Fahari Investment: Changamkia fursa kwa shilingi 3000 tu

Hii kitu sio lazima uanze na kiingilio cha sh. 3000 ukisoma vizur hapo utaona kuna viingilio tofauti tofauti, ni kwa sababu kama umeamua kujiunga kwa kifurushi cha sh. 3000 basi hata hao utakaowaunga watakuwa wanajiunga kwa sh. 3000 natumia kiwango cha chini zaidi nikilenga maisha halisi ya watanzania wengi kwani hawana kipato kikubwa Ila kama MTU unachannel za watu ambao unajua wanaweza kujiunga kwa vifurushi vikubwa haina shida unajiunga tu.....
Halafu nyie mnaosema hii kitu ni ujinga kuliko kubeti mnakosea betting unarisk pesa ambayo unajua unaweza ukala au ukaliwa hapa tunafanya investment ambayo ukishaweka pesa Mara moja unategemea kupata faida kwa kipindi Fulani na hii utaona inafaida haraka kama utakuwa na channel ya watu wengi....

Changamoto ya hizi biashara ni kwamba unamtegemea MTU ajiunge then ndo ulipwe lakini sidhani kama ni jambo jema kusema kuwa hii kitu ni ya utapeli....kuna system ambazo ni zakimatapeli lakini sio hii
Chanzo cha pesa kwenye hyo kampuni yako ni Nini?
 
JAMAA KAJIZUNGUSHAA KUTAJA VITU KIBAO MARA KILIMO,MARA MIRADI MWISHO WA SIKU KAANGUKIA KULE KULE KWENYE MICHEZO YA UPATU.
ILISHAFANYIKA SANA HYO MICHEZO MIAKA HIYO KITAMBO.
KUNA VIKAMPUNI VINGI SANA VILIANZISHWA LKN LEO HII VIMEPOTELEA HEWANI.
MOJAWAPO ILIKUWA INAITWA ELNET AFRICA.
ANADHANI TUTAINGIA HIVI HIVI TU
 
Utaokota watu wako kadhaa sibure...ila utapeli sio biashara. Ingekuwa rahisi kihivyo ungeshakuwa tajiri wewe na ukoo wako kwanza...wengine tungekuomba utuunge nasio wewe kutuomba tujiunge!!
 
Mkuu hii ni kama unavyosikia hawa forever, na makampuni mengine Ila huku hakuna kununua bidhaa Ila unafaidika pale unapowashirikisha wenzako kiingilio ni kuanzia sh. 3000 ukishatoa hiyo basi hakuna charge zingine
Acha kuibia wananzengo,utalaaniwa
 
Facebook ungepata watu sio huku jamii forum ukiona mtu anatumia jamii forum mpe respect he/she is not stupid
 
Mkuu sio kila kitu cha kubisha me jamaa flani kaning'ang'aniza juzi nijiunge nikaamua kujaribu leo nimewithdraw 18000 kiulaini kama ningejiufanya mjuaji hata ya pango ningekosa ukijunga ni kuchukua link yako ya reffer na kuishare kazi kwao watu kui-click na kujoin na sio kama kampuni nyingine masuala ya kuitana kwenye vikao nk
Hyo uliyopewa wewe maana yake wameliwa wenzako ukapewa wewe.
Hivyo vitu havijaanza leo labda wewe ndio mgeni wa hayo mambo.
Hiyo chain huwa inakwendaa then badae wanakuja kulia watu
 
Haya dakika ya 80 hiyo mabao ni bila kwa bila...Si tapeli wala mtapeliwa ambae kashaona lango la mwenzake......Mwalimu Kashasha, unaizungumziaje hii?
 
Back
Top Bottom