Faini ya Milioni 350 dhidi ya viongozi wa Chadema itumike kuwalipa fidia wazazi wa Akwilina

Geeque

JF-Expert Member
Aug 17, 2007
936
316
Hukumu iliyotolewa na hakimu wa mahakama ya Kisutu jijini Dar Es Salaam ikiwataka viongozi wa Chadema walipe faini ya shilingi milioni 350 itumike kuwalipa fidia wazazi wa marehemu Akwilina Akwiline. Haingii akilini hii pesa kurudi serikalini wakati waathirika wakubwa wa mauaji hayo yaliyofanywa na jeshi la Polisi la Tanzania ni familia ya marehemu Akwilina.

Ni muda muafaka kwa familia ya marehemu Akwilina kutafuta mwanasheria mzuri na kufungua kesi ya madai ya kifo cha mtoto wao mpendwa dhidi ya Jeshi la Polisi Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kesi hii ya madai ilenge kudai fidia kutokana na pesa zitakazopatikana kupitia faini hiyo.

Rais Magufuli amekuwa akijipambanua kuwa yeye ni rais wa wanyonge, basi huu ndio muda muafaka kuonyesha kwa vitendo upendo wake kwa wanyonge kwa kuagiza pesa zote zitakazopatikana kutokana na faini dhidi ya viongozi wa Chadema zilipwe kwa familia ya marehemu Akwilina Akwiline.

_100069499_76d3756a-0b0d-4286-8457-96a2800e8482.jpg
 
Kwani CDM wanahusikaje hapa? Fidia maana yake nini?
Japo unakumbusha machungu but wazo lako zuri, nakumbuka serikali iligharamia shughuli za mazishi pekee.

Mimi nimefikiria kwenye hii michango CHADEMA wanayochanga, vyema nao watoe kiasi fulani waipelekee hiyo familia japo kuwapoza kwa kukumbushwa mauaji ya mtoto wao.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Geeque,
UMEKOSA MTAJII WAMAISHA MNATAKAA KUCHANGIWA KUPITIA AKWILINA HIZO FAMILIA ZA AJABU AISEE PAMBANEN NA HALI ZENUU PESA ZA MAHAKAMA.SIO ZA MAHAWARA UNACHAGUA UMPE NANI
ALLAH ONDOA HIII KICHEFI CHEF
 
Geeque,

..sijui hili litakuchekesha au kukukasirisha.

..lakini serikali iliwavutia bomba la maji familia ya Akwilina.
 
Sheria inasemaje au unaropoka tu?

..Familia ya Lt.Gen.Imran Kombe ambaye aliuawa kimakosa na askari polisi wakati wa utawala wa Raisi Mkapa waliishtaki serikali na kulipwa fidia.

..kwa upande wa Akwilina familia yake inatakiwa ifungue kesi ya madai dhidi ya serikali. Kuna ugumu ktk kesi yao ambao sitataka kuutaja hapa, lakini they should try.

..mwingine anayepaswa kufungua kesi dhidi ya serikali ni familia ya muandishi wa habari Daudi Mwangosi ambaye aliuwa na askari wa kikosi cha kutuliza fujo wakati wa utawala wa Raisi Kikwete.
 
Kwani aliye muua akwilina ni nani? Maana hakuna mahali katika hukumu pameonesha kuwa viongozi wa CDM walikuwa na bunduki na kuwa walimuua Akwi. Maana hakuna shita la mauaji kwa viongozi hao. Waliokiri kumuua Akwi ni polisi.
Hukumu iliyotolewa na hakimu wa mahakama ya Kisutu jijini Dar Es Salaam ikiwataka viongozi wa Chadema walipe faini ya shilingi milioni 350 itumike kuwalipa fidia wazazi wa marehemu Akwilina Akwiline. Haingii akilini hii pesa kurudi serikalini wakati waathirika wakubwa wa mauaji hayo yaliyofanywa na jeshi la Polisi la Tanzania ni familia ya marehemu Akwilina.

Ni muda muafaka kwa familia ya marehemu Akwilina kutafuta mwanasheria mzuri na kufungua kesi ya madai ya kifo cha mtoto wao mpendwa dhidi ya Jeshi la Polisi Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kesi hii ya madai ilenge kudai fidia kutokana na pesa zitakazopatikana kupitia faini hiyo.

Rais Magufuli amekuwa akijipambanua kuwa yeye ni rais wa wanyonge, basi huu ndio muda muafaka kuonyesha kwa vitendo upendo wake kwa wanyonge kwa kuagiza pesa zote zitakazopatikana kutokana na faini dhidi ya viongozi wa Chadema zilipwe kwa familia ya marehemu Akwilina Akwiline.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom