Fahamu ni kwa namna gani unaweza kuongea na Watoto kuhusu mlipuko wa CoronaVirus

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Ni rahisi kuhisi kuzidiwa na kila kitu unachosikia kuhusu #COVID_19. Inaeleweka pia ikiwa watoto wako wanahisi wasiwasi. Watoto wanaweza kupata shida kuelewa kile wanachokiona mtandaoni au kwenye Runinga - au kusikia kutoka kwa watu wengine - kwa hivyo wanaweza kuwa katika hatari ya kuhisi wasiwasi, mafadhaiko na huzuni. Lakini kuwa na mazungumzo ya wazi na watoto kunaweza kuwasaidia kuelewa na kukabiliana na ugonjwa huu

Blue Brushstroke Moms Influencer Asymmetry Facebook Post Set(39).png

Katika kuzungumza na watoto kuhusu mlipuko huu fuata nji ahizi zifuatazo;

1. Uliza maswali ya wazi na sikiliza
Fahamu kwanza anajua nini kuhusu #Corona na muache aongoze mazungumzo. Thamini hisia zake na muahakikishe kuwa ni kawaida kuhisi hofu juu ya vitu hivi. Kama ni mdogo na hajui kuhusu Corona, unaweza usimwambie ili usimpe hofu mpya ila mfundishe kuhusu usafi kwa ujumla

Hakikisha uko katika mazingira salama na umruhusu mtoto wako azungumze kwa uhuru. Mchoro, hadithi na shughuli zingine zinaweza kusaidia kufungua mjadala

Onyesha kuwa unasikiliza kwa kuwapa umakini wako kamili, na hakikisha wanaelewa kuwa wanaweza kuzungumza na wewe wakati wowote wanapotaka.

2. Kuwa mwaminifu, eleza ukweli kwa njia rafiki mtoto
Watoto wana haki ya kupata taarifa ya kweli juu ya kile kinachotokea ulimwenguni, lakini watu wazima pia wana jukumu la kuwalinda ili wasipate mawazo. Kama hujui jibu la swali lake usibahatishe, tumia nafasi hiyo kutafuta majibu pamoja hata mtandaoni

3. Waoneshe namna ya kujinda na #CoronaVirus
Wahamasishe kunawa mikono mara kwa mara. Haihitaji kuwa mazungumzo ya kutisha. Pia unaweza kuwafunsha kupiga chafya au kukohoa na kujizuia kwa kutumia sehemu ya ndani ya kiwiko. Waambie wakueleze watakapoanza kuhisi dalili za ugonjwa huo

4. Bila Kuwatisha waeleze kwa namna mapambano yanavyoendelea
Waeleze kwa namna wafanyikazi wa afya, wanasayansi na watu wengine ambao wanafanya kazi kuzuia kuenea kwa #COVID19 na kuweka jamii salama. Inaweza kuwa faraja kubwa kujua kwamba watu wenye huruma wanachukua hatua

5. Funga mjadala kwa kuonesha kujali na kutoa uhakika
Ikiwa unakabiliwa na mlipuko katika eneo lako, wakumbushe watoto wako kwamba hawawezi kupata ugonjwa huo kirahisi, kwamba watu wengi wenye ugonjwa huo hawaugui sana na kuwa jitihada zinaendelea kuzuia maambukizi

Wakumbushe watoto wako kuwa wanaweza kuwa na mazungumzo mengine magumu na wewe wakati wowote. Wakumbushe kwamba unajali, unasikiliza na unapatikana kila wanapohisi kuwa na wasiwasi
 
Tumezoea kuwaona watoto wetu wakisimama kwenye magari kisa wanalipa 200. Sasa janga limeingia na tunatakiwa level seat. Japo shule zimefungwa zikifunguliwa watasafirije kufika shuleni?

Nao watakaa level siti?
 
Wazazi mnatakiwa kuwa makini mnapowaambia habari zinazohusu corona au kuongelea sana habari nzito nzito zinazohusu corona kama vifo na vitisho vya corona mana zinaweza kumpelekea mtoto kupata distress ,ambayo inaweza kusababisha mtoto kupata magonjwa ya moyo, kukojoa kitandani,na kuogopa kipindi cha usiku pia hali iyo inatokana na wao kuona utaratibu wao wa maisha mbona umebadilika tofauti na mwanzo ,maana wanashangaa mbona hawaendi tena shule kama mwanzo?,wanahisi corona ni kitu kinachotisha kama simba, ushauri wangu kwa wazazi mpunguze kuongelea corona mbele za watoto hasa zihusuzo idadi ya vifo,maana watoto wa kuanzia miaka 2 na kuendelea ushika sana information,
ASANTENI
 
As long as corona virus continues to threaten the livelihood of Tanzanians! Forget about reopening of schools and colleges
 
Tumezoea kuwaona watoto wetu wakisimama kwenye magari kisa wanalipa 200.sasa janga limeingia na tunatakiwa level seat. japo shule zimefungwa zikifunguliwa watasafirije kufika shuleni?
nao watakaa level siti?
Ndo hapo sasa lakini tutafika tuu.
 
Shule zinafunguliwa lini?. Mbona watu wengine mnakuwa na hofu sana juu ya mambo yajayo hata bila kujua kama yakifika yatakuwa vivyo hivyo mnavyoyatarajia?. Vitabu vitakatifu vinasema, "msisumbukie mambo ya kesho, kila siku yatosha uovu wake yenyewe"
Nimekubaliana na ule utafiti unaosema, asilimia 50 ya watu hupata msongo/stress kwa mambo yajayo ambayo hata hivyo, hayatatokea.
Hadi shule zikifunguliwa, naamini taratibu zao zote za namna ya kufika shuleni, namna ya kukaa shuleni hadi kurudi nyumbani zitakuwa zimewekea utaratibu ambao utakuwa ni rafiki kwa watoto wetu. Relax
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom