madindigwa
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 2,453
- 2,849
Pole sana mkuu maisha ndivyo yalivyo changamoto hayo yote yatapita Muombe MunguHabari wana JF,
Mie kijana wa kiume, naishi Dodoma! Nina mke na mtoto mchanga wa miezi 4. Kitaalum ni muhitimu wa Bachelor ya Computer Science, na nilikuwa nimeajiriwa sehem lkn tulipunguzwa kipindi kile janga la corona limepamba moto.
Sina kazi maalum kwa muda sasa, naunga unga tu kiukweli, nikibahatisha kupata kazi ya mtu binafsi mfano kutengeneza website au la kidogo imekuwa ikinibeba hasa kulipia kodi, lkn sijapata hizo kazi kitambo sasa! nimejaribu sana na bado naendelea kutuma maombi lkn sijafanikiwa, hali imekuwa ngumu kweli kweli kwetu! Nafanya vibarua sometimes hadi vya kubeba zege japo tu familia ipate mlo hasa mke anaenyonyesha!
Lakini saa nane kasoro hii usiku naandika hapa, tumelala njaa, leo nimejaribu vibarua bila mafanikio, hatuna hata sh. mia hapa ndani, imeniuma sana ndio maana nimekuja kwenu kuomba kazi, kibarua chochote halali hata cha kipato kidogo tu!
Mtoto wa miezi minne imebidi tu aanze kunywa uji maana mlo wetu mmoja kwa siku mama anakosa maziwa ya kutosha!
Mwenye chumba kanivumilia hadi kachoka kaniambia nikabidhi tu chumba, japo hii laptop naitumia kwa kazi zangu, lakn kama kuna mteja wana JF naiuza laki3, au kama kuna mtu anakopesha niiweke bond, atunusuru tafadhalini tunatolewa kwenye hii nyumba!
Nipo tayari kuja popote kufanya kazi/kibarua chochote halali! Naombeni sapoti nateseka sana, hasa huyu mzazi kulala njaa hivi inanipa stress sana!
Kwa mawasiliano, namba zangu 0767 960 255 au 0629 531 358.
Natanguliza Shukrani na Mungu atubariki!