Monica Mgeni
Member
- Oct 7, 2021
- 82
- 134
Mwalimu Ester Shayo
Moshi
22.07.2022
Nimepita katika mitandaoni nimeona maoni mbalimbali ya watumishi wa umma mbalimbali kuhusu ongezeko la mishahara yao katika mwaka wa fedha wa 2022/ 2023, baada ya Serikali kutangaza kuwa mishahara itaongezeka kwa 23.3%
Nimegundua kuwa baadhi ya wananchi wakiwemo watumishi wa umma hawakujua kuwa ongezeko la 23% lilikuwa kwa ajili ya kuwainua watumishi wa umma wenye mishahara ya kima cha chini.
Sasa nawafumbua macho ili kuondoa upotoshaji uliopo kutokana na uelewa mdogo uliopo juu ya suala hilo.
Ukweli ni kwamba katika mshahara uliongia siku ya leo watumishi wenye mishahara ya kima cha chini wameona kuwa kuna ongezeko kubwa katika mishahara yao, Ila watumishi wenye mishahara mikubwa wameona kuwa ongezeko ni dogo.
Hivyo basi hii inamaanisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais SAMIA SULUHU HASSAN imetekeleza ahadi ya kuboresha maslahi ya watumishi wa Umma wenye kipato cha chini kwa maslahi mapana ya Taifa na jamii kwa ujumla.
Nina imani kuwa kwa dhamira kuu ya Rais SAMIA SULUHU HASSAN huu ni mwanzo tu ila yajayo yanafurahisha kwa kuwa amedhamiria kuboresha zaidi maslahi ya watumishi wa umma. Tuendelee kumuunga mkono na kupiga kazi kwa bidii kulijenga Taifa letu.
Moshi
22.07.2022
Nimepita katika mitandaoni nimeona maoni mbalimbali ya watumishi wa umma mbalimbali kuhusu ongezeko la mishahara yao katika mwaka wa fedha wa 2022/ 2023, baada ya Serikali kutangaza kuwa mishahara itaongezeka kwa 23.3%
Nimegundua kuwa baadhi ya wananchi wakiwemo watumishi wa umma hawakujua kuwa ongezeko la 23% lilikuwa kwa ajili ya kuwainua watumishi wa umma wenye mishahara ya kima cha chini.
Sasa nawafumbua macho ili kuondoa upotoshaji uliopo kutokana na uelewa mdogo uliopo juu ya suala hilo.
Ukweli ni kwamba katika mshahara uliongia siku ya leo watumishi wenye mishahara ya kima cha chini wameona kuwa kuna ongezeko kubwa katika mishahara yao, Ila watumishi wenye mishahara mikubwa wameona kuwa ongezeko ni dogo.
Hivyo basi hii inamaanisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais SAMIA SULUHU HASSAN imetekeleza ahadi ya kuboresha maslahi ya watumishi wa Umma wenye kipato cha chini kwa maslahi mapana ya Taifa na jamii kwa ujumla.
Nina imani kuwa kwa dhamira kuu ya Rais SAMIA SULUHU HASSAN huu ni mwanzo tu ila yajayo yanafurahisha kwa kuwa amedhamiria kuboresha zaidi maslahi ya watumishi wa umma. Tuendelee kumuunga mkono na kupiga kazi kwa bidii kulijenga Taifa letu.