Faida na Hasara za Maamuzi ya Zimamoto: Tuletewe Mrejesho Isije Kuwa Tunatwanga Maji Kwenye Kinu!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,571
Wanabodi
Preamble: Naunga mkono juhudi zote zinazofanywa na rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli katika kubana matumizi yasiyo ya lazima na badala yake fedha hizo zitumike kuleta maendeleo.

Baadhi ya maamuzi haya ni maamuzi ya zimamoto ambayo yamefanyika ghafla kama uamuzi wa kufuta mialiko ya kuhudhuria tukio la kuzimwa Mwenge wa Uhuru.

Uamuzi huo umefanyika ghafla as if tukio la kuzimwa Mwenge. Wa Uhuru ni tukio la ghafla na limekuja bila taarifa kama lile tetemeko la ardhi Bukoba!, tukio hili lilikuwepo, limepangwa kwa mwaka mzima, mwenge umezungushwa nchi nzima, protocol ya kilele cha sherehe hizo inajulikana mwaka mzima, bajeti ilipangwa, ikapitishwa, madokezo yakaandikwa, fedha zikaidhinishwa, barua za mialiko zikatolewa, fedha zikalipwa, safari zikapangwa, then ghafla at an eleventh hour ndipo inakuja taarifa ya Ikulu kuifuta mialiko hiyo na waliochukua fedha kurudisha! . What a disturbance and inconveniences? . Kulikuwa na udharura gani kuuzuia mialiko hiyo mapema at the planing stage na kuja kuahirisha kwa mtindo wa zimamoto at the last minute?!.

Kuna kitu kinaitwa "A legitimate expectations", mtu akiishajiandaa kwa safari, na unachukua malipo, unakuwa umeishajiondoa nyumbani na kujipanga kisafari safari, tena wengine hata kupanga utalala wapi na bulangeti la aina gani!, wengine husafiri na ndoo, wengine vidumu na wengine watajua mbele kwa mbele alimradi ni safari halali ya kikazi.

Safari kama hiyo inaweza tuu kuahirishwa kama kumetokea jambo ambalo halikutarajiwa "force majeure", lakini safari inapoahirishwa kwa uamuzi tuu wa utashi wa kiongozi bila kutumia sheria yoyote wala kanuni yoyote, then a legitimate expectations zinawataka watumishi waliokwisha lipwa fedha, kurudishwa zile fedha tuu ambazo hazijatumika ambazo ni fedha za maduhuli (imprest) lakini hawapaswi kurudisha zile fedha za masurufu (allowances), hizo ni halali yao kisheria.

Kitu kingine muhimu kupitia sheria mpya ya the right to information, wananchi tunapaswa kuelezwa maamuzi haya ya Zimamoto yameleta tija gani, kiasi gani kimeokolewa na fedha hizo zimefanyia maendeleo gani isije kuwa watu Tunatwanga Maji Kwenye Kinu, kisha tunapongezana kwa uamuzi wa busara.

Lilipoundwa Baraza ndogo la Mawaziri huku makatibu wakuu wakiongezeka, kuna watu tulisema humu tumeongeza gharama za uendeshaji wa serikali badala ya kupunguza, hata baada ya kupungua wafanyakazi hewa na kutoajiri wafanyakazi wapya, wage bill ya serikali bado unazidi kuongezeka badala ya kupungua, ili usije kuwa ni kutwanga maji kwenye Kinu, wananchi tuambiwe kupunguza ukubwa wa serikali tume save kiasi gani, safari za nje tumeokoa kiasi gani,kufuta sherehe za uhuru tumeokoa kiasi gani, na hizi fedha zote zililookolewa ndio zimepelekwa kwenye huduma za jamii kama afya, elimu etc, ili Watanzania tuone tija ya kubana matumizi na sio kubana matumizi huku tukitwanga maji kwenye Kinu.

Wakati tukiendelea kumpongeza rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa maamuzi yake yenye tija kwa taifa letu, tuendelee kumsisitizia kuwa taifa hili linahitaji zaidi kujengwa kwa mifumo imara ya iutendaji, usimamizi, utekelezaji, na tathimini ili kupata mresho hivyo kufanya uwajibikaji na matumizi mazuri ya fedha za umma kwa shughuli zote zisizo na manufaa kwa taifa zikiwemo Mbio za Mwenge, na sherehe nyingine mbalimbali zisizo na tija na maslahi kwa taifa letu zifutwe rasmi kwa waraka na sio kutegemea utashi tuu wa rais. Hili la rais kutoa maagizo kwa waraka, nilishauri hapa
AG, Mshauri Mh.Rais Atoe Maagizo kwa Presidential Decrees Kuyapa Nguvu ya Kisheria

Suala la nini kina manufaa kwa taifa na nini hakina manufaa kitajulikana kwa kupokea mrejesho na you never know taifa letu linaweza kufikia hatua, kwenye kila mpango, kila wizara, kila idara, kila taasisi, kila mradi kila mpango wa maendeleo, tujenge mfumo wa SMART OBJECTIVES, wenye malango mahsusi na mwisho wa siku tunaletewa mrejesho

Mfano tukifanya tathmini ya majukumu ya post za Wakuu wa Wilaya, tutagundua hizi ni post za colonial legacy tuu, yaani post za kikoloni tuu na hazina maana yoyote ukilinganisha na the expenditure na work done kwa sababu Wakurugenzi wa Halmashauri wanatosha sana tuu hivyo gharama za Wakuu Wa Wilaya nazo ni ufisadi tuu, post hizi zikifutwa zitalisaidia sana taifa letu.

Tumefanya miradi mingi, Mkukuta, Mkurabita, Mkuza, Mkumbita, Uhaulishaji fedha, Kilimo Kwanza, etc ambayo huianza kwa mbwembwe sana, lakini hatupewi mrejesho.

JK alikuja na drive ya uchumi wa gesi kuipeleka Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati, takapanga mipango mingi ya matumizi ya gesi, hadi kwenye magari, viwandani hadi majumbani, gesi ndio iwe the main source of power kwa kufikishwa hadi Bagamoyo kwenye ile industrial park na bandari ya Bagamoyo. Magu kaingia, kaja na drive yake ya Tanzania ya viwanda, SGR, ndege, na the source of power sasa sio gesi tena bali ni hydropower, badala ya kuendeleza miradi ya gesi, sasa tunaanza mradi wa Stigler Gorge!, Bandari ya Bagomoyo imesimamishwa!.

JK akaanzisha mchakato wa Katiba mpya, tukatumia mabilioni, Magu kaingia, kwake katiba sio kipaumbele!. Nchi haiwezi kuendeshwa hivi na tukafika, lazima tujenga tabia ya kufanya tathmini na tuletewe mrejesho.

Hongera sana rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchukua maamuzi magumu kulisaidia taifa letu lenye lindi la umasikini uliotopea uliogubikwa na rushwa na ufisadi, maamuzi haya hata yakiitwa ni ya udikiteta, then afadhali ya udikiteta ili taifa liponywe kama kilivyo kidonge kichungu cha dawa au sindano yenye maumivu ndio iponyeshayo lakini tusianzishe miradi kwa kukurupuka, tufanye kwanza upembuzi yakinifu na mwisho tuletewe tathmini.

Nawatakia maandimisho mema ya Nyerere Day hapo kesho.

Wa Salaam
Pasco
Rejea.
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ..
 
Nimewaambia dawa ni moja tu.....

Rais ajihudumie kwa mshahara wake awapo ikulu.....

Mshahara wa Rais ukatwe kodi....

Hivyo hivyo kwa wasadizi wake akiwemo Makamo wa Rais,Waziri mkuu,Na jaji mkuu.......

Tukifanya hivyo ndipo watu watajua uchungu wa kodi na dhana nzima ya kubana matumizi..............

Rais hawezi kupewa kila kitu ashindwe kulipa kodi na aendelee kuwatisha wasaidizi wake eti waludishe posho....

Eti nimeokoa pesa pesa zipi? Za kumlipa lipumba? Na wakati Ajira hakuna ,Dawa hakuna hospitali?
 
Nchi imekuwa ya ajabu sana hii..mtu mmoja ndo amekuwa ulimi wa kila kitu ..kila kitu ni kukurupuka na kutafuta sifa za kijinga..sherehe za kitaifa zinajulikana..alikuwa wapi kutoa mwongozo mapema..imebaki siku moja ndio anakuja na tamko kama sio sifa za kijinga ni nini..hela zilishafika wahasibu wakazigawa kwa wahusika..lei unasema rudishen wakati mtu ameshaanza kuzitumia..
By the way hiyo hela wanayookoa inaenda wapi mbona kila siku wanaokoa na kukusanya trilion kila mwezi halafu nchi ina uhaba wa madawa?!! ..hizo hela zinaenda wapi..au zinaenda kumalizia mahari?!..
Lazima kama taifa tuwe na utaratibu wa kufanya maamuzi...
 
Pasco
Zamani ilikuwa ukisikiliza mpira unatangazwa redioni mara nyingi ungesikia "Lunyamila na mpira, Lunyamila anakwenda, Lunyamila, Lunya, Lunya...." Dakika mbili nzima mpira anao mtu mmoja.
Siku hizi hata hao mastaa kina Messi husikii wakikimbia na mpira na wakipenda kutajwa wao tu...One touch pass the ball

Je huoni kwamba kuna mazingira ya mchezaji mmoja ndio anapenda jina lake tu litajwe na watangazaji [media] hata kama tupo zama za kucheza ki-Timu?
 
Kufuta safari za siku moja ili kuokoa fedha wakati mwenge umeshatafuna fedha kwa kuzunguka mwaka mzima ni wazimu!!

Bahati mbaya watanzania wengi ni maiti kifikra ndio maana hakuna anayehoji kupata mantiki!!
Kwa tuliokaa serikalini tunaelewa taratibu za fedha zilivyo maana mpaka kufikia juzi kuna watu wengi walikwishalipwa na wengine walishafika bariadi!!

Magufuli anatafuta sana attention but aelewe muda unasonga na 90% ya maamuzi yake huleta hasara zaidi kuliko faida!!

Nilidhani zile purukushani zake za uwaziri kaziacha kumbe wapi!!

Kwa hali hii ikiendelea nchi itarudi ground zero!!

Yetu Macho!
 
Nimewaambia dawa ni moja tu.....

Rais ajihudumie kwa mshahara wake awapo ikulu.....

Mshahara wa Rais ukatwe kodi....

Hivyo hivyo kwa wasadizi wake akiwemo Makamo wa Rais,Waziri mkuu,Na jaji mkuu.......

Tukifanya hivyo ndipo watu watajua uchungu wa kodi na dhana nzima ya kubana matumizi..............

Rais hawezi kupewa kila kitu ashindwe kulipa kodi na aendelee kuwatisha wasaidizi wake eti waludishe posho....

Eti nimeokoa pesa pesa zipi? Za kumlipa lipumba? Na wakati Ajira hakuna ,Dawa hakuna hospitali?
lakini mkuu,professor Lipumba ni mtu muhimu sana ,sioni ubaya akisaidiwa kwa hali na mali,mimi kwa hili niko pamoja na mheshimiwa,
 
Nimewaambia dawa ni moja tu.....

Rais ajihudumie kwa mshahara wake awapo ikulu.....

Mshahara wa Rais ukatwe kodi....

Hivyo hivyo kwa wasadizi wake akiwemo Makamo wa Rais,Waziri mkuu,Na jaji mkuu.......

Tukifanya hivyo ndipo watu watajua uchungu wa kodi na dhana nzima ya kubana matumizi..............

Rais hawezi kupewa kila kitu ashindwe kulipa kodi na aendelee kuwatisha wasaidizi wake eti waludishe posho....

Eti nimeokoa pesa pesa zipi? Za kumlipa lipumba? Na wakati Ajira hakuna ,Dawa hakuna hospitali?
lakini mkuu,professor Lipumba ni mtu muhimu sana ,sioni ubaya akisaidiwa kwa hali na mali,mimi kwa hili niko pamoja na mheshimiwa,
 
Nimewaambia dawa ni moja tu.....

Rais ajihudumie kwa mshahara wake awapo ikulu.....

Mshahara wa Rais ukatwe kodi....

Hivyo hivyo kwa wasadizi wake akiwemo Makamo wa Rais,Waziri mkuu,Na jaji mkuu.......

Tukifanya hivyo ndipo watu watajua uchungu wa kodi na dhana nzima ya kubana matumizi..............

Rais hawezi kupewa kila kitu ashindwe kulipa kodi na aendelee kuwatisha wasaidizi wake eti waludishe posho....

Eti nimeokoa pesa pesa zipi? Za kumlipa lipumba? Na wakati Ajira hakuna ,Dawa hakuna hospitali?

Ni nzuri sana,maana hata wastaafu watumie viinua mgongo vyao kulisha familia zao.Kwanza asilimia 99 ya hao wastaafu wetu wamekwapua mali za umma
 
Yaani hakuna total management, hakuna team work, hakuna team spirit tunachokiona ni mtu mmoja kutoa maelekezo na wengine kufuata, haingii akilini watu wamelipwa na wameishaanza kutumia hela kwa ajili ya maandalizi ya safari halafu ghafla mnaambiwa safari imefutwa rudisheni hela, this is not fair, halafu utashangaa uvccm wanaunga mkono makada wenzao kuaibishwa na kudhalilishwa.
 
Nchi imekuwa ya kipumbavu sana hii..mtu mmoja ndo amekuwa ulimi wa kila kitu ..kila kitu ni kukurupuka na kutafuta sifa za kijinga..sherehe za kitaifa zinajulikana..alikuwa wapi kutoa mwongozo mapema..imebaki siku moja ndio anakuja na tamko kama sio sifa za kijinga ni nini..hela zilishafika wahasibu wakazigawa kwa wahusika..lei unasema rudishen wakati mtu ameshaanza kuzitumia..
By the way hiyo hela wanayookoa inaenda wapi mbona kila siku wanaokoa na kukusanya trilion kila mwezi halafu nchi ina uhaba wa madawa?!! ..hizo hela zinaenda wapi..au zinaenda kumalizia mahari?!..
Lazima kama taifa tuwe na utaratibu wa kufanya maamuzi...
tumenunua ndege kwa pesa taslimu,
tumeanza ujenzi reli ya kati,
elimu bure,
etc etc
 
Wanabodi
Preamble: Naunga mkono juhudi zote zinazofanywa na rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli katika kubana matumizi yasiyo ya lazima na badala yake fedha hizo zitumike kuleta maendeleo.

Baadhi ya maamuzi haya ni maamuzi ya zimamoto ambayo yamefanyika ghafla kama uamuzi wa kufuta mialiko ya kuhudhuria tukio la kuzimwa Mwenge wa Uhuru.

Uamuzi huo umefanyika ghafla as if tukio la kuzimwa Mwenge. Wa Uhuru ni tukio la ghafla na limekuja bila taarifa kama lile tetemeko la ardhi Bukoba!, tukio hili lilikuwepo, limepangwa kwa mwaka mzima, mwenge umezungushwa nchi nzima, protocol ya kilele cha sherehe hizo inajulikana mwaka mzima, bajeti ilipangwa, ikapitishwa, madokezo yakaandikwa, fedha zikaidhinishwa, barua za mialiko zikatolewa, fedha zikalipwa, safari zikapangwa, then ghafla at an eleventh hour ndipo inakuja taarifa ya Ikulu kuifuta mialiko hiyo na waliochukua fedha kurudisha! . What a disturbance and inconveniences? . Kulikuwa na udharura gani kuuzuia mialiko hiyo mapema at the planing stage na kuja kuahirisha kwa mtindo wa zimamoto at the last minute?!.

Kuna kitu kinaitwa "A legitimate expectations", mtu akiishajiandaa kwa safari, na unachukua malipo, unakuwa umeishajiondoa nyumbani na kujipanga kisafari safari, tena wengine hata kupanga utalala wapi na bulangeti la aina gani!, wengine husafiri na ndoo, wengine vidumu na wengine watajua mbele kwa mbele alimradi ni safari halali ya kikazi.

Safari kama hiyo inaweza tuu kuahirishwa kama kumetokea jambo ambalo halikutarajiwa "force majeure", lakini safari inapoahirishwa kwa uamuzi tuu wa utashi wa kiongozi bila kutumia sheria yoyote wala kanuni yoyote, then a legitimate expectations zinawataka watumishi waliokwisha lipwa fedha, kurudishwa zile fedha tuu ambazo hazijatumika ambazo ni fedha za maduhuli (imprest) lakini hawapaswi kurudisha zile fedha za masurufu (allowances), hizo ni halali yao kisheria.

Kitu kingine muhimu kupitia sheria mpya ya the right to information, wananchi tunapaswa kuelezwa maamuzi haya ya Zimamoto yameleta tija gani, kiasi gani kimeokolewa na fedha hizo zimefanyia maendeleo gani isije kuwa watu Tunatwanga Maji Kwenye Kinu, kisha tunapongezana kwa uamuzi wa busara.

