Pinkman
JF-Expert Member
- Aug 23, 2017
- 707
- 1,538
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amepongeza familia ya Rais wa kwanza wa nchi hiyo Nelson Mandela kwa kusema wazi kwamba binti yao, Zindzi, alikufa kwasababu ya ugonjwa wa virusi vya corona, Jumatatu.
Hilo litafanya jamii kutonyanyapaa wanafamilia waliopata maambukizi, Bwana Ramaphosa amesema.
Zindzi alizikwa Ijumaa asubuhi kando ya kaburi la mama yake ambaye pia alikuwa mwanaharakati aliyepinga ubaguzi wa rangi Winnie Madikizela-Mandela
Afrika Kusini ni moja ya nchi za Afrika iliyopata maambukizi ya juu ya ugonjwa wa virusi vya corona ikiwa na zaidi ya maambukizi 320,000
Kumekuwa na zaidi ya vifo 4,600 na serikali imekadiria kwamba idadi hiyo inaweza kuongezeka hadi 50,000 kufikia mwisho wa mwaka huu.
Licha ya kwamba raia wamefahamishwa kuhusu vile virusi vya corona vinavyosambaa, dalili na athari zake bado kumekuwa na taarifa za unyanyapaa dhidi ya waliopata maambukizi.
Rais Ramaphosa amesema nini?
"Ningependa kushukuru familia ya Mandela kwa mfano mzuri wa kushirikisha taarifa hizi na taifa. Hivi ni virusi ambavyo vinaathiri kila mmoja, na hakustahili kuwa na unyanyapaa wowote miongoni mwa waliopata maambukizi," alituma ujumbe kupitia mtandao wa Twitter kabla ya mazishi ya Zindzi Mandela.
Aliongeza kwamba kusema wazi sababu ya kifo chake, ni ishara ya mshikkamano wa juu zaidi kwa mwanamke aliyejitolea maisha yake kwa raia wenzake wa Afrika Kusini."
Hilo litafanya jamii kutonyanyapaa wanafamilia waliopata maambukizi, Bwana Ramaphosa amesema.
Zindzi alizikwa Ijumaa asubuhi kando ya kaburi la mama yake ambaye pia alikuwa mwanaharakati aliyepinga ubaguzi wa rangi Winnie Madikizela-Mandela
Afrika Kusini ni moja ya nchi za Afrika iliyopata maambukizi ya juu ya ugonjwa wa virusi vya corona ikiwa na zaidi ya maambukizi 320,000
Kumekuwa na zaidi ya vifo 4,600 na serikali imekadiria kwamba idadi hiyo inaweza kuongezeka hadi 50,000 kufikia mwisho wa mwaka huu.
Licha ya kwamba raia wamefahamishwa kuhusu vile virusi vya corona vinavyosambaa, dalili na athari zake bado kumekuwa na taarifa za unyanyapaa dhidi ya waliopata maambukizi.
Rais Ramaphosa amesema nini?
"Ningependa kushukuru familia ya Mandela kwa mfano mzuri wa kushirikisha taarifa hizi na taifa. Hivi ni virusi ambavyo vinaathiri kila mmoja, na hakustahili kuwa na unyanyapaa wowote miongoni mwa waliopata maambukizi," alituma ujumbe kupitia mtandao wa Twitter kabla ya mazishi ya Zindzi Mandela.
Aliongeza kwamba kusema wazi sababu ya kifo chake, ni ishara ya mshikkamano wa juu zaidi kwa mwanamke aliyejitolea maisha yake kwa raia wenzake wa Afrika Kusini."