Faida ya Buzwagi ni hii: Serikali

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Hapendwi mtu bila kuifanyia mikataba yote ya madini marekebisho au kuiandika upya mikataba hiyo.

Serikali sasa yaweka wazi faida ya Buzwagi
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Tuesday,October 02, 2007 @00:02

SERIKALI imesema mkataba wa Buzwagi umeboreshwa kwa masilahi ya taifa ikilinganisha na mikataba ya zamani ya madini, na kutaja faida za mradi huo wa uchimbaji dhahabu. Kutokana na hali hiyo, Serikali imesema tuhuma zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa wa upinzani kuwa katika kusaini mkataba wa Buzwagi, sheria na taratibu za nchi zilikiukwa, si za kweli na zina lengo la kuupotosha umma.

Taarifa ya Serikali iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema mkataba wa Buzwagi uliandaliwa Tanzania na wataalamu wa hapa nchini na ukapitia taratibu zote zinazopaswa kufuatwa, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa na Kamati ya Ushauri ya Madini. Serikali ilieleza kuwa wataalamu waliohusika katika mchakato wa majadiliano ya mkataba huo na Kamati ya Ushauri ya madini iliyoupitisha, wote ni wazalendo na wakati wote walihakikisha masilahi ya nchi yanawekwa mbele.

“Kulinganisha na mikataba mingine iliyotangulia, mkataba huo wa Buzwagi unavyo vipengele vilivyoboreshwa zaidi,” ilisema taarifa hiyo iliyotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo. Vipengele ambavyo vimetajwa na serikali kuwa vimeboreshwa ni kupungua kwa asilimia 80 kwa mwaka wa kwanza na asilimia 50 miaka inayofuata; Kodi za zuio kwa kazi za kitaalamu kuongezeka kutoka asilimia tatu hadi kufikia asilimia tano.

Eneo jingine ni kodi za zuio kwa gharama za utawala kuongezeka kutoka asilimia tatu hadi asilimia 15; Masharti ya kununua bidhaa na huduma mbalimbali nchini; na kuchangia mfuko wa uwezeshaji dola za Marekani 125,000 kwa mwaka.

Serikali pia imesema ujenzi wa mgodi utakapokamilika na uzalishaji kuanza rasmi inatarajiwa kwamba miaka 10 ya kwanza ya uendeshaji wa mradi huo utakuwa na faida nyingi, ikiwamo mrahaba na kodi nyingine zinatarajiwa kufikia dola za Marekani milioni 198.8. Faida nyingine zilizotajwa na serikali ni ajira kwa Watanzania 696 wa fani mbalimbali; kodi zinazotokana na mishahara ya wafanyakazi (PAYE) dola za Marekani milioni 50.3 na ujenzi wa laini ya umeme utakaogharimu dola za Marekani milioni 30.

“Laini hii itawezesha upatikanaji wa nishati ya umeme ambayo ni pamoja na maeneo ya mji wa Kahama, vijiji vya Mwine, Chapulwa, Mwendakulima, Sangiwa,” ilisema taarifa hiyo na kutaja faida nyingine kuwa ni ujenzi wa miundombinu ya uchumi na jamii kama vile shule na zahanati katika maeneo yanayozunguka mgodi.

“Hivi karibuni pamejitokeza baadhi ya wanasiasa hususan kutoka vyama vya upinzani kutoa matamshi hadharani, kuwatuhumu viongozi kadhaa wa umma walioko madarakani sasa au awamu zilizopita kuwa walikiuka taratibu au kuvunja sheria kwa kusaini mikataba ya madini,” ilisema taarifa hiyo. Serikali ilisema viongozi hao wamejaribu kupotosha umma juu ya tafsiri sahihi za sheria inayoongoza mikataba hii.

Vile vile kuna jitihada za makusudi za kuuhadaa umma kwamba kusainiwa mkataba wa Buzwagi kulikiuka taratibu na sheria za nchi, ilisema taarifa hiyo. Katika kuwaelimisha wananchi, serikali imeelezea mchakato wa mkataba huo kwa kueleza kuwa mikataba ya uendelezaji wa madini ya mwaka 1998 inampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya madini kuingia makubaliano na mmiliki au muombaji wa leseni kubwa ya uchimbaji madini.

Taarifa ilisema kwa mujibu wa kifungu hicho, Waziri hutakiwa kupata ushauri wa Kamati ya Ushauri ya Madini kabla ya kusaini mkataba. Kampuni tanzu ya Barrick iitwayo Pangea Minerals ilipatiwa leseni ya utafutaji wa madini katika eneo la Buzwagi wilayani Kahama, Shinyanga kuanzia mwaka 2003.

Baada ya utafiti wa miaka takriban mitatu, kampuni ya Pangea Minerals iliwasilisha maombi yake serikalini ili kuingia mkataba wa uendelezaji wa mradi wa uchimbaji wa madini katika eneo hilo. Maombi hayo yaliambatanishwa na upembuzi yakinifu wa mradi huo. Timu ya wataalamu wa serikali ilianza majadiliano na kampuni ya Pangea Minerals kuanzia Mei mwaka jana kwa nia ya kuingia katika mkataba. Kufikia Februari 16 mwaka huu, taratibu zote za kisheria kwa ajili ya kusaini mkataba huo zilikuwa zimekwisha kukamilika na hatimaye mkataba huo kutiwa saini Februari 17 mwaka huu.

Katika hatua nyingine, malumbano juu ya suala la ufisadi na rushwa yanaweza yakafikia kiwango cha kuleta mafarakano na uhasama katika jamii yakizidi kiasi. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Jaji Mstaafu Mark Bomani alisema kutokana na malumbano ya ufisadi yanayotokea kwa sasa, vitendo vya rushwa na ufisadi ni lazima vipigwe vita kwa nguvu zote, lakini sheria za kutuwezesha kufanya hivyo na sababu za kufanya hivyo vipo, kinachotakiwa ni utashi wa kufanya jambo hilo.

Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved
 
Hawa watu hawaachi kunifanya niamini ni wajinga tuu..hivi nani anataka contribution kutoka kwa hao macapitalist? yaani as if wanatusaidia na hayo mambo ya line ya umeme kama faida kwetu ni upuuzi mtupu na sitaki kusikia huo ujinga wao wamekuja kwa deal la mining sio kutujengea umeme au sijui tutapata PAYE kwani nani halipi PAYE ile nchi,wanatuona mbumbumbu sana hawa ....tunachotaka ni vitu vitatu tuu tulipwe kutoka kwenye hii deal Royalty yetu na Corporate tax ya 30% and all local Taxes & levies....ukiangalia hapo hakuna corporate Tax ambayo ndio the most important of all na ndiyo itatuhakikishia fair deal lakini wapi bwana maana hawa ng'ombe account zao Swiss zimeshafanyiwa mambo
 
jamani kama ndio wataalam wetu ndio walio engineer hii contract ya Buzwagi na vipengere kama contribution za 125,000 kila mwaka,PAYE,masharti ya kununua bidhaa local wakati tunajua hata breakfast yao itakuwa ikitoka South Africa na kutuambia line ya umeme watakaojenga ni part ya contract huku tukijua expense kama hizo zina deductions zake na technically itakuwa ni pesa yetu mana hizo deductions ni ua mtu,jamani inasikitisha sana tunadanganywa na vipesa vidogo huku jama wakijichotea billions...angalieni Geita hakuan lolote ukitoka nje ya mgodi mile moja tuu ni umaskini wa kutupa...hawa jamaa hawalipi local Tax na ningekuwa mbunge lazima wangezitoa tuu na ningeenda mahakamani maana biashara yeyote lazima ilipe local Tax
 
"SERIKALI imesema mkataba wa Buzwagi umeboreshwa kwa masilahi ya taifa ikilinganisha na mikataba ya zamani ya madini."

Tunaomba kuiona hiyo "mikataba ya zamani ya madini" ili na sisi tuilinganishe na huu wa Buzwagi na kuona ukweli umelalia wapi.
 
Sasa kama huu wa Buzwagi umeboreshwa na tunauona ni utombo, sasa ile ya mwanzo sijui itakuwaje.
Pili wanataka kusema ya mwanzo hakutengenezwa na wataalamu wetu wenyewe.
Basi kweli kazi ipo
 
Hawa wajinga sehemu amabyo wamejinasa ni kuhusu suala zima la kusainiwa kwa huo mkataba. Si walisema kwamba usainishwaji wa misaada umesimamishwa ili kutoa nafasi kwa wataalamu uchwara wa serikali wafanye review ya mikataba ya zamani? Sasa iweje waende kusaini mkataba MPYA, tena ndani ya chumba cha GUEST HOUSE au HOTELI?
 