Lilipoundwa Baraza ndogo la Mawaziri huku makatibu wakuu wakiongezeka, kuna watu tulisema humu tumeongeza gharama za uendeshaji wa serikali badala ya kupunguza, hata baada ya kupungua wafanyakazi hewa na kutoajiri wafanyakazi wapya, wage bill ya serikali bado unazidi kuongezeka badala ya kupungua, ili usije kuwa ni kutwanga maji kwenye Kinu, wananchi tuambiwe kupunguza ukubwa wa serikali tume save kiasi gani, safari za nje tumeokoa kiasi gani,kufuta sherehe za uhuru tumeokoa kiasi gani, na hizi fedha zote zililookolewa ndio zimepelekwa kwenye huduma za jamii kama afya, elimu etc, ili Watanzania tuone tija ya kubana matumizi na sio kubana matumizi huku tukitwanga maji kwenye Kinu.

Wakati tukiendelea kumpongeza rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa maamuzi yake yenye tija kwa taifa letu, tuendelee kumsisitizia kuwa taifa hili linahitaji zaidi kujengwa kwa mifumo ya uwajibikaji na matumizi mazuri ya fedha za umma kwa shughuli zote zisizo na manufaa kwa taifa zikiwemo mbio za mwenge, na sherehe nyingine mbalimbali zisizo na maslahi kwa taifa zifutwe rasmi kwa waraka na sio kutegemea utashi tuu wa rais.

Suala la nini kina manufaa kwa taifa na nini hakina manufaa kutajulikana kwa kupokea mrejesho na you never know taifa letu linaweza kufikia hatua ya kujenga mfumo wa SMART OBJECTIVES, hadi tukagundua hata post za Wakuu wa Wilaya post za kikoloni tuu hazina maana yoyote kwa sababu Wakurugenzi wa Halmashauri wanatosha sana tuu hivyo gharama za Wakuu Wa Wilaya nazo ni ufisadi tuu, post hizi zikifutwa zitalisaidia sana taifa letu.

Hongera sana rais wetu mpendwa Mhe Dr John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchukua maamuzi magumu kulisaidia taifa letu lenye lindi la umasikini uliotopea uliogubikwa na rushwa na ufisadi, maamuzi haya hata yakiitwa ni ya udikiteta, then afadhali ya udikiteta ili taifa liponywe kama kilivyo kidonge kichungu cha dawa au sindano yenye maumivu ndio iponyeshayo.
Nawatakia maandimisho mema ya Nyerere Day hapo kesho.

Wa Salaam
Pasco
Rejea.
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...
kwani hujajua bado kuwa hii ni movie?
 
Futa mkuu wa Wilaya Hata polepole anakubaliana na hili wazo.
Mwenge Utunzwe Uwe unawashwa na Kuzima siku ya Kumbukumbu ya Uhuru.Sioni logic kutembea na mwenge kwenda kufungua Miradi ambayo ipo tayari. Mradi haufunguliwi Mradi Unafungwa na kutoka kwenye mradi na kuwa operation.


Ahsante mkuu Pasco.
 
Ni nzuri sana,maana hata wastaafu watumie viinua mgongo vyao kulisha familia zao.Kwanza asilimia 99 ya hao wastaafu wetu wamekwapua mali za umma
Wastaafu wengi ni mzigo kwa taifa, hata hawajitokezi kutoa ushauri ktk maswala mhimu yanayohitaji uzoefu na weledi wao wengi wao hujitokeza wakati wakampeni, Sana sana nao wamekuwa chombeza tu.
 
Ukiona hivyo jua hata mkulu hajui kinachoendelea ndani ya kaya yake. Watu wanagawana posho alafu yeye nashtuka siku ya mwisho. Hapo kuna tatizo
 
Pasco
Zamani ilikuwa ukisikiliza mpira unatangazwa redioni mara nyingi ungesikia "Lunyamila na mpira, Lunyamila anakwenda, Lunyamila, Lunya, Lunya...." Dakika mbili nzima mpira anao mtu mmoja.
Siku hizi hata hao mastaa kina Messi husikii wakikimbia na mpira na wakipenda kutajwa wao tu...One touch pass the ball

Je huoni kwamba kuna mazingira ya mchezaji mmoja ndio anapenda jina lake tu litajwe na watangazaji [media] hata kama tupo zama za kucheza ki-Timu?
Ha ha ha eti lunya lunya kitambo
 
Back
Top Bottom