Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,692
- 155,120
MAKOROKOCHO MARKET 🇹🇿
FAHAMU JINSI KUKU ANAVYOTUMIKA KATIKA ULIMWENGU WA GIZA MBALI NA KITOWEO.
Wengi wetu tunamtambua kuku ni kama ndege afugwaye na watu wengi na kutumika kama kitoweo, kutoa mayai ukiuza unapata pesa lakini kumbe kuna siri kubwa ambayo ndege huyu Mungu amemuumbia nazo pasipo watu wengi kuzijua zenye faida kibao kwa mwanadamu, kivipi? Hebu nifuate.....
Kuku huyu yupo katika jinsia mbili kama viumbe wengine yaani Jogoo na Koo ila hapa nieleweke kuku ninaemsemea hapa ni kienyeji na si hao wanyama,mayai au aina nyingine mbali na hiyo.
Leo nitakupa faida za jinsia hizi mbili katika maisha ya mwanadamu kiafya kupambana na matatizo mbalimbali yatokanayo na nguvu za Giza pamoja na kujiletea manufaa ya kimaisha.
1.JOGOO;
Hii ni jinsia ya kuku wa kiume ambaye ana mambo mengi ya ajabu, kwanza Jogoo mweupe hutumika kama tulizo la magonjwa yote ya kichawi kwa mtu sababu amebeba nguvu ya uzima ndani yake.
Ukichukua ile nyama yake ya kichwani ambayo ipo kama upanga na kuchanganya na dawa husika basi inauwezo wa kuita kimbunga cha katrina, mbegu zake hutumika kutengeneza dawa kali kabisa ya nguvu za kiume hii ndiyo walikua wakitumia machifu hapo zamani na kuwa na uwezo wa kumiliki wake zaidi ya kumi hivyo ukiwa na dawa hii ni lazima uwe na wanawake wa kutosha.
Nyoya lake hutumika kutibia ugonjwa wa ndimi mbili, ubongo wake hutumika kutoa taarifa kwa njia ya njozi au kujua endapo mbaya wako anakuandama tena ndani ya wakati kama jinsi yeye atambuapo masaa na kuwika.
Mshipa wake wa shingoni hutumika kutibia matatizo ya ganzi mwilini
Jicho lake hutumika kuona chochote kisichoonekana katika hali ya kawaida kama kuona wachawi, misukule au chuma ulete akija kwenye biashara yako.
Pia Jogoo mweusi hutumika katika mazindiko ya kuficha mali, pesa au nyumba na wewe mwenyewe usionekane na mchawi au jambazi.
2.KOO
Huyu hutumika katika kufungua kizazi au mwanamke alie tasa kuzaa ila kwa kulogwa tu husaidia huyo mtu kuzaa,
Pia hutumika kufungia mimba zinazoporomoka au kudondoka
Mayai yake hutumika kumfungua mtu aliyefungwa kichawi yaani nuksi, pia yai lake ambalo ni viza hutumika kusambaratisha ubaya wa adui au kumrudishia ubaya wake.
Lakini pia kuku ndio kafara kubwa itumikayo kama ufunguo wa kufungulia ulimwengu wa Giza yaani kuita mizimu, majini, na kuwatuma utakacho ila hapa itategemea na moyo wako umekusudia kuwatuma kwa ubaya au jambo zuri.
Mambo ni mengi ila kwa leo niishie hapa. Sio kila unachosoma mtandaoni kina ukweli, vingine ni magirini na miyeyusho, unalainishwa ili upigwe.
NAWATAKIA HERI YA NOELI NA MWAKA MPYA.
FAHAMU JINSI KUKU ANAVYOTUMIKA KATIKA ULIMWENGU WA GIZA MBALI NA KITOWEO.
Wengi wetu tunamtambua kuku ni kama ndege afugwaye na watu wengi na kutumika kama kitoweo, kutoa mayai ukiuza unapata pesa lakini kumbe kuna siri kubwa ambayo ndege huyu Mungu amemuumbia nazo pasipo watu wengi kuzijua zenye faida kibao kwa mwanadamu, kivipi? Hebu nifuate.....
Kuku huyu yupo katika jinsia mbili kama viumbe wengine yaani Jogoo na Koo ila hapa nieleweke kuku ninaemsemea hapa ni kienyeji na si hao wanyama,mayai au aina nyingine mbali na hiyo.
Leo nitakupa faida za jinsia hizi mbili katika maisha ya mwanadamu kiafya kupambana na matatizo mbalimbali yatokanayo na nguvu za Giza pamoja na kujiletea manufaa ya kimaisha.
1.JOGOO;
Hii ni jinsia ya kuku wa kiume ambaye ana mambo mengi ya ajabu, kwanza Jogoo mweupe hutumika kama tulizo la magonjwa yote ya kichawi kwa mtu sababu amebeba nguvu ya uzima ndani yake.
Ukichukua ile nyama yake ya kichwani ambayo ipo kama upanga na kuchanganya na dawa husika basi inauwezo wa kuita kimbunga cha katrina, mbegu zake hutumika kutengeneza dawa kali kabisa ya nguvu za kiume hii ndiyo walikua wakitumia machifu hapo zamani na kuwa na uwezo wa kumiliki wake zaidi ya kumi hivyo ukiwa na dawa hii ni lazima uwe na wanawake wa kutosha.
Nyoya lake hutumika kutibia ugonjwa wa ndimi mbili, ubongo wake hutumika kutoa taarifa kwa njia ya njozi au kujua endapo mbaya wako anakuandama tena ndani ya wakati kama jinsi yeye atambuapo masaa na kuwika.
Mshipa wake wa shingoni hutumika kutibia matatizo ya ganzi mwilini
Jicho lake hutumika kuona chochote kisichoonekana katika hali ya kawaida kama kuona wachawi, misukule au chuma ulete akija kwenye biashara yako.
Pia Jogoo mweusi hutumika katika mazindiko ya kuficha mali, pesa au nyumba na wewe mwenyewe usionekane na mchawi au jambazi.
2.KOO
Huyu hutumika katika kufungua kizazi au mwanamke alie tasa kuzaa ila kwa kulogwa tu husaidia huyo mtu kuzaa,
Pia hutumika kufungia mimba zinazoporomoka au kudondoka
Mayai yake hutumika kumfungua mtu aliyefungwa kichawi yaani nuksi, pia yai lake ambalo ni viza hutumika kusambaratisha ubaya wa adui au kumrudishia ubaya wake.
Lakini pia kuku ndio kafara kubwa itumikayo kama ufunguo wa kufungulia ulimwengu wa Giza yaani kuita mizimu, majini, na kuwatuma utakacho ila hapa itategemea na moyo wako umekusudia kuwatuma kwa ubaya au jambo zuri.
Mambo ni mengi ila kwa leo niishie hapa. Sio kila unachosoma mtandaoni kina ukweli, vingine ni magirini na miyeyusho, unalainishwa ili upigwe.
NAWATAKIA HERI YA NOELI NA MWAKA MPYA.