denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,141
Unaposema bora CCM kuliko upinzani sijui kama unakumbuka 2015 walivyomfuata Lowassa Chadema? na hao hao tena wakaja kumfuata alivyorudi CCM? umetumia maneno "relatively better" kuhalalisha CCM iendelee kubaki madarakani, binafsi sioni huo unafuu unaouzungumzia kwa hiyo CCM.
Kwa upande wa upinzani; unaweza vipi kukilaumu chama kwa baadhi ya wanachama wake kununuliwa? hawa watu wananunuliwa kwasababu hawana misimamo wako selfish, hilo sio tatizo la chama, ni tatizo la watu binafsi, na hata wale waliokimbia CCM kumfuata Lowassa Chadema walienda kwa sababu zao binafsi, sio kosa la chama chao, ni ubinafsi wao.
Simply put; siasa za nchi yetu zimetawaliwa na wanasiasa wenye tamaa ya madaraka, na wako tayari kupata chochote wanachotaka bila kujali upande, wako wanaoondoka chama kimoja kwenda kingine kwa mapenzi yao binafsi, na wapo wanaoondoka chama kimoja kwenda kingine kwa kurubuniwa, tuliona hilo 2015, na tuona tena sasa 2020, na Mungu akipenda tutayaona tena mengine 2025 kutegemeana na upepo wa kisiasa utakavyovuma.
Mpaka pale wanasiasa wetu watakapostaarabika, wakaacha kuweka matumbo yao mbele kwa maslahi yao binafsi, wajue jukumu lao ni kuwatumikia wanatanzania, mtu akatae kuhama chama chake hata kama akirubuniwa kwa pesa, siasa zetu zitaendelea kuwa za maigizo tu, japo wako wachache wenye misimamo, wanatumika kama mfano.
Kwa upande wa upinzani; unaweza vipi kukilaumu chama kwa baadhi ya wanachama wake kununuliwa? hawa watu wananunuliwa kwasababu hawana misimamo wako selfish, hilo sio tatizo la chama, ni tatizo la watu binafsi, na hata wale waliokimbia CCM kumfuata Lowassa Chadema walienda kwa sababu zao binafsi, sio kosa la chama chao, ni ubinafsi wao.
Simply put; siasa za nchi yetu zimetawaliwa na wanasiasa wenye tamaa ya madaraka, na wako tayari kupata chochote wanachotaka bila kujali upande, wako wanaoondoka chama kimoja kwenda kingine kwa mapenzi yao binafsi, na wapo wanaoondoka chama kimoja kwenda kingine kwa kurubuniwa, tuliona hilo 2015, na tuona tena sasa 2020, na Mungu akipenda tutayaona tena mengine 2025 kutegemeana na upepo wa kisiasa utakavyovuma.
Mpaka pale wanasiasa wetu watakapostaarabika, wakaacha kuweka matumbo yao mbele kwa maslahi yao binafsi, wajue jukumu lao ni kuwatumikia wanatanzania, mtu akatae kuhama chama chake hata kama akirubuniwa kwa pesa, siasa zetu zitaendelea kuwa za maigizo tu, japo wako wachache wenye misimamo, wanatumika kama mfano.