Faida za kujiweka wazi (disclosure) ukiwa umeathirika na virusi vyaUKIMWI

My sister WoS, kwanza nikushukuru sana kwa mada nzuri. Mawazo yangu ni kwamba tatizo kubwa kwa UKIMWI Tanzania ni ELIMU. Najua wengi watapinga kua mbona kuna NGOs nyingi zinatoa ushauri na elimu ya afya na UKIMWI. Ukweli ni kua wote tuliosoma thread hii tutakubali kuna mambo mapya tumejifunza kutoka kwa WoS na wachangiaji wengine. Sasa jiulize kama wewe/sisi tunaoweza kupata hizi taarifa kwa intaneti (elites) tumepata elimu mpya kutokana na thread hii, vipi walioko vijijini au wasio na uwezo wa kupata hizi taarifa? Vipi kuhusu watanzania wengi ambao hata magazeti hawanunui wala redio hawasikilizi? Ukweli ni kwamba wengi wanakufa/kuathirika na UKIMWI kwa sababu moja tu...WANADHANI WANAJUA SANA KUMBE HAWAJUI..... mnasemaje kuhusu hili?
 
265027v1_jpg_92007b.jpg

Posted Apr 15, 09 5:35 AM CDT in Science & Health, Crime & Courts, World | Share Newser
(Newser Summary) – A singer in Germany's biggest girl band has been arrested on suspicion of having unprotected sex while aware she was HIV-positive, the BBC reports. Prosecutors suspect that No Angels singer Nadja Benaissa had unsafe sex with three men after she knew she was infected, at least one of whom now has the virus. She may be charged with inflicting grievous bodily harm.

Kwakweli ni ngumu sana kuwaambia watu uko HIV+, katika kesi hii, hata hao walioambukizwa, walikaa kimya miaka mingi bila kujitokeza, sababu ukimpeleka mtu kwenye vyombo vya sheria, lazima baadhi ya watu wajue kama umeadhirika. Kutokana na haya madawa ya kuongeza maisha , watu wanakuwa + miaka mingi sana , mi nafikiri mpaka wanazoea hali yao( kama huyu msichana alijua alipokuwa 15/16) msichana mdogo anaenda out , anakutana na wanaumme, jamani kuna mwanamme atabaki akimwambia ni +? Kwahio apate + mwenzake (kama kila mtu anaficha ngumu kupata) au awe hana sexual life. Mambo ya fifanyio mara nyingi ni mwanzoni tuu, baadae watu wanazoeana, hawatumii tena.
Zamani nilikuwa sielewi kabisa watu wanaambukizaje wenzao jamani, lkn toka huu mkasa , najaribu kidogo kuelewa. Unyanyasaji wetu ndio utakao tuuwa, maana watu wanaogopa kutuambia ukweli.
 
265027v1_jpg_92007b.jpg

Posted Apr 15, 09 5:35 AM CDT in Science & Health, Crime & Courts, World | Share Newser
(Newser Summary) – A singer in Germany's biggest girl band has been arrested on suspicion of having unprotected sex while aware she was HIV-positive, the BBC reports. Prosecutors suspect that No Angels singer Nadja Benaissa had unsafe sex with three men after she knew she was infected, at least one of whom now has the virus. She may be charged with inflicting grievous bodily harm.

Mambo ya fifanyio mara nyingi ni mwanzoni tuu, baadae watu wanazoeana, hawatumii tena.
Zamani nilikuwa sielewi kabisa watu wanaambukizaje wenzao jamani, lkn toka huu mkasa , najaribu kidogo kuelewa. Unyanyasaji wetu ndio utakao tuuwa, maana watu wanaogopa kutuambia ukweli.

Ni vema tukaambizana... inakuwaje watu waanze kufanya na kinga kisha baada ya muda waache? wanapima na kipimo gani kama hawaendi for VCT?
 
Ndugu yangu..mimi kama watu wengine wenye kupenda kujua mambo mengi hasa yale mtambuka( cross-cutting) na kuyazamia ili kuwa na uelewa mpana/mzuri, najisikia kudaiwa kama sita share ninachokijua na wengine.Ni kwa msingi huu tu.

Nakushukuru na wewe kwa kukazia point za maana sana kwenye hii ishu.

Pia nafikiri kila mtu anayo status yake kuhusu UKIMWI - ila wengi wanaogopa kujua.Uzuri wa kujua ni kujilinda kama status yako ni negative na kuishi positively kama wewe uko positive.Kwa wale walio negative wako mashakani zaidi kuliko hata wale wanaojijua wameathirika.Wasiojua status zao hao ni hatari zaidi kwao wenyewe na hata kwa watu wengine.
Pia nakushukuru kwa hilo la unapojua kitu na kuwaelisha wengine nao wajue, unasaidia na amini usiamini unaongeza hazina yako kwa mujibu wa "law of the Karma" Keep it up.
 
Halafu there is talk kwamba Bill Gates amepewa patent ya dawa ya kutibu ukimwi lakini anaificha,he doe not want to make it public,hataki watu wapone ukimwi.Nimeiona hii patent katika internet.

patent unaifichaje? mtu anapopewa patent ya uvumbuzi fulani ujue kwamba taarifa zote kuhusu huo uvumbuzi zinakuwa public. patent inakuruhusu kuzuia kisheria mtu/watu wengine kutumia uvumbuzi unaolindwa na patent bila ruhusa ya mwenye patent husika. kwa manziki hiyo bill gates hawezi ficha patent ya dawa ya ukimwi. aidha, kuna kitu kinaitwa compulsory license ambapo mwenye patent analazimika kuwapa license ya kutumia uvumbuzi wake wakati wa janga. brazil wameitumia hii kutengeneza dawa za kurefusha maisha kwa wagonjwa wa ukimwi.
 
imani kwamba mwenye kuathirika ni mzinzi/muasherati n.k. ndio kwa kiasi kikubwa inafanya watu wasijitangaze wajuapo wameathirika. ni vyema ifike mahali jamii imkubali muathirika bila kumhukumu kwamba ni mzinzi n,k. naamini hii itasaidia kuwafanya waathirika wajitokeze.
 
Ni vema tukaambizana... inakuwaje watu waanze kufanya na kinga kisha baada ya muda waache? wanapima na kipimo gani kama hawaendi for VCT?

Wanadai ni bora wenzio wasijue wakijua utanyanyapaliwa utatengewa mpaka vyombo vya kulia chakula nimeona ndugu yangu wanavyo mnyanyapaa. Kisa aliwaambia victim.
 
Wanadai ni bora wenzio wasijue wakijua utanyanyapaliwa utatengewa mpaka vyombo vya kulia chakula nimeona ndugu yangu wanavyo mnyanyapaa. Kisa aliwaambia victim.

Fidel, itabidi tuanzishe darasa au kipindi ili kuelewesha umma kuhusu unyanyapaa na mchango wake katika kufifisha vita dhidi ya ukimwi!!! new infections are higher in areas with high stigma and discrimination

MTM
 
Back
Top Bottom