Watanzania kweli tumekuwa wagumu, wenzenu wanajitahidi kueleza weeeeee.. watu bado mnabisha, mnataka wafanye nini?
 
tena kwenye maelezo yao wanalinganisha mkataba wa Buzwagi na mikataba ambayo hatujaiona. hapo hapo hawajakataa kwamba mkataba uliovuja sio wa kweli. Na vile vile hawataki kutuonyesha hiyo mikataba mingine ili na sisi tuweze kuilinganisha na huu mzuri kabisa wa Buzwagi. Serikali poa sana hii. Hawajawahi kufanya kosa hata siku moja. wala rushwa hawachukui kamwe. Wanafanya kazi kwa maslahi yetu na sio yao binafsi. Safi sana MMKKJ
 
Hapa patamu sasa.Walete hiyo mikataba mingine ili sisi watanzania kama "mashareholders" tulinganishe na huo Buzwagi ili tujue kama kweli umeboreshwa kuliko hiyo mingine.
Sasa ndio imethibitika kuwa kuna tatizo kubwa kwenye hiyo mikataba. Kwa sababu tangu Zito alipoibuwa hii hoja bungeni serikali imechanganyikiwa kabisa kila mmoja ndani ya ccm na serikali yake anazungumza lugha yake kama yaliyowakuta walikuwa wanajenga mnara wa babeli!
 
Chizi siku zote huwa anatembea na vyeti vyake vya shule, hiyo yote ni ktk kuthibitisha kuwa yeye sio chizi. Kitendo cha Serikali kutuelezea kuwa mkataba wa Buzwagi una faida kuliko mikataba mingine ambayo hatuijui hata ina nini ndani, haina tofauti sana na chizi ambaye anataka kututhibitishia yeye sio chizi.
 
naam,mambo yanazidi kuwa mambo,hapo hapo Cabinet itazunguka nchi nzima "kufafanua" swala hili na kuelezea "mafanikio" ya serikali ya awamu ya nne,jamani tujue kuwa tatizo hili ni kubwa kuliko tunavyofikiri,sasa kama wao wanaamini ni kwa faida yetu kwa nini hwakumkubalia Zitto kabwe iundwe kamati ya Bunge?Hii gharama ya kuzunguka nchi nzima nani anailipia?Je hiyo mikataba ya zamani mbona hatujaiona?tutalinganishaje ubora wa Buzwagi na vitu ambavyo hatujaviona?Kama Buzwagi ni bora sana sitamani hata kuiona hiyo ya zamani...Mungu Ibariki Tanzania!!!
 
Ibambasi,
Ukishangaa ya Musa mazingaombwe na mauzauza ya Bulyankulu, Tulawaka, IPTL, RICHMOND na Chopper za jeshi, yatakufanya ukane uraia wa Udanganyika.
 
Ibambasi,
Ukishangaa ya Musa mazingaombwe na mauzauza ya Bulyankulu, Tulawaka, IPTL, RICHMOND na Chopper za jeshi, yatakufanya ukane uraia wa Udanganyika.

Ndugu yangu Machifula siwezi kuukana uraia wa tanzania, kwani hata baba yako akiwa mlevi,mzinzi,mwizi sugu na mfanya maovu yote bado tu hutaweza kumkana,cha muhimu ni kufight kuhakikisha hiyo bad legacy atakayoiacha unaisafisha kwa kazi zako nzuri,kwa maana hiyo basi kuukana utanzania sio solution,cha muhimu ni kuhakikisha kuwa tunapambna mpaka mwisho na hawa mafisadi,vipi kama Zitto na Slaa wangeukana utanzania moto huu wa mabadiliko mapya na mwanzo mpya unaoanza kuwaka tungekuwa tunaushuhudia?wapinzani wako 45 tu lakini unashuhudia mwenyewe wanavyoipelekesha CCM,nadhani kama ulisoma literature miaka ile utakuwa inakumbuka kitabu/play ya "AN ENEMY OF THE PEOPLE" kinachoongelea ugumu wa kuleta mabadiliko (Dr. Peter Stockmann kama sijakosea)...muhimu tukomae nao mpaka kieleweke...
 
jamani hiyo mikataba mingine fumbeni macho wala msitamani kuiona kwani mtakufa kabla ya siku uliyopangiwa na muumba wako.kwa hiyo chonde chonde nowaombeni tuachane nayo hiyo.
 
Katibu Tarafa heshima mkuu wa kitongoji,
Usemayo ni sahihi.Hizi kashfa zitatufupishia maisha yetu lakini wacha tuzione tu.
Kama mkataba wa Buzwagi ulipitiwa na jopo la wataalamu wote hao tena "eti wazalendo". Ilikuwaje Karamagi akaamua kufuta kifungu cha mkataba pale hotelini tena dakika za mwisho?

NanukuuTaarifa ya Serikali iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema mkataba wa Buzwagi uliandaliwa Tanzania na wataalamu wa hapa nchini na ukapitia taratibu zote zinazopaswa kufuatwa, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa na Kamati ya Ushauri ya Madini. Serikali ilieleza kuwa wataalamu waliohusika katika mchakato wa majadiliano ya mkataba huo na Kamati ya Ushauri ya madini iliyoupitisha, wote ni wazalendo na wakati wote walihakikisha masilahi ya nchi yanawekwa mbele".

