Anakata
Senior Member
- Aug 4, 2020
- 171
- 252
VIFAA VINAVYOHITAJIKAnaomba brief kidogo ya gharama ya both,nahitaji kufunga moja wapo kwenye biashara yangu
1. IP Camera(aka IP CCTV Cameras, Network Cameras, Digital Cameras, Security Cameras & Web Cameras)
- IP Camera
- NVR(Network Video Recorder)
- Cat6 UTP Cable
- Cat6 RJ Connectors
- Surveillance HDD(Hard Disk Drive)
- LED/LCD Monitor/Screen
- Analog Camera
- DVR(Digital Video Recorder)
- PSU(Power Supply Unit)
- BNC Crimp Connectors
- RG59+2C Cable
- Surveillance HDD(Hard Disk Drive)
- LED/LCD Monitor/Screen
- Gharama za kuuhudumia mfumo zipo chini, hii ni kwasababu mfumo wa IP Camera hauna vifaa vingi ukilinganisha na mfumo wa analog, mfano, ukingalia hapo juu utaona idadi ya vifaa vinayotakiwa na mfumo wa IP Cameara ni chache.
- Mfumo wa IP Camera hauhitaji waya nyingi ukilinganisha na mfumo wa analog, kwanini? kwenye mfumo wa IP, waya(cable) i.e in Cat5e/Cat6, unaotumika kuunganisha camera na NVR ni huohuo utakaobeba signal za video na power kwasababu NVR in mfumo wa switch uitwao PoE(Power over Ethernet) yaani camera inapata umeme kutoka kwenye switch moja kwa moja bila kuhitaji chanzo kingine cha umeme kama ilivyo kwenye mfumo wa analog, ambao utahitaji PSU na cable mbili kwa ajili ya signal ya video na power.
- IP Camera zina ubora wa juu wa video
- Unaweza kutumia IP Cameras pekee kwenye nyumba/au sehemu ya biashara kuliko bila kuwa na NVR, kwasababu zipo IP Camera ambazo zina uwezo wa kuhifadhi recorded footage kweye built-in microSD card slot hadi 256GB, hii ni tofauti na mfumo wa analog ambao ni lazima uwe au utumie DVR.
GHARAMA
- IP Camera System - Makadirio ya kamera nne za 2MP ni TZS 1,200,00 hadi 1,500,000
- Analog Camera System - Makadirio ya kamera nne za 2MP ni TZS 1,100,000 hadi 1,300,000
Kwasasa kuna IP camera zenye hadi 30megapixels, ila kwa soko letu nimeona za hadi 12MP.
Ni hayo tu kwa uchache.