WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
Wana JF,
Kuwa na VVU/UKIMWI ni kitu kinachoogopesha sana.Watu wengi huogopa kupima kwa sababu hawataki kujua hali zao kama wako positive au la.Mtu anakuwa na hofu sana endapo atapima agundulike ndio ivo tena kaathirika.
Tukumbuke kuwa kwa miaka ya sasa, status ya kuwa positive haikatishi tamaa kama miaka ya nyuma wakati hatujafahamu zaidi kuhusu ugonjwa wa UKIMWI au kuwa na maambukizi ya VVU/HIV.Sasa hivi kuna matumaini ya kuishi zaidi na hata miaka mingi endapo tu mtu utajua hali yake MAPEMA.
Kuwa na HIV haimaanishai kuwa na UKIMWI.....wataalamu wanashauri kuwa ni vema watu kupima na kujua hali zao ili kama ni negative ujue namna ya kujilinda na maambukizi.Ukiwa positive pia siyo mwisho wa dunia..utapata ushauri nasaha wa kukufanya uishi kwa matumaini......utakuwa umepata faida zaidi hasa kama utapima kabla Virusi havijafanya mashambulizi ya kukudhoofisha hadi ukaingia kwenye stage ya UKIMWI (AIDS).
Ukishajua status yako kuwa ni positive, inashauriwa ufikirie kujulisha wengine kwa hatua - ndugu wa karibu, mwajiri wako, mume/mke n.k. Ila uwe mwangalifu kwa kujiandaa na matokeo ya disclosure.Disclosure yenyewe ni kama tiba...ni ajabu! Watu ambao wamepitia hali hii wanatoa ushuhuda huu ambao kama hujaona na kuwasikiliza ukaona faida walizozipata unaweza kufikiria ni porojo tu.
JF mnaonaje hii?
Kuwa na VVU/UKIMWI ni kitu kinachoogopesha sana.Watu wengi huogopa kupima kwa sababu hawataki kujua hali zao kama wako positive au la.Mtu anakuwa na hofu sana endapo atapima agundulike ndio ivo tena kaathirika.
Tukumbuke kuwa kwa miaka ya sasa, status ya kuwa positive haikatishi tamaa kama miaka ya nyuma wakati hatujafahamu zaidi kuhusu ugonjwa wa UKIMWI au kuwa na maambukizi ya VVU/HIV.Sasa hivi kuna matumaini ya kuishi zaidi na hata miaka mingi endapo tu mtu utajua hali yake MAPEMA.
Kuwa na HIV haimaanishai kuwa na UKIMWI.....wataalamu wanashauri kuwa ni vema watu kupima na kujua hali zao ili kama ni negative ujue namna ya kujilinda na maambukizi.Ukiwa positive pia siyo mwisho wa dunia..utapata ushauri nasaha wa kukufanya uishi kwa matumaini......utakuwa umepata faida zaidi hasa kama utapima kabla Virusi havijafanya mashambulizi ya kukudhoofisha hadi ukaingia kwenye stage ya UKIMWI (AIDS).
Ukishajua status yako kuwa ni positive, inashauriwa ufikirie kujulisha wengine kwa hatua - ndugu wa karibu, mwajiri wako, mume/mke n.k. Ila uwe mwangalifu kwa kujiandaa na matokeo ya disclosure.Disclosure yenyewe ni kama tiba...ni ajabu! Watu ambao wamepitia hali hii wanatoa ushuhuda huu ambao kama hujaona na kuwasikiliza ukaona faida walizozipata unaweza kufikiria ni porojo tu.
JF mnaonaje hii?