Kwa maana ingine ni kuwa mikataba iliyotangulia,haikuandaliwa na wataalam na watu wasio wazalendo(Wenye nia ya kuiba),ambao walihakikisha maslahi ya nchi hayana kipaumbele!!

255Texter
Kauli mbiu yako ni bomba sana,naomba kuiendeleza.

NDUGU MTANZANIA.......PAMBANA NA RUSHWA, PAMBANA NA UFISADI, PAMBANA NA CCM!
 
jamani hiyo mikataba mingine fumbeni macho wala msitamani kuiona kwani mtakufa kabla ya siku uliyopangiwa na muumba wako.kwa hiyo chonde chonde nowaombeni tuachane nayo hiyo.

IPTL? Au mingine ipi? Tatizo nadhani ni ukubwa wa documents za mikataba yenyewe huwatia uzembe wadau kuisoma kipengele kwa kipengele na wanabakia kupigwa 'changa la macho' wanadondosha wino kulimalizia taifa!
 
IPTL? Tatizo nadhani ni ukubwa wa documents za mikataba yenyewe huwatia uzembe wadau kuisoma kipengele kwa kipengele na wanabakia kupigwa 'changa la macho' wanadondosha wino kulimalizia taifa!

Mkuu nadhani ukubwa wa doc. haupashwi kuwa tatizo kwani hao wanao takiwa kuisoma na kuangusha wino hicho ndo kibarua chao, wanatafuna kodi zetu kwa ajili ya kazi hiyo!!

Kwahiyo kushindwa kuisoma ni uzembe wa hali ya juu ambao haupaswi kuvumilika katika hali yoyote ile!

Binafsi nashawishika kwamba maamzi ya kisiasa zaidi ya utaalamu, plus ten percent ndiyo tatizo kubwa hapa!

na hatuwezi kuacha hali hii iendelee kulimaliza Taifa letu, tukizidi jawa woga wa kunguru, Haturudi nyuma sasa.. lazima kieleweke!!
 
IPTL? Au mingine ipi? Tatizo nadhani ni ukubwa wa documents za mikataba yenyewe huwatia uzembe wadau kuisoma kipengele kwa kipengele na wanabakia kupigwa 'changa la macho' wanadondosha wino kulimalizia taifa!


Ndio maana ya urais ati! Time is up and the buck stops with JK. Aamue kusuka au kunyoa.
 
Kwahi huo mkataba anasoma mtu mmoja si wanasoma wengi kila mmoja mwenye utaalamu fulani katika fani husika ? kwahiyo kama watashirikishwa wataalamu wengi kila mmoja asome kipengele chake kinachomhusu katika mkataba husika hakuna cha Uzembe

MFANO MKATABA WA BUZWAGI

1) WATAALAMU WA MAZINGIRA WASOME

2) MKUU WA WILAYA ,KATA AU MTAA

3 ) WANASHERIA

4 ) TAASISI ZA USALAMA

5 ) WATU WANAOHUSIKA NA USAFIRISHAJI

6 ) MAMLAKA ZA KODI

NA WENGINE WENGI ZAIDI KILA MMOJA ASOME KIPENGELE CHAKE NA KUKUBALIANA , MIKATABA HII INAKUWA SIO WAZI KWA SABABU UNAWEZA KUKUTA MAMLAKA ZA KODI HAZINA MUWAKILISHI HAPO WAU WATU WA MAZINGIRA NI WANASIASA PEKE YAO AMBAO HAWAJUI MAMBO YA MAZINGIRA NA KODI AU USALAMA
 
shy,
kwa bongo mambo ni tofauti hiyo kazi alipewa mtu mmoja tu na waziri ya kunakili huo mkataba,hapo hakuna cha wanasheria wala wataalamu wa madini wa kiumbe kingine.ndio maana kuna madudu kama hayo hao wengie hata kopi hawana ndio maana imekuwa kazi hata kujibu hizo tuhuma zenyewe kwa sababu wahusika hawakuhusishwa kwenye mchakato mzima.
Tanzania mambo yanafanyika kama watu hawaja kwenda shule,ndio maana wao kila kitu ni siri.kama kweli ni mimi au wewe ndio ungekuwa umeandika huo mkataba nafikiri leo hii ungekwisha sahaulika nandio ungekuwa mbuzi wa shughuli.kinyume chake wanamtafuta haliye ulikisha huo mkataba na siye aliyeandika hayo madudu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom