Kwa kifupi umeongea mambo ya maana sana na ya msingi.@FaizaFoxy, : Dadangu, hata mie nimezaliwa na kulelewa ndani ya CCM. Nadhani tunahitaji mabadiliko. Sijui unafanya kazi serikalini, au wapi, Mie nafanya Private Sector, lakini baba yangu mzazi ni Waziri kwenye serikali ya Kikwete. Mama ni mtumishi wa serikali pia, lakini nakiri kwamba mabadiliko ni muhimu. Nimeondoka asubuhi na mapema kuja Arusha kujiunga na Wanaharakati na hali ambayo nimeikuta inasikitisha tamaa. Sitaki siasa za majungu za Ngeleja za kuchafua watoto wa makamba
Hebu fikiria tuliowapa madaraka wanavyojilimbikizia mali kwa wizi. Hebu tazama raia wa kawaida wanavyoonewa. Hali inatisha kwenye mahospitali, vyuo vikuu. Nchimbi katoa wapi utajiri wake, Loawassa, Chenge, Kikwete, Msekwa, Wakina Kinje Mwiru, Wakina Abdala kigoda listi ni ndefu. Watu wa EPA wanadunda mitaani, Richomnd hawajulikani. Dowans ni mapepo, TCRA, UDA listi ni ndefu aliyewajibishwa? Hakuna. liumba kaenda jela kwa sababu ya Demu siyo Ufisadi. Nchi gani hii Dada yangu? unachotetea ni nini? Ardhi inauzwa, rasilimali zetu zinachotwa, Rais ni kuzurura tu cha maana anachokifanyia taifa HAKUNA.
Mahakama zetu hazina haki, polisi ni majambazi. Sasa tukimbilie wapi? siwezi kuiunga CCM mkono kwa maslahi ya familia yangu au Baba yangu. Ni heri tuishi maisha ya zamani ya umasikini badala ya kuishi kama watumwa. Sitaki nife leo na kuwaacha wanangu watumwa kwenye nchi yao. siwezi kamwe. Sijui unao watoto, ila kama unao, hebu niambie nchi watakayoishi bada ya miaka 10 CCM ikizidi kukaa madarakani ni nchi ya aina gani. Ukiwa na uwezo na nia, sidhani hata CCM ikiondoka utakosa kazi, lakini ukiwa mchafu, lazima utayaona mabadiliko kuwa machungu. Sijui hupo upande gani, nijuzi dadangu.
Sijui wewe dada yangu au mdogo wangu ila hiyo haijalishi mimi ni (33) watoto wawili wakiume 7 na wakike 9 ambao naomba Mungu wakue na kusoma katika nchi yenye matumaini. Kwa sasa hata kama familia yangu ina uwezo wa kifedha, uwezo tulionao ni wa muda mfupi, kwani tumezungukwa na wengi masikini, kwa maana hiyo hakuna amani. Siwezi kuishi na kuitakasa CCM ni kuishi kitumwa. Na inaniuma sana kukuona kila mara ukishabikia CCM wakati unajua fika kwamba CCM inayumbisha nchi yetu. nilijifungua Aghakan, wewe sijui ulijifungua India lakini pia kumbuka mwanamke mwezio amejifungua kwenye sakafu Temeke.
Siyo mshabiki wa CHADEMA ila hata kama mabadiliko yataletwa na chama kingine, mara 100 afadhali kuliko kubaki kwenye utawala wa CCM. Sitazami maslahi yangu, natazama Maslahi ya watoto wangu na vitukuu vyao. Samahani sana lakini huo ndio ukweli wa mambo, nadhani kwenye utetezi wako wa CCM fikiria ukweli wa mambo. Ukiniita muhasi, basi waasi watakuwa wengi sana ndani ya CCM. Kama vipi mjadala uendelee....
Msisahau 15/11/2011 Hakuna kutumia Simu za TIGO..... Ni Wezi wanawanyonya walalahoi