‘Fair comments’ kuhusu CCM, Vyama mbadala na Uchaguzi wa Oktoba

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Kwenye siasa za Tanzania, kuna watu wanafanya wanachofanya kwa kuwa tu wanalipwa, kuna wengine kwa sababu ya ushabiki tu, wengine changamoto ya uelewa wa mambo, na wachache kwa sababu wanaelewa wanachokifanya na wanajua umuhimu wake kwao wenyewe, jamii na hatima ya Tanzania.

Kwa bahati mbaya, kundi la washabiki na wenye changamoto ya uelewa ndilo kundi kubwa zaidi ya hayo mengine na kupelekea tafiti mbalimbali kuonesha kuwa mara nyingi wapiga kura walio wengi wanakuwa hawajui wanachokifanya. Kwa mantiki hiyo, kuelekea kipindi cha uchaguzi kama sasa; ni muhimu kuyasaidia makundi haya kujua kipi ni kipi, ikiwaje matokeo gani yanatarajiwa na kwa nini. Ni muhimu kufanya hivyo kwa lugha rahisi ili angalau watakapoamua wajue wanaamua nini na ili iwe nini.

Dhana ya vyama mbadala nyakati za uchaguzi, haipo kwa ajili tu ya kuwapa watu uhuru wa kuchagua au kujifurahisha tu, bali kuchagua ambacho kina uafadhali Zaidi ya vingine. Hivyo basi ili kuepuka uwezekano wa kuchagua hatari Zaidi badala ya afadhali, ni muhimu kujiridhisha kwamba anachochagua mchaguaji ni bora kuliko unachokikataa.

Hoja ya kwamba unachokikataa mtu kina udhaifu fulani, hoja hiyo pekee haitoshi kuchagua mbadala wake, ispokuwa kama amejiridhisha kuwa huo mbadala ni bora zaidi. Kwa mfano, kama una simu inakaa na chaji masaa nane tuu, hilo linaweza kuwa ni tatizo lakini hilo peke yake haitoshi kuwa sababu ya kubadili simu hiyo, ispokuwa kama umejirishisha kwamba simu mbadala unayotaka kutumia inaweza kutunza moto zaidi ya hiyo ya awali.Kwa mantiki hiyo ni vyema kujenga uelewa juu ya hili kwa ajili ya makundi tajwa hapo juu.

Hili la kujenga uelewa ni muhimu sana maana makundi tajwa hapo juu ambayo ndio makubwa, hayawezi kuamua yakijua yanaamua nini 'Making rational and informed decisions' hivyo kufanya bahati nasibu 'Liwalo liwe'. Kwa bahati mbaya michakato inayozalisha viongozi hasa wa ngazi za juu wa kisiasa sio ya kufanyia bahati nasibu kwa kuwa hao ndio huamua hatma ya Maisha ya watu kwenye kila sekta.


=======
Inaendelea (Ni mjadala mpana sana, kwa hiyo tutaenda taratibu)
 
Kwa ushahidi na uzoefu tulioupata hadi sasa; tunaweza kusema ni salama zaidi kuendelea kuiunga mkono CCM kuelekea uchaguzi huu mkuu kuliko kinyume chake. Sio kwa sababu CCM ni tamu sana 'Perfect', bali kwa sababu CCM ni afadhali miongoni mwa vyama vilivyopo ‘Relatively better’. Yaani kwenye aina ya visima tulivyo nanyo, angalau maji yake yana uafadhali ukilinganisha na visima vingine.

Tutatumia maeneo makubwa kumi (10) kueleza ni kwa vipi tunaweza kufikia hitimisho hilo hapo juu. Maeneo hayo ni 1. dhana ya kujitambua kwa viongozi na wanachama, 2. Uwezo wa rasilimali watu ndani ya vyama, 3. Tabia za kundi, 4. Maono na jinsi yanavyowasilishwa kwa watu, 5. Kushaurika na kukosoleka, 6. Uwazi na uwajibikaji, 7. Uwezo wa kuishi demokrasia kwa matendo, 8.Usimamiaji wa haki za watu, 9. uwezo wa kutambua matatizo na kujaribu kuyatatua na 10. ushirikishaji wa wanachama kwenye maamuzi mbalimbali.

Maeneo haya yatachambuliwa kwa kina moja baada ya jingine na kufanya mlinganisho kulingana na vielelezo na ushahidi wa wazi ili kuweza kuelewa kwa nini hitimisho linaloelezwa hapa limefikiwa.
 
Kwa kuwa tushasema, tunachotaka ni kutoa 'Fair comments' na sio kufanya propaganda kwani tukifanya propaganda tutakuwa tushaingia kati kati ya makundi tajwa hapo juu (washabiki & wenye changamoto ya uelewa), tunatumia vigezo ambavyo vitatuwezesha kupima pande zote kwa mzani sawa na darubini yenye lensi zinazolingana.

Kwa mantiki hiyo, tutafanya ulinganifu katika level za vyama na sio serikali kwa sababu kwa kuwa vyama mbadala havijawahi kushika serikali; tukitumia kigezo cha usimamizi wa serikali kama kigezo kikuu cha upimaji, vyama mbadala havitakuwa na mizani ya kuvipima, kwa hiyo angalau kupima katika level za chama kuna uwanja sawa kwa vigezo tunavoelekea kuvitumia kupimia, na hivyo kuwa na mizania ya haki inayotupelekea kufikia hitimisho tunalofikia.
 
Saisa za bongo tunahitaji wapinzani wenye kuwaza maendeo tu na sio kuwalisha watu maneno mfano mbunge yuko bungeni badala ya kumbana waziri anakimbilia kutuma Twitter kwa wananchi kuwaambia eti wanatatizo flani badala ya kusema tatizo flani nimefikia hapa kulipambania
 
Nakuomba upokee ushauri kwamba kama inawezekana mada yako ifikie tamati hapo hapo ilipoishia na tafadhali usiendelee. Iwapo utaendelea please count me out, sina muda wa kupoteza!
Ombi lako halijakubalika kwa sababu halina mantiki.
Itaendelea kwa kadiri muda utakavyopatikana. Tatizo unadhani kwamba kila mtu yupo duniani kukutumikia na kukuridhisha wewe halafu wewe uko kwa ajili ya kutumikiwa na kuridhishwa. Wewe kama ukiona mada haikuhusu fanya yanayokuhusu, mengine achia wengine.

Kwa hiyo mada ikiendelea huna muda wakuchangia, ila isipoendelea utakuja kuchangia, hivyo unashauri isiendelee ili uje kuchangia, yaani kwa lugha nyingine uje kuchangia kitu ambacho kimsingi hakipo, sio?
 
Mtoa mada kaleta hoja nzuri wewe umekuja kucomment utumbo wewe unaweza ukawa sehemu ya tatizo aliyoainisha mtoa mada
@Azizimusa mtu Kama huyu unamsaidiaje?
Unampuuza tu, unaendelea na hoja ya msingi. Kulingana na Joel Nanauka, kuna watu ambao ni 'vision distractors' akiona unazungumza kitu cha msingi anachokifanya anakukatisha tamaa, au kukutoa kwenye hoja ya msingi ili uungane naye kujadili ujinga anaotaka. kwa hiyo unachopaswa kufanya ni kumpuuza.
 
Tukianza kuingia ndani sasa kwenye mizania yetu, tunaanza kuangalia dhana ya kwanza ambayo ni "kiwango cha kujitambua miongoni mwa viongozi na wanachama wa CCM na wale wa vyama mbadala".

Ijapokuwa ni vigumu kutoa hitimisho ambalo linaakisi uwezo wa kujitambua wa kundi kubwa la watu kwa kuwa kila mtu ana tabia tofauti na kwa kiwango tofauti, bado kuna vigezo mbalimbali ambayo tunaweza tukavitumia kujua chama kipi kina uafadhali dhidi ya kipi.

