Faida za Majina ya Mungu yaliyotumika kuumba na kauli zenye nguvu na Maajabu yake ya hali ya juu

BAADHI YA MAJINA NA KAULI ZA MWENYEZI MUNGU ZILIZOTUMIKA KUUMBA

View attachment 1101739

Yatakayo Elezewa:

1: majina ya kuamsha walinzi wa mbingu zote na faida zake

2: majina yaliyokuwapo kwenye fimbo ya Mussa na Nabii (Issa/Yesu) kufufulia wafu na kuponya na kauli alizotumia baba yetu Adam kuombea msamaha na faida zake

5: Majina ya kuamsha malaika wa Huruma Israfil

6: Majina yaliyopo kwenye Paji la uso wa malaika Jibril (Gabriel)

7: Majina yaliyofundishwa kwa malaika Mikail (Michael)

8: Majina yaliyofundishwa kwa malaika Izrail (Azrael)


Kwa kufupisha thread lisiwe refu zaidi kuna majina na kauli ambazo sitazungumzia wala kuorodhesha hapa kwa sababu mengi yatakuwa kama ni vitu vipya na watu hamtaelewa ninachozungumzia yanayotumiwa na kila malaika wa ardhini na mbinguni in short ni majina mengi nitakayojaliwa nitayajadili ili muweze kupata elimu,

Kwa kuanza:

MAJINA YA NGUVU YANAYOWEZA KUAMSHA WALINZI WA KITI CHA MWENYEZI MUNGU

Majina yenyewe ni ********************

Siwezi kuyadhihirisha hapa kwa sababu si ruhusa kuyaweka hadharani,kuna watu hutumia kwa kutaja taja hovyo.

Maana na maombi yake:
Ewe muumba, Mwenyezi mungu mmoja, wewe tu ndiye na unayestahiki kuabudiwa; wewe ni wa mwanzo na wa mwisho mwenye utawala wa kila kitu, wewe uliye hai bwana wa mabwana, mungu wa vyote muweza wa yote,mjuzi wa vyote, hakuna kisichotenda ila kwa mizani yako, wewe ndio unayepima tunayoona na tusiyoona...

Maarifa yake:
Tambua kwamba mwenyezi mungu akikujaalia kupokea maombi yako kwa majina hayo niliyoyaficha hapo basi ukiyasema hali ya kuwa mwili wako ni msafi,nguo na mazingira yako na moyo mmoja malaika wa mwanga/roho takatifu watakutokea mbele yako na kila kitu mbinguni na ardhini vitatetemeka kwa hofu ya mwenyezi mungu mmoja..
Na unaweza kuyatumia majina hayo kwa kuita nafsi yoyote unayotaka, kuingia kwa mkuu yoyote bila matatizo na kuskilizwa,kukubaliwa utakacho,kufunga midomo ya watu,kupokelewa posa na kukubaliwa hata kama kwa mtoto wa mkubwa yoyote,kukidhiwa haja utakayo,kutolea mapepo kwenye miili ya watu,kuita yoyote au kumrudisha unaemtaka,kukinga,kuponya maradhi yasiyotibika na chochote utakacho omba kitakubalika kwa Muumba wa Mbingu na Ardhi

Hii ni siri kubwa basi usiwafundishe wasiokuwa na dini wala wasiona huruma wala imani wakatumia vibaya na kunyonyea watu, hivyo katika kujifunza funza kwako ukiyapata majina haya ya kumuombea Mungu basi siri hii ifiche sio kila anayekuzunguka ni mwema au mwenye kufaa kujua.


2: MAJINA YA NGUVU KWENYE FIMBO YA MUSSA

Haya ni majina katika list ya pili ambayo muumba aliyaumbia malaika wenye kusifu utukufu wake na utakatifu, ndio haya Adam (rehema na amani ziwe juu yake) aliyasema na Allah akamsamehe kosa lake,
Pia ndio haya Nabii Issa mwana wa Mariam/Yesu mwana wa Maria (rehema na amani ziwe juu yake) aliyatumia kufufulia wafu na kuponya wana wa Izrael, alikuwa akiwaponya watu kwa ruksa ya Allah na kufufua kama ukiwa msafi ukayasema, milima itatetemeka kwa utukufu wake:


Majina na Kauli zenyewe ni *************

Maana na Dua yake:
Wewe ni muumba,tofauti na wewe hakuna Mwenyezi mungu,mtakatifu kabisa kwa wale wanaokukumbuka na kukutii,pekee katika kila kinachoonekana na kisichoonekana unabudiwa, mwenye utakaso mkubwa kabisa wenye kukosa mipaka,pekee ndiye unayeombwa,unaeongoza kwenye njia nyoofu na mwenye kuwapa wenye kutoa hakuna Mungu isipokua wewe, mjuzi zaidi wa wale wanaojua,hakimu wa wenye kuhukumu,mwenye msaada mkubwa kwa wale ambao msaada unawafaa,hakuna mungu isipokua wewe, umejificha kwa ulivyoviumba, umejiwekea sifa zote njema wewe mwenyewe, wewe pekee ndio mwenye kumiliki majina mazuri,umevifanya vitu kuwa kwa elimu na nguvu, unapoombwa unajibu, umehifadhi mwanzo na mwisho wa kila kiumbe, wewe ni mfalme,mwenye nguvu,Mmoja na wapekee,mmiliki wa vyote hakuna mungu unayemtegemea upo peke yako,umejawa na neno na kauli tu na ukitaka jambo kuwa linakuwa. Wewe ni Mungu Mjuzi na mkuu, moyo wa kila kiumbe upo mikononi mwako, na una uwezo wa kuvigeuza utakayo kwa kusema tu, kauli ni zile unazozungumza tu,utambuzi ni wako pekee. Hukumu, ni hukumu yako pekee, hakuna wa kupinga amri yako, hakuna wa kujua ambacho hujaruhusu ajue, Wewe ni wa Mwanzo na wa Mwisho,

FAIDA ZAKE:

Fahamu ewe ndugu yangu haya majina yalikuwa kwenye fimbo ya Mussa (rehema na amani ziwe juu yake) ni majina 31 kumi kila upande na la kati yao ndio mtu anaweza kufanya muujiza wowote na ndio jina kuu la siri la Mwenyezi mungu basi washindane na wanaoshindana hakika atakae lijua atafunuliwa mengi wanayoyajua watu na wasioyajua, na yote kwa ujumla basi huweza kufanya maajabu yenye kufungua loki zote za duniani,kuvunja uchawi na nguvu za giza,kufunga ndimi,kutawanyisha mapepo,kushinda maadui,na kuvuta malaika yoyote wa ardhini na makudam wowote wa mbinguni na ardhini,unaweza ukayatumia kwa kukuzia mazao,kukata chochote,kutenganisha,kupendwa,kuvuta waliombali,na kukidhi mahitaji yote, kwa nguvu ya Allah unatakiwa uyatumie kwa mambo ya haki tu,

Miongoni mwa maajabu yake ukiyaandika kwenye kioo kwa usiyekuwa na imani wala usiyesali na ukayalaza nje usiku saba kwa kufuata taratibu, basi kioo hicho unaweza ukakitumia kuita yoyote au chochote kikaja na ukaagiza unavyotaka au unaweza ukamuita yoyote na kumuuliza mambo yake na akakwambia hakuna utakachoita kikagoma kuja, pia unaweza kutumia kwa kutafuta ulichoibiwa na kikarudi na hazina zilizojificha,

Unapoyataja majina hayo basi malaika watakutokea kila mmoja wao mbawa zake zitakuwa mbili na moja inagusa mashariki mwa dunia na nyingine inagusa magharibi mwa dunia na wanaweza kufanya chochote unachotaka,

MAJINA YA NGUVU YA KUMUAMSHA MALAIKA WA HURUMA

Haya ni majina yanayohusiana na malaika wa huruma kuumbwa kwao na uwezo waliopewa malaika anaye yasimamia ni Israfil (Selaphiel) ambaye yeye yameandikwa katika paji lake la uso na ndiye aliyesimama katika upande wa kulia wa amri ya Mwenyezi mungu na anayesubiri kuamrishwa na Mungu kupuliza Baragumu siku ya Kiyama(siku ya hukumu) ambapo siku hiyo roho zote zitafunuliwa na kukufuliwa na kurudishiwa kila kitu chao kwa kuhesabiwa ukumu, Allah atukinge na siku hiyo nzito kwetu sote,
Na majina yenyewe ni:

