacho kinafuata misingi ya baba wa taifa kwa vitendo ni cdm.Hata hivyo badala ya kuibeza cdm,maköngoro angeonesha uungwana hata kidogo kuisifu kwa kupigania nchi irudi kwenye misingi ya utu,haki na usawa kama jinsi mwalim mwenyewe alivyotaka.Vilevile kujaji kitu kwa kutumia habari leo tuwe makini kwa kuwa ni moja ya vyombo vya kueneza propaganda za ccm kama ilivyo TBC.
 
Hiyo habari sio ya kweli mana mpaka kuna video kijana wa nyerere akiisifia chadema.huu ni uchakachuaji wa ccm
 
Habari leo, huu ugali wenu mnachukua siku ngapi kuupika?! Poleni sana hatuwezi kuula huu, mmechelewa sana. Siku nyingine jaribuni kuwahisha labda wapo watakaoonja kidogo!!!! Ila huu wa leo kuleni wenyewe mvimbiwe.
 
Kashaga inawezekana una tabia mbaya tena sana wewe unajua kuwa nyumba yako tunaijua wewe?Acha ujinga kwani maisha yako unayaweka rehani kwa mawazo yako ya kishabiki.
 
TAHARIFA RASMI NI HII;

WAKATI Watanzania wakizidi kujitokeza kulaani maandamano ya kichochezi ya Chadema, familia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, imeelezea kushangazwa na uongo wa viongozi wa chama hicho, kwamba familia hiyo inakiunga mkono.

Mbali na kuelezea kilichotokea wakati viongozi wa chama hicho walipotembelea familia hiyo hivi karibuni, pia imekemea mbinu za kutumia kaburi la Baba wa Taifa kujipatia umaarufu.

Kwa mujibu wa taarifa ya familia hiyo, tofauti na ilivyotangazwa na vyombo vya habari vinavyoshabikia maandamano hayo, familia hiyo haikuunga mkono maandamano hayo na badala yake ilisisitiza umuhimu wa kuzingatia utaratibu wa Serikali na kudumisha utulivu.

Akitoa taarifa hiyo jana, mmoja wa wanafamilia hiyo, Makongoro Nyerere, aliweka bayana kwamba familia hiyo haijaunga mkono Chadema kwa mambo inayoendelea nayo sasa, ikiwamo maandamano yaliyoendeshwa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kwamba chama hicho kimepata baraka na kuombewa dua yenye lengo la kuungwa mkono na mjane wa Mwalimu Nyerere, Mama Maria na familia yake kwa lengo la kukitabiria ushindi.

Makongoro, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mara, akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM ya Mkoa kilichoshirikisha wajumbe na wabunge wa CCM wa mkoa huo, alisema kilichofanyika Butiama ni utaratibu wa kawaida wa kupokea wageni wanaotembelea kaburi la Mwalimu.

habari yenyewe inanuka udaku-udaku tu. hakuna nukuu hakuna nini.

hivi makongolo anatumia bia gani?
 
Sasa huyo Makongoro Nyerere alikuwa wapi wakati kaka yake pamoja na Mama yake walipokuwa wakitoa maoni yao pale Butiama wakati wa ziara ya viongozi wa CHADEMA? Tumeona Video ikitolewa kwenye TVs za hapa Bongo, it's too late Sir. Na tangu lini Makongoro akawa msemaji wa familia ya Nyerere?
Amagito gano SISIEMU gapumbafu.
 
Chadema ni maarufu tayari kutokana na sera zake haiwezi kutegemea kaburi kupata umaarufu wala famalia fulani.Nseme ivi Chadema songa mbele wala msikate tamaa kwa maneno ya shombo.Tupo nyuma yenu!
 
nakubaliana na wanaosema thread kama hizi zisiwekwe pale tumeshapoteza ma great thinkers kibao tusikubali kupoteza wengine kwa kugeuza hapa kuwa ni rumour mills, tuliona hizi propaganda za kimaslahi za wakina salva hazina nafasi kwetu. Wasitufanye tuanze kumchambuo makongoro kwa sababu tunaouwezo huo, alikuwepo na aliwaka neno na kupongeza, kila familia ina guinea pig wake huyo ni wa wakina Nyerere, alisema Leticia asitumie jina la mume wake madaraka lakini madaraka hajakaza hilo, amemuacha hakimu Arusha kwa kushindwa kumuhudumia, amekubali kuwa mmojawapo wa wana CCM 4m wanaokubali na kuangalia mtu mmoja JK akivuruga na kuua chama kilichoasisiwa na baba yake kwa posho isiyoweza hata kuwapa maisha ya heshima, heshima za kawaida tu za familia ya kawaida, ni nani anayejua maisha wanayoishi familia yake pale Msasani? kwanza akumbuke familia yake haitunzwi na chama inatunzwa na watanzania wote kwa kodi zetu ambazo hata hawazipati, sisi hatulalamiki kutunza familia ya baba yetu maana ametusomesha, ametufikisha hapa na kutupa maisha mazuri kuliko hata wa uzao wake, sasa atasema nini, atakikataaje chama ambacho ndugu yake ni mbunge, tena wa heshima kubwa? huyu tusimtetee kama kapandikiziwa maneno kwa nini asiyakanushe leo siku ya pili ama tatu? he is an embarassment to his late father, nahakika huko aliko baba yetu anageuka kaburini kwa habari hizi maana hakudhania angekua amezaa mtoto mjinga aneyeonea aibu kukemee mambo ya msingi aliyoyapigania baba yake, angesimama kwenye NEC na kumwambi mwenyekiti wake, haya sio baba aliyoyaamini na kuyapigania, hata kama angefukuzwa chama, angebaki na heshima na kuunyesha Umma kwamba he is his father son, legacy ya baba yake ingekua imekua protected. He is an embarassment tusimtetee ndio anaowapa hao wapumbavu wa Habari leo ambao naamini ndani yake kuna Salva mzee wa PR wa Dowans
 
CCM KIANZA CHOKOCHOKO JUU YA CHADEMA NA VYOMBO VYA DOLA KUTEKELEZA
AZMA YENU NA BASI SISI WANANCHI TUTAMALIZIA KWA
UFASAHA ZAIDI PICHA NZIMA HIVI KARIBUNI


Mheshimiwa Kikwete kidogo kachanganya mada hapa: kati ya Chama (CCM) kilichoshiriki, kupanga na kutekeleza njama za kuwapora wananchi HAKI YA KUCHAGUA viongozi wanaowapenda , upande mmoja, na kwa upande kuna chama (CHADEMA) kinachotekeleza wajibu wake wa kikatiba kushiriki kwenye kupiga mayowe kwa njia ya maandamano ya amani kote nchini kwa kudai kwa uchungu mkali kwamba Watanzania TUMEPORWA HAKI YETU YA MSINGI kikatiba; mpaka hapo ni chama gani kinastahili kufutwa usajili na kuchukuliwa hatua zote na vyombo vya dola???

Mbele ya 'Nguvu ya Umma' hakuna cha John Tendwa na ukada wake kwa CCM, Mrema na fadhila yake kwa uenyekiti wa kamati ya bunge, wala hakuna cha Maswahiba kama Said Mwema wala nani. Tunawasubirini kwa hamu muanze mchezo mzima ili mtakapoandika moja sisi tutaandika kumi na kuendelea.

Chonde msikose kutekeleza amri na busara za Kanali Kikwete, Kapteni Chiligati na Luteni Kanali Makamba maana hiyo ni HARUSI AMBAYO tumekua tukiisubiri kwa muda mrefu sana mpaka hivi sasa sisi Vijana Nguvu kamili ya Umma.
 
mnategemea mwenyekiti wa ccm makongoro nyerere aitetee cdm? mmesahau wakati wa kampeni alimkana pia leticia nyerere na kumwita shemeji muasi simply kwa kuwa aligombea ubunge kupitia chadema? kwenye familia ya nyerere kuna ccm na chadema na pia nccr-mageuzi wana haki yao ya kidemokrasia.
 
Mbona iyo aina tatizo pale ilikua stop by, move iko palepale, CCM mnatapatapa mwisho wenu umefika non stop, iyo imekula kwenu iyo aitusumbui. waseme wasiseme tumeshapiga bao ujumbe umesha fika, mbona mmechelewa kutoa tamko au mlikua mnachakachua kama kawaida yenu.
 
Hee hivi kuna Watanzania wamejitokeza kupinga maandamano? zaidi ya Mwenyekiti wa C.C.M na wenda wazimu wengine kama KASHA GA?
Wapo, Mrema, Wasira, Makamba, JK, na yule kigeugeu wa Temeke aliyenunuliwa kutoka CUF, nani yule, nani nani nani.....yule mropokaji mashuhuri anayeshindana na Makamba. Wapo japo wengine wanasemea mvunguni kuifagilia CHADEMA lakini wanapayuka kila wakimwona mwandishi wa habari yeyote wasikike. Si unajua tena? Unaweza kupata ukuu wa Tarafa.
 
Sis ni kama wanamapindunzi na wakeleketwa wa Chama cha Chadema.Tunachosema ni hivi "Hatuwezi tema jojo kwa karanga za kuomba"Hilo gazeti walilosoma wao ni lip?Mbona Vyombo vya habar vilirush matulio live sas huko kukanush kwenu kunatok wap?
 
Kashaga inawezekana una tabia mbaya tena sana wewe unajua kuwa nyumba yako tunaijua wewe?Acha ujinga kwani maisha yako unayaweka rehani kwa mawazo yako ya kishabiki.

dogo unanitishia maisha au? tanzania ni nchi ya demokrasia na kila mtu ana uhuru wa kufuata chama anachokitaka so mimi nishachagua changu na usinibabaishe kama chama chako kinabelieve kwenye vurugu na kutishia watu kama unavyofanya am very sorry hakitafika mbali
 
nakubaliana na wanaosema thread kama hizi zisiwekwe pale tumeshapoteza ma great thinkers kibao tusikubali kupoteza wengine kwa kugeuza hapa kuwa ni rumour mills, tuliona hizi propaganda za kimaslahi za wakina salva hazina nafasi kwetu. Wasitufanye tuanze kumchambuo makongoro kwa sababu tunaouwezo huo, alikuwepo na aliwaka neno na kupongeza, kila familia ina guinea pig wake huyo ni wa wakina Nyerere, alisema Leticia asitumie jina la mume wake madaraka lakini madaraka hajakaza hilo, amemuacha hakimu Arusha kwa kushindwa kumuhudumia, amekubali kuwa mmojawapo wa wana CCM 4m wanaokubali na kuangalia mtu mmoja JK akivuruga na kuua chama kilichoasisiwa na baba yake kwa posho isiyoweza hata kuwapa maisha ya heshima, heshima za kawaida tu za familia ya kawaida, ni nani anayejua maisha wanayoishi familia yake pale Msasani? kwanza akumbuke familia yake haitunzwi na chama inatunzwa na watanzania wote kwa kodi zetu ambazo hata hawazipati, sisi hatulalamiki kutunza familia ya baba yetu maana ametusomesha, ametufikisha hapa na kutupa maisha mazuri kuliko hata wa uzao wake, sasa atasema nini, atakikataaje chama ambacho ndugu yake ni mbunge, tena wa heshima kubwa? huyu tusimtetee kama kapandikiziwa maneno kwa nini asiyakanushe leo siku ya pili ama tatu? he is an embarassment to his late father, nahakika huko aliko baba yetu anageuka kaburini kwa habari hizi maana hakudhania angekua amezaa mtoto mjinga aneyeonea aibu kukemee mambo ya msingi aliyoyapigania baba yake, angesimama kwenye NEC na kumwambi mwenyekiti wake, haya sio baba aliyoyaamini na kuyapigania, hata kama angefukuzwa chama, angebaki na heshima na kuunyesha Umma kwamba he is his father son, legacy ya baba yake ingekua imekua protected. He is an embarassment tusimtetee ndio anaowapa hao wapumbavu wa Habari leo ambao naamini ndani yake kuna Salva mzee wa PR wa Dowans

kwanini zisiwekwe? tuambieni publically kwamba JF ni ya chama fulani tuu dunia nzima ifahamu ili wale wasiohusika wasikanyage coz mi njua jf ni public forum kila mtu mwenye hoja yake anaewza toa hatakama hoja hiyo haigemei chama fulani
 
Hayati Julius Nyerere did his part. He is gone. He is history.

CDM will stand. It is doing its part. Familia ya Mwl. Nyerere inaheshimiwa sio kwa sababu kama familia kuna lolote la kujisifia wamefanya ila ni kwa sababu ya Mwl. Nyerere. Wao ni familia SIO Nyerere.

Hata wakisema wanaisupport CDM au hawasupport sio suala la msingi. Wao kama watanzania wana maamuzi yao, na maamuzi yao yanaonekana. Wako CCM. Hatuwezi kuwatofautisha na wenzao au chama chao kwa sababu eti ni familia ya Mwl. Nyerere.

Kama bado wanaiamini CCM waendelee. Wananchi wataamua wao wenyewe sio kwa kuwaangalia wao.
 
Back
Top Bottom