Fahamu mambo mbalimbali kuhusu Kilimo cha Korosho

Naomba kujuana juu ya kilimo hicho cha korosho
Nipo ikungi singida nataka nipande miche 2000
Ni wapi ntaipata hii miche na kwa gharama gani?
Na wapi ntaweza kuuza korosho?
 
Unataka kupanda kitu usichokifahamu vizuri,yani hata soko hujui.Fanya utafiti wa soko.Mikoa mingi sana wanamipango ya kupanda korosho ikiwemo Dom, Mbeya na Kigoma. Kutokana na kanuni ya Demand and Supply sidhani kama hill zao litakuwa natija hasa kwa mfumo waa kutegemea wahindi. Kama haktakuwa na viwanda vya kuchakata korosho hazitakuwa dili labda watz wenyewe waanze Ku-export.
 
Unataka kupanda kitu usichokifahamu vizuri, yani hata soko hujui.Fanya utafiti wa soko.Mikoa mingi sana wanamipango ya kupanda korosho ikiwemo Dom,Mbeya na Kigoma. Kutokana na kanuni ya Demand and Supply sidhani kama hill zao litakuwa natija hasa kwa mfumo waa kutegemea wahindi. Kama haktakuwa na viwanda vya kuchakata korosho hazitakuwa dili labda watz wenyewe waanze Ku export.
Tunafanyaje sasa sisi wa kuliwa tumeachana na uctumie wa karibu tunapambana kuufikia.
 
tunafanyaje sasa sisi wa kuliwa tumeachana na uctumie wa karibu tunapambana kuufikia
Fanya market survey and projection ya ten years mbele.Andaa your business proposal iwapo wanunuzi hawatakuwepo utauzaje bidhaa yako.Heka 2000 zinatosha Ku export kwa mjasiliamali mdogo.Panda hizo korosho ila usitegemee wahindi wanunue kwa 100% .Jenga uwezo binafsi qa kuuza bila kumtegemea MTU au serikali.UWazo lako ni zuri ila fikiria zaidi ta kupanda.

. Kusindika korosho zilizobanguliwa
. Kutengeneza bidhaa ndogondogo kutokana na korosho
. Kutengeneza wine.
. Kutumia maganda ya korosho kama nishati..kuzalisha mafuta yatokanayo na korosho..
Kutengeneza juisi kutokana na mabibo.

Anza kupanda weka side plan jinsi ya kuuza korisho zako.
.
 
Binafsi nimeingia ktk zao La parachichi, sasa najiuliza iwapo hawa wazungu na wakenya wasipo kuja kununua nitafanyaje na heka zang 30?

Kwa hio nimeamua nitaanzisha usindikaji wa juisi nikapambane na MOE, kwa kuwa Mimi nazalisha parachichi nitasindika na kuuza pungufu ya moe.

Nauhakika nitauza.Vilevile nitasindika parachichi ghafi na kuingia mtaani mwenyewe bila kusubiri walanguzi.Nchi inamiundimbinu muzuri, hata sudani kusini nauwezo wa kufikisha mzigo.Huku sio kipindi cha kuhofia soko,soko ni akili yako.

Nakushauri panda mazao yaki"Kilimo hai" hutaangaika wanunuzi,watajileta wenyewe.
 
Nina mikorosho km 30 shamba langu la urithi, mavuno madogo nifanye nini nipate mihela mingi.
 
Kununua mbegu unachukua maji na chumvi 100g ya chumvi unaweka katika maji kiasi cha lita 5 unakoroga vizuri na unachukua mbegu zako unaweka kwenye maji hayo zile zitakazo zama ndio mbegu zenye uwezekano mkubwa wa kiota.

NAOMBA UFAFANUZI ZAIDI unaloweka kwa muda gani kwenye maji ya chumvi kabla ya kupanda mbegu?
Wang Shu
 
kununua mbegu unachukua maji na chumvi 100g ya chumvi unaweka katika maji kiasi cha lita 5 unakoroga vizuri na unachukua mbegu zako unaweka kwenye maji hayo zile zitakazo zama ndio mbegu zenye uwezekano mkubwa wa kiota.


NAOMBA UFAFANUZI ZAIDI unaloweka kwa muda gani kwenye maji ya chumvi kabla ya kupanda mbegu?
Wang Shu
masaa 24 adi 72 tu inatosha kukuonyesha mbegu mzima na mbovu, ukitaka pia unaeza kuziacha adi siku 4 adi 5 kwenye maji ili zisichelewe kuota ukienda kupanda.
 
MREJESHO WA THREAD HII KUHUSU KOROSHO.

Napenda kuwashirikisha japo kwa uchache hatua niliyofikia baada ya kuandaa shamba la ekari 25. Hapa chini nimeweka picha za mikorosho niliyopanda japo changamoto ni nyingi sana na ukiwa muoga unaweza kuachia ngazi. Nilichojifunza: Fika mwenyewe shambani, epuka kuwaamini watu kwa kufanya kilimo cha simu
LUMUMBA
.View attachment 1293371View attachment 1293373View attachment 1293376

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba unisaidie ulipipata mbegu, nahitaji kuanza hichi kilimo tafadhali
 
Wakuu Salaam,

Napenda kuwashirikisha kwenye fursa hii ya korosho tena, Nilihamasika na kufuatilia kilimo cha korosho katika mikoa ya kanda ya kati, yaani Dodoma na Singida.

Sina data za uhakika lkn kwa taarifa zilizopo ardhi ya Singida na Dodoma zinafaa sana kulima korosho na yield yake ni kubwa kushinda mikoa ya kusini.

Wilayani manyoni zimepandwa korosho nyingi sana karibu hekta 12000 na zinavutia kwa kweli, Kitu kizuri ardhi bado sio ghali huku nami nishaanza kuchukua mamia ya ekari kwa kilimo hiki.
Wanauza je huko mapori?
 
PatriceLumumba naweza kuwaangamiza kwa mbinu ipi wadudu wanaoshambulia mashina ya mikorosho hadi kukausha mti?
Wadudu hao hutoboa mti na kupekecha ganda la nje kuzunguka mti wote na wanamuonekano kama funza.
 
Though imenichukua muda,nimefanikiwa kuusoma uzi wote na nimekutana na mengi ya kunivutia kujiingiza katika kilimo hiki,,lakini sijaona maelezo yanayoeleza kwamba korosho ni malighafi ya kutengeneza bidhaa gani tofauti na kuliwa kawaida,,?
pia nimeona tunategemea zaidi soko LA nje kwa hao wahindi,,je hatuwezi kutengeneza uhitaji wa bidhaa za korosho hapa ndani ya nchi ili viwepo pia viwanda vitavyokuwa vikinunua korosho na baadae kuleta bidhaa zinazotokana na korosho
 
Aliyopo kwenye mnada leo masasi na Tandahimba atupe mrejesho wa bei kama mnada umeshafanyika huko
 
Anayependa kupata Miche Bora ya mikorosho awasiliane nami no 0784474935 nipo masasi, nasambaza Miche popote ulipo. Mwaka Jana nilisambaza Miche 4000 singida
 
Back
Top Bottom