***************************
MAANA YAKE:

Wewe ni mwenye nguvu, Je wapo wapi wenye nguvu? wewe ni mtukufu, wako wapi watukufu? wewe upo hai na unaishi, milele unajibu enyi makundi ya msaada kutoka kwa Mungu nijibuni,

FAIDA ZAKE:
Pindi utakapo yataja majina hayo ya siri ya mwenyezi Mungu ukiwa na moyo wa imani kwake na kwa mategemeo yake tu basi utaona ajabu ya Mungu kwa maana roho takatifu zitakushukia na kukutimizia lile linalompendeza Mungu lililopo kwenye akili yako au moyo wako muda huo huo na fahamu ya kwamba rafiki yangu mwenye imani ya Mungu mmoja ya kwamba ukiyasema majina hayo ya Mungu ukiwa na moyo msafi na roho yenye imani thabiti na Mungu basi ardhi hutetemeka na milima kutikisika kwa utukufu wa majina hayo ya Mungu na nafsi zote za malaika,majini,wanyama na roho vyote hukimbia haraka sana kukufuata kukutimizia kwa kuhitaji radhi za mwenyezi Mungu kupitia utakatifu wa sifa zake hizi na malaika watukufu waliobeba bendera za mwanga mweupe pia watafika na utawaona kwa unusu.
majina haya pia ndio majina ambayo ukiyatumia pia kwa mshambuliaji katika viumbe chochote basi hakiwezi kuzungumza wala kushindana na wewe hata kama ni simba au chochote cha hatari pia ndio haya haya ukilipata hata moja ukatumia basi utapata maajabu kama kushinda wivu,maadui,fitina na wahalifu kwa kujaliwa na mwenyezi Mungu unaweza pia kuyatumia kwa kufunga ndimi,kujikinga na maradhi au magonjwa yoyote yale ambayo ni tishio. hakuna malaika aliyepo ardhini ambaye akiskia unayataja majina haya akaacha kuja kukutizama wakati unataja.

Onyo:
Usithubutu kutaja majina haya kwa wakati upo vibaya,mchafu,na pia usitumie kwa yale yasiompendeza Mwenyezi Mungu sababu kubwa ya vijana na wazee wengi waganga au wenye imani thabiti za dini kuharibikiwa wao na vizazi vyao ni kutumia utakatifu wa Mwenyezi Mungu kwa machafu yao.

MAJINA YA NGUVU YALIYOPO KWENYE PAJI LA MALAIKA JIBRIL (GABRIEL)

Haya ni majina yaliyoandikwa kwenye paji la us la malaika jibril amani iwe juu yake, ambaye ni malaika wa mwenyezi mungu ambaye yupo pia katika amri za kulia za mwenyezi mungu ambaye yeye husubiri kuamrishwa kupeleka ujumbe kokote kule ambayo ndio yametumika kuumba malaika wote waliochini ya usimamizi wa Jibril na ambayo malaika hao huyatumikia pale yanapotamka na ukiwataka basi huja haraka zaidi na kukufanyia ulichowaitia haraka na ndio majina haya Issa bin Maryam (Yesu mwana wa Maria) alikuwa akiyatumia na kuyataja kwenye hafla maalum

Majina yenyewe ni:

*************************
Maana zake:
Utukufu upo kwako ewe bwana uliye hai, utukufu upo kwake ewe wa milele, utukufu upo kwako wewe mwenye kutegemewa, utukufu upo kwako wewe ambaye hujazaa wala kuzaliwa na usiyefanana na yoyote(chochote) hakuna Mungu unayemtumikia wala mwenye nguvu anayekusadia wala hakuna anayestahili kukuokoa, utukufu ni wako ewe mwenye nguvu na mkuu na mwenye uwezo juu ya kila kitu,

Faida zake:
Haya tamka uwezavyo mtake malaika yoyote unaemtaka uliza chochote fanya lolote lenye kumpendeza Mungu basi utaona ajabu kubwa ya mwenyezi Mungu, kila kitu unaweza kupata kwa sharti lile lile kwamba roho yako iwe ipo kwa yeye pekee unayemuabudu na uwe msafi mwili hadi roho

MAJINA SABA ALIYOFUNDISHWA MALAIKA MIKAIL (MICHAEL)

Kuna majina saba ambayo mwenyezi mungu alifundisha malaika mikail amani iwe juu yake ambayo yeye na malaika wote waliopo mbingu ya saba na waliosimama katika kiti cha enzi cha mwenyezi mungu mtukufu, malaika wa mwanga huyatumikia na ndio malaika wanaowafanikishia ushindi mitume wote katika mikono yao hawa kuna mikuki ya mwanga ambayo hupasuka kwa moto kwa wale wasiotii mambo ya kiroho na malaika wa duniani unapoyatumia kutaka kutimiziwa jambo na malaika hawa, basi wao hukujibu halaka sana na kufanya miujiza mikubwa sana na unaweza kutumia kwa mambo yaliyotakasika na kuwatuma wale malaika wanaosimamia majira (hali ya hewa) waliopo ardhini haya ndio majina pia yaliyopo kwenye paji la uso wa malaika Mikail amani iwe juu yake.

MAJINA YENYEWE NI:

************************************

MAANA ZAKE:

Utukufu ni wako ewe mungu mwenye nguvu utukufu ni wako ewe bwana wa mabwana,utukufu ni wako ewe unayefahamu hata majani mangapi yamedondoka mitini, utukufu ni wako ewe uliyefunikwa na vazi la utukufu na hekima, utukufu ni wako ewe unayehesabu kila uhai(pumzi) inayoingia na kutoka, ewe bwana wangu upo juu ya kila yale wanayokuzulia viumbe wako,

FAIDA ZAKE:

Fahamu ndugu yangu ya kwamba mwenyezi mungu ajalie utakapo fanikisha kuyasema kwa ufasaha majina haya basi jua kwamba malaika wa mwanga juu ya farasi wa mwanga waioshikilia mapanga ya mwanga watakutokea nao ni masters katika maswala ya kuchomelea mbali lolote, unaweza kutumia kwa kuponya,mafanikio,kinga,kuchoma,kuomba, kukata na kufunga ndimi, na kuita roho yoyote ile yote hayo utayafanya kwa ruhusa ya mwenyezi mungu na atakujalia kwa maana yeye si mchoyo.
Na haya majina ndio wanatokea humu manabii wa uongo,wafanya miujiza na wakemea mapepo wengi tu hutumia kwa kujua au bila kujua na pia waganga na wengineo wote ambao unaona wanafanya mambo ya kiroho msaada wake hutoka kwa malaika hawa ikiwa tu wanatumia majina haya au maana zake, yote hayo utayafanya kwa kujiweka karibu na mwenyezi mungu. Nakushauri ndugu yangu usitumie kwa kukufuru mwisho wake ni mbaya..

MAJINA SABA ALIYOFUNDISHWA MALAIKA IZRAIL (IZRAEL)

Huyu ni malaika maarufu sana kwa kutoa roho za viumbe vya mwenyezi mungu basi hatoi ila kwa kuruhusiwa na mwenyezi mungu mmoja na kwa hesabu maalum. na hatoi ila kaamrishwa na Allah

MAJINA YENYEWE NI:

**************************************


MAANA ZAKE:

Mimi ni muumba,Mimi ni mtengenezaji, Mimi ni wa asili,na mimi ndiye mwenye kufufua,ninafanya vile ninavyotaka, Mimi ninagawa maisha na ninagawa Kifo,Mimi ni mwenye nguvu na mtukufu,na mwenye kusamehe, ambaye peke yangu nihahurumia pia. Njoo Nje ewe roho, Nje na utii amri hii (kauli hii) aliyoamrisha Mwenyezi Mungu.