Kwa muktadha wa mada hii tutatumia vigezo viwili kupima uwezo wa kujitambua kati ya pande mbili tunazojaribu kuzilinganisha. Kigezo cha kwanza ni uwezekano wa kununulika dhidi ya uwezekano wa kununua, na uwezekano wa usaliti dhidi ya uwezekano wa kusimamia kile mtu anachoamini.

Kigezo cha kwanza kuhusu kununuliwa dhidi ya kununua; tumekuwa tukiona viongozi kadhaa wa vyama vya mbadala wakihamia CCM. Wao kwa maelezo yao wanadai wameona udhaifu kwenye vyama hivyo na wameona unafuu kwenye CCM lakini kwa maelezo ya vyama vyao ni kwamba wanakuwa wamenunuliwa na CCM. Tuchukulie kuwa maelezo ya vyama vyao ndio sahihi, na wanakuwa wamenunuliwa kweli.

Ijapokuwa kununua watu na kununuliwa yote sio mambo mazuri, Ni jambo la wazi kwamba kiongozi anayenunulika kirahisi kiwango chake cha kujitambua kiko chini kuliko anayenunua mwenzake. Hii haijalishi ni kwa nini mnunuaji ananunua na kwa nini mnunuliwaji ananunuliwa.

Kwa mantiki hiyo, kuelekea uchaguzi mkuu, ni afadhali kumuamini anayenunua walioko tayari kununuliwa (ikiwa kweli ananunua) kuliko kuamini anayenunulika kirahisi (ikiwa kweli ananunuliwa) kwa sababu anayenunulika leo hata kesho atanunulika na ni vigumu kujua atakayemnunua ni nani na kwa gharama gani.

Kuhusu kigezo cha pili cha usaliti, kumekuwa na sauti nyingi zaidi zikilalamikia usaliti ndani ya vyama mbadala kuliko CCM. Ikiwa wanaolalamikiwa kuwa ni wasaliti ni wasaliti kweli, na wanafanya usaliti wakiwa hawajapewa madaraka makubwa na imeshindikana kuwabadili katika level za vyama vyao, maana yake wakipewa madaraka makubwa zaidi ni ngumu kujua nani atakayemsaliti nani juu ya nini na kwa kiasi gani.

Ijapokuwa hata CCM kuna malalamiko ya usaliti, malalamiko hayo si kwa kiwango kile ambacho kinasikika kutoka kwenye vyama mbadala na kwa mantiki hiyo, tunaweza kusema kuna uafadhali kwa kiwango fulani.

Kama hayo mawili ni kweli, basi ni sahihi kusema wale ambao wananunua wengine wanajitambua kuliko wanaonunuliwa na wenye kiwango kidogo cha usaliti wanajitambua kuliko wenye matukio mengi wanayodai wenyewe ni ya usaliti.

Mtu anayejitambua zaidi ya mwenzake ana nafasi nzuri ya kuwa kiongozi bora zaidi ya mwenzake na hapo ndipo tunapokuja na hitimisho la uafadhali wa CCM ukilinganisha na vyama mbadala.
 
Kwenye siasa za Tanzania, kuna watu wanafanya wanachofanya kwa kuwa tu wanalipwa, kuna wengine kwa sababu ya ushabiki tu, wengine changamoto ya uelewa wa mambo, na wachache kwa sababu wanaelewa wanachokifanya na wanajua umuhimu wake kwao wenyewe, jamii na hatima ya Tanzania.

Kwa bahati mbaya, kundi la washabiki na wenye changamoto ya uelewa ndilo kundi kubwa zaidi ya hayo mengine na kupelekea tafiti mbalimbali kuonesha kuwa mara nyingi wapiga kura walio wengi wanakuwa hawajui wanachokifanya. Kwa mantiki hiyo, kuelekea kipindi cha uchaguzi kama sasa; ni muhimu kuyasaidia makundi haya kujua kipi ni kipi, ikiwaje matokeo gani yanatarajiwa na kwa nini. Ni muhimu kufanya hivyo kwa lugha rahisi ili angalau watakapoamua wajue wanaamua nini na ili iwe nini.

Dhana ya vyama mbadala nyakati za uchaguzi, haipo kwa ajili tu ya kuwapa watu uhuru wa kuchagua au kujifurahisha tu, bali kuchagua ambacho kina uafadhali Zaidi ya vingine. Hivyo basi ili kuepuka uwezekano wa kuchagua hatari Zaidi badala ya afadhali, ni muhimu kujiridhisha kwamba anachochagua mchaguaji ni bora kuliko unachokikataa.

Hoja ya kwamba unachokikataa mtu kina udhaifu fulani, hoja hiyo pekee haitoshi kuchagua mbadala wake, ispokuwa kama amejiridhisha kuwa huo mbadala ni bora zaidi. Kwa mfano, kama una simu inakaa na chaji masaa nane tuu, hilo linaweza kuwa ni tatizo lakini hilo peke yake haitoshi kuwa sababu ya kubadili simu hiyo, ispokuwa kama umejirishisha kwamba simu mbadala unayotaka kutumia inaweza kutunza moto zaidi ya hiyo ya awali.Kwa mantiki hiyo ni vyema kujenga uelewa juu ya hili kwa ajili ya makundi tajwa hapo juu.

Hili la kujenga uelewa ni muhimu sana maana makundi tajwa hapo juu ambayo ndio makubwa, hayawezi kuamua yakijua yanaamua nini 'Making rational and informed decisions' hivyo kufanya bahati nasibu 'Liwalo liwe'. Kwa bahati mbaya michakato inayozalisha viongozi hasa wa ngazi za juu wa kisiasa sio ya kufanyia bahati nasibu kwa kuwa hao ndio huamua hatma ya Maisha ya watu kwenye kila sekta.


=======
Inaendelea (Ni mjadala mpana sana, kwa hiyo tutaenda taratibu)
Mada yako ni nzito kweli, nashangaa wachangiaji wanapita tu kama haiwahusu.

Huna haja ya kuendeleza chochote kwenye mada hii, kwa sababu imejitosheleza kabisa; kinachotakiwa ni kwa wachangiaji kujaza hayo mengine unayoyawaza.

Mimi nichangie sehemu moja.

Katika vyama hivyo vyote, wananchi wanapochagua inabidi wachague wakijua kwamba chama wanachokichagua na kukipa madaraka, baadae kisiwageuke wananchi hao na kuwanyang'anya hata huo uwezo wao wa kuchagua.

Hili ndilo takwa kubwa zaidi kuliko mengine yote wanalotakiwa kulifahamu wananchi wa makundi yote.

Chama kinaposhika madaraka waliyopewa na wananchi, wasitumie madaraka hayo kuwanyima wananchi hao kufanya mabadiliko kama wananchi hawaridhiki na utawala wa chama hicho.

Wananchi wakiweza kuwa na ufahamu huo, vyama vyote vitabadilika na kuanza kufanya kazi za wananchi na kuheshimu haki za wananchi hao.

Hii ndio 'cardinal rule' ya kuwaelimisha nayo wananchi hao bila kujali wapo kundi gani kati ya hayo uliyoorodhesha hapo juu.

Sasa hivi CCM hawana shaka, wanajua polisi na bunduki ni zao. Wakurugenzi wote watakaotangaza matokeo ni wao. Kuna sababu gani tena ya CCM kuwa na kuhofu ya uwepo wa wananchi wasiojali na hawastushwi na kunyimwa haki zao za kuwachagua viongozi wanaowataka?

Ndio maana CCM wameridhika sana kwa uwepo wa kundi kubwa sana kati ya hayo yaliyopo kwenye orodha yako. Na wala hawana sababu ya kuwafanya sasa waanze kuwaelimisha wananchi kuhusu haki zao za msingi.

Kazi hii ilitakiwa ifanywe na taasisi husika; wakishirikiana na vyama vya upinzani. Haieleweki kwa nini na wao hawana msukumo wa kuifanya.
 
Mkuu,
Tukianza kuingia ndani sasa kwenye mizania yetu, tunaanza kuangalia dhana ya kwanza ambayo ni "kiwango cha kujitambua miongoni mwa viongozi na wanachama wa CCM na wale wa vyama mbadala".

Ijapokuwa ni vigumu kutoa hitimisho ambalo linaakisi uwezo wa kujitambua wa kundi kubwa la watu kwa kuwa kila mtu ana tabia tofauti na kwa kiwango tofauti, bado kuna vigezo mbalimbali ambayo tunaweza tukavitumia kujua chama kipi kina uafadhali dhidi ya kipi.

Kwa muktadha wa mada hii tutatumia vigezo viwili kupima uwezo wa kujitambua kati ya pande mbili tunazojaribu kuzilinganisha. Kigezo cha kwanza ni uwezekano wa kununulika dhidi ya uwezekano wa kununua, na uwezekano wa usaliti dhidi ya uwezekano wa kusimamia kile mtu anachoamini.

Kigezo cha kwanza kuhusu kununuliwa dhidi ya kununua; tumekuwa tukiona viongozi kadhaa wa vyama vya mbadala wakihamia CCM. Wao kwa maelezo yao wanadai wameona udhaifu kwenye vyama hivyo na wameona unafuu kwenye CCM lakini kwa maelezo ya vyama vyao ni kwamba wanakuwa wamenunuliwa na CCM. Tuchukulie kuwa maelezo ya vyama vyao ndio sahihi, na wanakuwa wamenunuliwa kweli.

Ijapokuwa kununua watu na kununuliwa yote sio mambo mazuri, Ni jambo la wazi kwamba kiongozi anayenunulika kirahisi kiwango chake cha kujitambua kiko chini kuliko anayenunua mwenzake. Hii haijalishi ni kwa nini mnunuaji ananunua na kwa nini mnunuliwaji ananunuliwa.

Kwa mantiki hiyo, kuelekea uchaguzi mkuu, ni afadhali kumuamini anayenunua walioko tayari kununuliwa (ikiwa kweli ananunua) kuliko kuamini anayenunulika kirahisi (ikiwa kweli ananunuliwa) kwa sababu anayenunulika leo hata kesho atanunulika na ni vigumu kujua atakayemnunua ni nani na kwa gharama gani.

Kuhusu kigezo cha pili cha usaliti, kumekuwa na sauti nyingi zaidi zikilalamikia usaliti ndani ya vyama mbadala kuliko CCM. Ikiwa wanaolalamikiwa kuwa ni wasaliti ni wasaliti kweli, na wanafanya usaliti wakiwa hawajapewa madaraka makubwa na imeshindikana kuwabadili katika level za vyama vyao, maana yake wakipewa madaraka makubwa zaidi ni ngumu kujua nani atakayemsaliti nani juu ya nini na kwa kiasi gani.

Ijapokuwa hata CCM kuna malalamiko ya usaliti, malalamiko hayo si kwa kiwango kile ambacho kinasikika kutoka kwenye vyama mbadala na kwa mantiki hiyo, tunaweza kusema kuna uafadhali kwa kiwango fulani.

Kama hayo mawili ni kweli, basi ni sahihi kusema wale ambao wananunua wengine wanajitambua kuliko wanaonunuliwa na wenye kiwango kidogo cha usaliti wanajitambua kuliko wenye matukio mengi wanayodai wenyewe ni ya usaliti.

Mtu anayejitambua zaidi ya mwenzake ana nafasi nzuri ya kuwa kiongozi bora zaidi ya mwenzake na hapo ndipo tunapokuja na hitimisho la uafadhali wa CCM ukilinganisha na vyama mbadala.
utaiharibu mada yako nzuri bure, kwa sababu unaingiza 'dhana chonganishi' nyingi mno!

Kwa mfano: "Mnunuzi awe nafuu ya anayenunuliwa", kweli?

Hebu nieleweshe sababu zinazofanya huko CCM wasiwepo wanaonunuliwa au wasaliti wanaohamia vyama vingine? Huoni kuwa ni rahisi sana kulieleza hili?

Hii mada yako itakuchosha sana ukitaka kuifanya kama 'lecture'. Itakuwa vigumu sana kupata darasa la kutosha.
 
Nakuomba upokee ushauri kwamba kama inawezekana mada yako ifikie tamati hapo hapo ilipoishia na tafadhali usiendelee. Iwapo utaendelea please count me out, sina muda wa kupoteza!
LOoo, sikujua kwamba alishapewa ushauri huu makini wakati nami nikimwaga wangu kule chini.
Nimeona akimjibu mmoja wa wachangiaji kukataa ushauri!

Sio kitu, mradi kisha shauriwa, ni juu yake kuukubali/kuukataa ushauri.
 
Kwa ushahidi na uzoefu tulioupata hadi sasa; tunaweza kusema ni salama zaidi kuendelea kuiunga mkono CCM kuelekea uchaguzi huu mkuu kuliko kinyume chake. Sio kwa sababu CCM ni tamu sana 'Perfect', bali kwa sababu CCM ni afadhali miongoni mwa vyama vilivyopo ‘Relatively better’. Yaani kwenye aina ya visima tulivyo nanyo, angalau maji yake yana uafadhali ukilinganisha na visima vingine.

Tutatumia maeneo makubwa kumi (10) kueleza ni kwa vipi tunaweza kufikia hitimisho hilo hapo juu. Maeneo hayo ni 1. dhana ya kujitambua kwa viongozi na wanachama, 2. Uwezo wa rasilimali watu ndani ya vyama, 3. Tabia za kundi, 4. Maono na jinsi yanavyowasilishwa kwa watu, 5. Kushaurika na kukosoleka, 6. Uwazi na uwajibikaji, 7. Uwezo wa kuishi demokrasia kwa matendo, 8.Usimamiaji wa haki za watu, 9. uwezo wa kutambua matatizo na kujaribu kuyatatua na 10. ushirikishaji wa wanachama kwenye maamuzi mbalimbali.

Maeneo haya yatachambuliwa kwa kina moja baada ya jingine na kufanya mlinganisho kulingana na vielelezo na ushahidi wa wazi ili kuweza kuelewa kwa nini hitimisho linaloelezwa hapa limefikiwa.
Sikujua.

Kumbe mada yako umeiulia hapa?

Baada ya kusoma uliyoweka kwenye bandiko lako la mwanzo, nilipenda sana uwasilishaji wa mada ulioufanya. Kwa hiyo ndio nikajibu kwa mchango wangu hapo #12.

Ndipo nikaanza kusoma michango toka chini kupanda juu, hadi huu hapa ulioweka #2.

Inawezekana sana hili darasa ukabaki nalo mwenyewe, au na wasomaji wachache sana.
 
Saisa za bongo tunahitaji wapinzani wenye kuwaza maendeo tu na sio kuwalisha watu maneno mfano mbunge yuko bungeni badala ya kumbana waziri anakimbilia kutuma Twitter kwa wananchi kuwaambia eti wanatatizo flani badala ya kusema tatizo flani nimefikia hapa kulipambania
Subiria tu mwisho wa maji ni tope.
 
Naona umekuja na Theory nyingi za kutuaminisha kwamba CCM ndo wanastahili tu na hawa wengine hawastahili ni lini walipewa wakakosa vyote ulivyovisema hapo na kama ni utafiti tuambie ni wapi na nchi gani vyama vilishindwa kuongoza kwa ajili ya hayo mambo uliyoyataja. Naona kama ni uoga wako wa kihisia unataka kila mtu aamini hivyo chama cha Kagame kilikuwa kidogo ingawa yeye alianzia msituni leo wako vizuri kuliko lichama likubwa na lenye kila kitu.Waganda nao wanakuja NRM ya Museven ilitoka msituni kupigana pia leo ni chama kikubwa angali wanavyoisimamia serekali yao nakwambia siku Museven akistaafu kitakuwa chama kizuri zaidi na wakati kinaanza hakuwa na watu wa kutosha hata kuendesha nchi Watanzania wengi walienda kusaidia nadhani udogo sijui wa resources na propaganda nyingine ni uoga wa Chama Tawala na watu kama wewe unatumika kutufanya tuwe waoga wa mabadiliko
 
Back
Top Bottom