Faida ya Mwanga wa jua katika mwili wa binadamu

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,316
33,112
Mwanga wa jua unasaidia kuimarisha kinga ya mwili





Huku kwa muda mrefu ikiwa inaaminiwa kwamba Vitamini D inayotokana na mwanga wa jua inaimarisha mifupa, uchunguzi mpya umeonyesha kwamba mwanga wa jua pia una umuhimu mkubwa katika kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili na uwezo wake wa kukabiliana na magonjwa.

Uchunguzi huo umeeleza kwamba, seli zinazoshambulia maradhi za mfumo wa kinga ya mwili ambazo hujulikana pia kama 'T Seli" zinategemea sana Vitamin D ili kuzifanya zitekeleze kazi yake.

Carsten Geisler aliongoza uchuguzi huo amesema kuwa, wakati T seli zinapokutana na kidudu toka nje ya mwili, hufungua antena yake inayoitwa 'D receptor' ambayo inaitumia kwa ajili ya kusaka vitamin D. Wakati kunapokuwa hakuna vitamin hiyo

inayotokana na jua suala ambalo hutokea kwa watu zaidi ya nusu duniani, seli hizo hushindwa kufanya kazi na kushindwa kufahamu tishio linalosababishwa na vijidudu vinavyosababisha maradhi.

Wataalamu wana matumaini kwamba uchunguzi huo mpya utawezesha kuandaliwa mazingira ya kuwekwa mikakati mipya kwa ajili ya kupambana na magonjwa katika siku zijazo.
 
Back
Top Bottom