Fahamu machache kuhusu special presidential division: Kikosi maalumu kilichomlinda Mobutu Seseseko enzi za utawala wake

kadoda11

JF-Expert Member
Jan 6, 2011
21,453
20,712
Special presidential division(SPD) ni kikosi maalumu cha jeshi alichounda mzee Mobutu mwenyewe mwaka 1985 kwa jukumu la kumlinda yeye na familia yake pia kushughulikia maadui wote wa mzee kwa namna ambayo wao SPD waliona inafaa.

Wanajeshi wa SPD walikuwa wanapewa mafunzo maalum na washauri wa kijeshi toka jeshi la israel ambao kwa namna moja ama nyingine walikuwa na ushirika na mzee mobutu enzi za utawala wake.

Kamanda wa SPD alikuwa ni binamu yake na mzeee mobutu aliyefahamika kwa jina la Etienne Nzimbi Ngbale Kongo wa Basa ambaye pamoja majukumu mengine alihakikisha recruitee wote wa SPD wanatoka katika kabila la mzee Mobutu. ikumbukwe Mobutu alikuwa ni wa kabila la Ngbandi linalopatikana Kaskazini mwa DRC.

Mzee Mobutu aliitumia SPD kwa ufanisi mkubwa sana katika kukabiliana na maadui/washindani wake wa kisiasa.SPD ilitumika kuteka, kuua, kutesa, kuonea, kunyanyasa, kutisha na kupoteza watu kimyakimya, kuwaweka watu kizuizini, kufunga watu jela bila kesi, kutengeneza matukio ya kipropaganda nk. matukio yao yalikuwa ni zaidi ya matukio ya kikundi cha ''watu wasiojulikana''.

Hiki ndio kikosi ambacho moja ya makapteni wake alikuwa ni mtoto mtukutu wa mzee Mobutu na mtu wa kula bata aliyefahamika kwa jina la Kongulu Mobutu almaarufu Sadam Hussein(sadam sene). kwa wale wadau wa band ya wenge bcbg hili jina sio geni kwao maana jina lake limetajwa sana katika nyimbo za band hiyo zilitoka miaka ya tisini.

Miaka ya mwisho ambayo mzee Mobutu alikuwa anaelekea kupoteza ushawishi wa kuitawala Zaire, Kongulu alichukua jukumu la kuki-command kikosi cha SPD ambapo alihakikisha maadui wa baba yake ndani ya Zaire wanashughulikiwa barabara.

Kongulu alifariki mwaka 1998 jijini Monaco kwa maradhi ya ukimwi.

NB:
Nimeitafsiri kutoka nyanzo mbalimbali vya kwenye mtandao. karibuni kujazia nyama.
 
kongulu mobutu alias sadam hussein enzi za uhai wake akiyarudi mangoma katika moja ya live performance ya bendi za zaire.
 
Sijui kama ndio hawa ama wengine wajuzi watakuja nisahihisha..... Kuna maandamano yalitokea chuo kikuu cha umma huko lubumbashi miaka ya 90, vijana walifanya vurugu sana na mobutu wala hakushughulika nao ule mchana ila akasubiri waliporudi kulala.... Alituma makomandoo wake walichinja mmoja baada ya mwingine kati ya wale viongozi wa maandamano.... kuamka asbuhi ni vilio tu takriban wanafunzi zaidi ya 200 walichinjwa kwa visu!!! Kisa kudai haki!!!

Alafu nilimsikia mwanae yule mchungaji anadai Mobutu yupo mbinguni sababu wiki moja kabla ya kufa aliamua kuokoka na kuungama dhambi zake dah yaani madhambi yote yale na bado kaingia mbinguni aseew then ukute lumumba ndio yupo kuzimu!!! Kazi kwelikweli hii dunia

Cc Malcom Lumumba Red Giant Prof
 
Sijui kama ndio hawa ama wengine wajuzi watakuja nisahihisha..... Kuna maandamano yalitokea chuo kikuu cha umma huko lubumbashi miaka ya 90, vijana walifanya vurugu sana na mobutu wala hakushughulika nao ule mchana ila akasubiri waliporudi kulala.... Alituma makomandoo wake walichinja mmoja baada ya mwingine kati ya wale viongozi wa maandamano.... kuamka asbuhi ni vilio tu takriban wanafunzi zaidi ya 200 walichinjwa kwa visu!!! Kisa kudai haki!!!

Alafu nilimsikia mwanae yule mchungaji anadai Mobutu yupo mbinguni sababu wiki moja kabla ya kufa aliamua kuokoka na kuungama dhambi zake dah yaani madhambi yote yale na bado kaingia mbinguni aseew then ukute lumumba ndio yupo kuzimu!!! Kazi kwelikweli hii dunia

Cc Malcom Lumumba Red Giant Prof
ndio hao hao brother...
 
Ninajikaza nisikukosoe lkn nashindwa hapa..!Ungeandika mission hata moja walioitekeleza na sio waliua,waliteka,walipoteza watu n.k eleza kinagaubaga
ukisoma bandiko langu kwenye mada kuu, mwisho kabisa nimehitimisha kwa kukaribisha wadau wengine waje kujazia nyama.

sio kila kitu kuhusu spd katika bandiko hili lazima nikiwakilishe mimi, hata wewe unaweza kujiongeza kwa kueleza ya kwako unayoyajua kuhusu spd.

ulitaka ni nikutajie mission moja wapo?, hii hapa:

After the Rwandan Patriotic Army invaded northern Rwanda at the start of the civil war, Mobutu sent several hundred DSP troops to assist the government of Juvénal Habyarimana.

In 1993, the DSP was sent to quell unrest in Masisi, North Kivu but inflamed the situation after it sided with the Hutu residents against the indigenous Bahunde.

A 1996 United Nations report noted that Prime Minister Étienne Tshisekedi and his staff were subject to routine surveillance and harassment by DSP soldiers
 
ukisoma bandiko langu kwenye mada kuu, mwisho kabisa nimehitimisha kwa kukaribisha wadau wengine waje kujazia nyama.

sio kila kitu kuhusu spd katika bandiko hili lazima nikiwakilishe mimi, hata wewe unaweza kujiongeza kwa kueleza ya kwako unayoyajua kuhusu spd.

ulitaka ni nikutajie mission moja wapo?, hii hapa:

After the Rwandan Patriotic Army invaded northern Rwanda at the start of the civil war, Mobutu sent several hundred DSP troops to assist the government of Juvénal Habyarimana.

In 1993, the DSP was sent to quell unrest in Masisi, North Kivu but inflamed the situation after it sided with the Hutu residents against the indigenous Bahunde.

A 1996 United Nations report noted that Prime Minister Étienne Tshisekedi and his staff were subject to routine surveillance and harassment by DSP soldiers
Sasa ni "DSP" au ni "SPD"? km ulivyoitafsiri mwanzoni?
 
Sijui kama ndio hawa ama wengine wajuzi watakuja nisahihisha..... Kuna maandamano yalitokea chuo kikuu cha umma huko lubumbashi miaka ya 90, vijana walifanya vurugu sana na mobutu wala hakushughulika nao ule mchana ila akasubiri waliporudi kulala.... Alituma makomandoo wake walichinja mmoja baada ya mwingine kati ya wale viongozi wa maandamano.... kuamka asbuhi ni vilio tu takriban wanafunzi zaidi ya 200 walichinjwa kwa visu!!! Kisa kudai haki!!!

Alafu nilimsikia mwanae yule mchungaji anadai Mobutu yupo mbinguni sababu wiki moja kabla ya kufa aliamua kuokoka na kuungama dhambi zake dah yaani madhambi yote yale na bado kaingia mbinguni aseew then ukute lumumba ndio yupo kuzimu!!! Kazi kwelikweli hii dunia

Cc Malcom Lumumba Red Giant Prof
Hiyo cha mtoto mkuu miaka ya themanini waganga wa Mobutu walimwambia mzee nguvu zako za kichawi zinaelekea kupungua ili kuziimarisha zinahitajika damu za watoto wa kike bikira mia NNE..Likatolewa tangazo na serikali ya Zaire kwamba Ikulu ya Mobutu imeandaa sherehe ya kuwapongeza mabinti bikira ambayo itaenda sanjari na kuwazawadia scholarship ya kwenda kusoma Ufaransa..Unaambiawa within the twinkling of an eye " mzigo " ukawa umekamilika na.kusaza..Inasemekana wale mabinti walie da kuchinjwa kwa ajili ya kafara halafu miili yao ikapakiliwa kwenye meli ambayo ikaenda kuzamishwa kimagumashi baharini.Wazazi na wananchi wakatangaziwa meli imezama na miili imeshindikana kuopolewa..Wazazi na watu wote waliotaka kuhoji waliishia futi sita chini ya ardhi
 
Back
Top Bottom