voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,550
- 11,879
Nimesikiliza hizi clips mbili,Sound clip pamoja na video clip ya Mwanafamilia!
Kwa kutaka kulianzisha mnalolitaka!Ni wazi kuna ka asili ka visasi ndani ya ukoo ,na nimekuja na tafsiri moja tu!
Kwamba anatafutwa Musiba mwingine wa kuamgushiwa jumba bovu!
Kubalianeni na kazi au maamuzi ya Muumba wa mbingu na Ardhi,kila nafsi hapa Duniani itapitia mauti.
Kumbukeni Kama ilivyotokea kwa Huyo mpendwa wenu,ndivyo pia ilivyotokea kwa mpendwa wetu!
Na hata sasa vidonda bado vibichi kwa watanzania wengi sana.
Tena kwa huyu mpendwa wetu tuliambiwa na kuaminishwa kwamba yuko salama na anachapa kazi kama kawaida!
Tena tukatangaziwa kutoka ziarani Tanga!
Lakini kilichofuatia ni historia!
Mpaka leo watanzania hawajui ni nini hasa kilitokea!
Na familia ziko kimya pamoja na sintofahamu hizo!
Waliosema hayo ndio hao ambao leo wako maofisini wakiendelea na wanachokijua wao!
Sasa kutaka kuanza kumsakama Daktari huyo,ni sawa na kuanzisha ka-mfumo ambako na sisi tutakatumia ili tuambiwe ni nini kilitokea na kwa nini watanzania walifichwa huu ukweli!
Wale mlioshikiwa akili....Nimewakilisha hizo clips,ili mzitumie kujitakari na kuelewa ninaongea nini!
Mpishi wa Fitna,muanzilishi wa visasi ndie Mungu akamuanzishia mfano halisi!
Na ninaikumbuka ile kauli ya kwamba "Mungu Kaamua Ugomvi"
Ilitolewa huko huko Rondo!
Pia ile kauli "Hatasimama tena"
Pia ilitolewa na kundi hilo hilo!
Na ule Moshi kwenye Msafara ulianzia huko huko!