Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 18,611
- 20,935
Binafsi sijafurahishwa na faini za bodaboda kushuka na kuwa 10,000/-kwani kwa jinsi ninavyowafahamu hawa ndugu zetu na rika lao,10,000/- itakuwa si chochote kwao na watadharau sana utaratibu wa barabara zetu hivyo huenda maafa yakawa makubwa zaidi kuliko vile itakavyofikiriwa.
Jambo lingine ambalo napingana nalo ni kuwa, bodaboda wengi kutokana na faini kuwa kubwa wanashindwa kukomboa pikipiki zao, sidhani kama hili lina mashiko maana nyingi ya pikipiki zinazoshikiliwa vituoni ni zile ambazo zinakuwa zimehusika na matukio mbalimbali yakiwamo ya wizi, ujambazi, aidha pikipiki hiyo kumilikiwa isivyo halali na anapotakiwa mwenyewe ajitokeze mhusika hukimbia mazima.
N.B: Sekta hii imeleta ajira nyingi Sana kwa vijana wetu na ujana ni maji ya moto na maafa yanayosababishwa na vyombo hivi hugharimu maisha ya wengi ambao ni abiria wa vyombo hivi, madereva wa vyombo hivi wanastahili mafuzo maalumu ya usalama barabarani kuliko hata madereva TAXI kama kweli tunawapenda usalama wao na abiria wao.
Jambo lingine ambalo napingana nalo ni kuwa, bodaboda wengi kutokana na faini kuwa kubwa wanashindwa kukomboa pikipiki zao, sidhani kama hili lina mashiko maana nyingi ya pikipiki zinazoshikiliwa vituoni ni zile ambazo zinakuwa zimehusika na matukio mbalimbali yakiwamo ya wizi, ujambazi, aidha pikipiki hiyo kumilikiwa isivyo halali na anapotakiwa mwenyewe ajitokeze mhusika hukimbia mazima.
N.B: Sekta hii imeleta ajira nyingi Sana kwa vijana wetu na ujana ni maji ya moto na maafa yanayosababishwa na vyombo hivi hugharimu maisha ya wengi ambao ni abiria wa vyombo hivi, madereva wa vyombo hivi wanastahili mafuzo maalumu ya usalama barabarani kuliko hata madereva TAXI kama kweli tunawapenda usalama wao na abiria wao.