Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,543
Hizo nyumba za kule sio sehemu ya utajiri wake, ni nyumba za kijana wake, zilizonunuliwa kwa fedha kutokana na biashara halali za kundi la makampuni ya Alfa!.Hizi nyumba mbona hakuziweka kama sehemu ya utajiri wake? Au alijua hazitajulikana? Kama hili sakata ni la ukweli basi ndio ARIE TU!!!
Lowassa aweka wazi utajiri wake - Kitaifa - mwananchi.co.tz
Amesema wazi yeye anamiliki ng'ombe 800!.
Tenganisha mali za kampuni ya Alfa na mali zake binafsi!. Hata mimi, ninamiliki kijikampuni kinaitwa PPR, mimi mwenyewe naishi pale Kwa Mtogole kwenye nyumba ya kupangisha nimechukua upande nzima, nalipa laki kila mwezi!, na usafiri ninaomiliki binafsi ni boda boda moja na iko juu ya mawe tangu ile ajali!. Lakini PPR imepanga jengo zima la NHC pale mtaa wa Mkwepu, inalipa kodi ya TZS. 3,000,000 kwa mwezi, inamiliki magari, inamiliki vifaa vya digital production, na imeajiri watu zaidi ya 10!.
Nikulizwa mimi nina nini, nasema ukweli, sina kitu!, kwa sababu vile vitu ni vya PPR!. Vivyo hivyo Mzee wetu anamiliki ng'ombe 800 tuu!, vingine vyote ni vya Alfa!.
Pasco