MAARIFA YAKE:

Ndugu yangu, ndugu yangu, heri upite katika maana hii kwa kumuhofia Mungu kabla ya kutamka kauli hii, ikiwa ni maana yake au majina yake. Ila kwa maarifa tambua ya kwamba
Mwenyezi Mungu akuongoze haya ndio majina ambayo yenye kuheshimiwa zaidi katika mbingu zote saba hakuna utakalo amrisha ila litatiiwa tu na kwa haraka sana maana hapo hakuna mjadala ni mwisho wa hesabu hakuna tena kuendelea au kurudi nyuma ni Kifo kwa aliyetaja/kilichotaja au Aliyetajiwa/kilichotajiwa papo hapo malaika wote hakuna anayeweza kupinga ikipita amri ya majina haya wala kuzuia.
Pia fahamu ya kwamba haya majina ni majina tishio na yenye maajabu makubwa, unapojikuta upo kwenye hukumu mji wa kigeni na umetekwa nyara au kufungwa bila hatia yani kwa kuonea ukayataja haya kwa roho ya kisasi basi kuanzia hakimu mashahidi na wote waliosikiliza kesi basi wote ni vifo au kukubwa na maafa yatakayo wafanya wasiweze hata kuuliza kesi hiyo au kuifuatilia na kila atakae taka kukufuatilia amekwenda na maji na kama kuna mtu unahitaji ajiue mwenyewe basi majina haya ni hatari zaidi wengi ambao huyatumia hovyo hufa vifo vibaya na vya ajabu na kudhalilika sana na pia ukitaka kugeuza kesi au hukumu ya kuzingiziwa na hakimu imrudie yeye na ahukumiwe yeye basi unaweza pia majina haya yanatumika kwa watu wenye jeuri wanaojiona miungu watu usitumie kwa mtu mnyonge utakufa dhalili sana usiyatumie unless upo kwenye mikono ya watu wanaojiona miungu watu au wafalme, pia hutumika kuuwa wafalme wa Kijini na Binadamu Wakuu wa Kijini na Kibinaadamu.

Matumizi ya salama na tahadhali:
Kupata kujua siri ya roho au chochote ndotoni,kufanya mambo bila kuonekana yasiyoonekana wala kusikika, kujua siri za roho za watu au wafu,kuwatumikisha wafalme,kuwa na kinga ya kifo(anaekukusudia baya anakufa) na kuwaka moto ukitembea usiku wa manane kwa maadui.

Hapo ndipo nimemaliza thread hii ambayo sijapenda kuelezea mambo mengine mengi kama:
kila mbingu na majina yake na malaika wake na kazi zao na wanavyoweza kukusaidia,kila sayari na malaika wake na majini na mashetani wake na wanachoweza kukufanyia, wakuu kuna mengi ya kujifunza ila nikijaaliwa kweye thread zingine



Kwa wale watakao ifuatilia thread hii hadi mwisho nitaachia baadhi ya majina kidogo kama mfano kwa manufaa ya wengine:

SAWA NARUDI KWENYE AHADI:
Baadhi ya majina niliyoyaficha hapo yanayojulikana ni:
1: HAYYU AL QAYUUM
2: ELOIM
3: ARADUNA
4:YAHWEH
5:QUDUS
6:AHAYA SHARA HAYA ADUWNAY ASWABAWUTI EL SHADAI/EHIEH ASHER EHIEH ADONAI TZABAOTH EL SHADDAI

Hapo kuna mawili ya kiislamu mawili ya kikristo na mawili ya waislamu na wakristo na pia yote hutumika pote kasoro matamshi tu
Hilo la sita tu ndio nawapa kidogo kazi yake chochote unachoomba utapata kiwe kinakuhusu wewe kama jibu la swali pa kupata rizqi ufanye nini n.k maombi yoyote ya kheri au shari pia hili ni moja kati ya majina aliyojibiwa Mussa alipomuuliza mwenyezi Mungu ni nani akamjibu

''AHAYA SHARA HAYA ADUWNAY ASWABAWUTI EL SHADAI/EHIEH ASHER EHIEH ADONAI TZABAOTH EL SHADDAI''
maana yake "MIMI NI MIMI" kwa wakristo na kwa waislam "MIMI NI MMOJA" ndivyo tunavyofasiliwa kwenye dini hizi mbili
Karibu kushare unayoyajua kuhusu MAJINA YA MWENYEZI MUNGU

Chagua moja kati ya majina hayo niliyoyatoa hapo nikuelezee maana na kazi yake, kwa watu wachache tu, kwa faida ya wote idadi ya jina moja ikifika watu 15 natoa.


Kwa haya na mengineyo:
Tembelea:

Rakims
Hii imenigusa sanaaaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom