Fahamu matumizi ya simu za mkononi mbali na kupigia picha

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397


Kuna matumizi mengi sana ya kamera ya simu janja zetu ukiachana na yale tuliyo yazoea ya kupiga picha tu

Unajua kama kamera ya simu janja yako inaweza ikawa na matumizi lukuki ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kurahisisha maisha yako



1. Scan Nyaraka

Kamera ya simu janja yako pia inaweza ikawa ina’scan’ nyaraka tofauti tofauti. Pata picha unakuwa na ‘scanner’ ambayo ipo mfukoni kwako. Unaweza uka ‘scan’ vitu kama vile mikataba,risiti au kitu chochote kilichopo katika karatasi na unataka ukifanye kiwe kidigitali

Baada ya hapo unaweza ukaamua kutuma vitu hivyo katika barua pepe au unaweza ukavihifadhi katika mfumo wa PDF au JPG
Unataka ku’scan’ vitu?

Kwa iOS shusha(download) Evernote

Kwa Android shusha Google Drive ndani yake kuna kipengele cha ku’Scan’

2. Tumia Kamera Ya Simu Janja Yako Kama Mkalimani Wako

Teknolojia inabadilisha dunia kwa kiasi kikubwa sana miaka kadhaa iliyopita ningebisha kata kata kama jambo hili lingeweza kutokea. Hivi unajua unaweza ukatumia kamera ya simu yako ili kutafsiri lugha Fulani?

Kumbuka kuna maandishi huwa yanaandikwa na mara nyingi tunakuwa hatuyaelewi kwa mfano ukiwa katika mgahawa ikaja menyu yenye maandishi ya kigeni hapo ndipo huduma hii utakapo ona ubora wake

Ukiwa na App ya Google Translate, ambayo inaweza kutafsiri lugha 29 utafanikisha hilo kwa kuweka kamera mbele ya maandishi yaliyoandikwa na hapo App itafanya zoezi zima la kutafsiri kwenda katika lugha unayotaka

3. Tumia Kama Kamera Ya Ulinzi

Hivi ulishawahi kuwa na hamu ya kutumia kamera ya simu yako kama njia ya ulinzi? Labda una kamzigo kako pale ndani na unataka ukachunge. Ondoa shaka kuna App maalum ambazo zinakuwezesha kufanya hayo yote. App hizi hutumia kamera ya simu janja ili kugundua mwondoko wa aina yeyote (motion) na kisha kukutaariffu kupitia barua pepe (e-mail) yako

Kwa Android shusha App ya Silent Eye

4. Fuatilia Barcodes Za UPC

Wakati mwingine wakati ukiwa unafanya manunuzi ya vitu na ukawa huna uhakika kama unanunua vitu imara achana na ku Google, tumia kamera ya simu janja yako kuweza kuichunguza bidhaa hiyo.

Zile App ambazo zinamsaidia mtu ku’scan code’ za UPC zinampatia mtu taarifa za bidhaa katika kiganja chake kabisa. Ukiachana na taarifa kuhusiana na bidhaa bado utaweza kufananisha bei tofauti tofauti ya bidhaa hizo ili kujua kama umepewa bei nzuri au la

Kwa Android shusha App ya ShopSavvy Barcode and QR Scanner

5. Shangaa Anga

Hivi ushawahi kukaa usiku na ukawa unashangaa anga na ukaanza kujiuliza maswali kama baadhi ya vitu unavyoviona ni nyota au ni sayari zingine?

Sasa App ya Skyview kwa Android na iOs itakupa majibu yote

App hii inatumia kamera ya simu yako katika kukuonyesha jinsi anga ilivyo cha kufanya hapa wewe elekeza kamera ya simu janja yako katika anga.

Pia kama remote ya Tv au kisimbusi inasumbua unaweza kutumia kamera ya simu kuona kama remote hiyo inatoa mionzi au la kabla ya kuchukua hatua nyingine kama kubadili betri au kuitengeneza.Washa kamera ya simu,nyoshea kile kitaa cha remote kwenye kamera huku ukiwa una bonyeza vitufe kwenye remote.Utaona mwanga unawaka kwenye screen ya simu endapo kama remote ni nzima

> Source: Ulimwengu Wa Teknolojia
 
Pia naipenda sana App ya Gesture lock screen, MTU akishika simu yako lazima imupige picha bila yeye kujijua, kisha picha itatumwa kwenye Email yako. Hata kama simu imeibiwa unaweza kuipata kiurahisi,
Na ukishika mhusika inakuaje?
 
Back
Top Bottom