Fahamu kuhusu uzazi wa mpango wa kisasa/modern contraceptives

Mackjnr

Member
Mar 22, 2020
25
14
Ni kujuzana mambo haya ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango,ili unapoamua kutumia utumie ukiwa na taarifa sahihi.sitasimama upande kwa kusema hazifai au zinafaa ninachofanya ni kukuelimisha, nitaelekeza kwa Lugha ya kawaida Sana pasipo kuingia mwenye sayansi ngumu ambayo kiufupi haitanufaisha watu waliowengi,nitaangazia mazingira haya yafuatayo:-

1.maana ya uzazi wa mpango
2.makundi ya njia za uzazi wa mpango za kisasa
3.Faida ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango za kisasa
4.maudhi /side effects amboyo mtumiaji wa njia hizo anaweza kuyapata

> Nini maana ya uzazi wa mpango?
-uzazi wa mpango ni uamzi wa hiari wa MTU binafsi au yeye na mwenza wake kuamua,waanze lini kuzaa,wazae watoto wangapi,hapo watoto wapishane umri gani,na lini wataacha/ataacha kuzaa.

> Kuna makundi makuu matatu ya njia za uzazi wa mpango wa kisasa
!.njia za muda mfupi

.kondomo (me au ke)
.vidonge(vyenye kichocheo kimoja(POPs)vichocheo viwili(COCs) pamoja na emergency (P2)
.Sindano
.Njia ya unyonyeshaji
Njia ya kuchomoa uume unapokaribia kufika kileleni/withdraw
.njia ya kufuata kalenda
.njia ya ute
.njia ya joto/bathal body temperature

!!.njia za muda mrefu
.kipandikizi/vipandikizi
.kitanzi/Lupu

!!!.njia za kudumu
.kufunga kizazi mwanaume/Vasectomy
.kufunga kizazi mwanamke/BTL

>Faida za uzazi wa mpango
.husadia kurudisha Afya ya mwanamke kabla ya kubeba mimba nyingine
.husaidia kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na ujauzito na uzazi
.hupunguza vifo vya watoto .Husaidia kudumisha mahusiano na mwenza wako
.husaidia kupangashughuli za maendeleo ya familia,Jamii na taifa
.husaidia kuwapunguzia wazazi gharama au majukumu ya kulea familia kubwa
.huwawezesha vijana na wanawake kufikia malengo yao ya maisha
.huwapa wanawake nafasi ya kushiriki kwenue shughuli mbalimbali za kiuchumi na maendeleo.

>Maudhi/side effects ambazo mtumiaji anaweza kuzipata
Hapa naweka kwa ujumla wake bila kuangalia ni njia ipi,maana maudhi yanatofautiana njia moja na nyingine.
.maumivu ya Kichwa
.maumivu ya tumbo hasa chini ya kitovu
.maumivu ya mgongo
.kuongezeka uzito
.kuchoka kusiko kawaida
.Mzunguko wa hedhi kabadilika,kubkeed kwa mda mrefu(menorrhagia),kupata hedhi inayoambatana na maumivu ya tumbo na kiuno(dismenorrhea),kukosa hedhi(amenorrhea)
.kizunguzungu
.kukosa hamu ya tendo LA ndoa
.kichefuchefu

Haya ni baadhi ya maudhi ambayo mtumiaji anaweza kuayapata.

Ahsante kwa muda wako wa kusoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kujuzana mambo haya ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango,ili unapoamua kutumia utumie ukiwa na taarifa sahihi.sitasimama upande kwa kusema hazifai au zinafaa ninachofanya ni kukuelimisha, nitaelekeza kwa Lugha ya kawaida Sana pasipo kuingia mwenye sayansi ngumu ambayo kiufupi haitanufaisha watu waliowengi,nitaangazia mazingira haya yafuatayo:-

1.maana ya uzazi wa mpango
2.makundi ya njia za uzazi wa mpango za kisasa
3.Faida ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango za kisasa
4.maudhi /side effects amboyo mtumiaji wa njia hizo anaweza kuyapata

> Nini maana ya uzazi wa mpango?
-uzazi wa mpango ni uamzi wa hiari wa MTU binafsi au yeye na mwenza wake kuamua,waanze lini kuzaa,wazae watoto wangapi,hapo watoto wapishane umri gani,na lini wataacha/ataacha kuzaa.

> Kuna makundi makuu matatu ya njia za uzazi wa mpango wa kisasa
!.njia za muda mfupi

.kondomo (me au ke)
.vidonge(vyenye kichocheo kimoja(POPs)vichocheo viwili(COCs) pamoja na emergency (P2)
.Sindano
.Njia ya unyonyeshaji
Njia ya kuchomoa uume unapokaribia kufika kileleni/withdraw
.njia ya kufuata kalenda
.njia ya ute
.njia ya joto/bathal body temperature

!!.njia za muda mrefu
.kipandikizi/vipandikizi
.kitanzi/Lupu

!!!.njia za kudumu
.kufunga kizazi mwanaume/Vasectomy
.kufunga kizazi mwanamke/BTL

>Faida za uzazi wa mpango
.husadia kurudisha Afya ya mwanamke kabla ya kubeba mimba nyingine
.husaidia kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na ujauzito na uzazi
.hupunguza vifo vya watoto .Husaidia kudumisha mahusiano na mwenza wako
.husaidia kupangashughuli za maendeleo ya familia,Jamii na taifa
.husaidia kuwapunguzia wazazi gharama au majukumu ya kulea familia kubwa
.huwawezesha vijana na wanawake kufikia malengo yao ya maisha
.huwapa wanawake nafasi ya kushiriki kwenue shughuli mbalimbali za kiuchumi na maendeleo.

>Maudhi/side effects ambazo mtumiaji anaweza kuzipata
Hapa naweka kwa ujumla wake bila kuangalia ni njia ipi,maana maudhi yanatofautiana njia moja na nyingine.
.maumivu ya Kichwa
.maumivu ya tumbo hasa chini ya kitovu
.maumivu ya mgongo
.kuongezeka uzito
.kuchoka kusiko kawaida
.Mzunguko wa hedhi kabadilika,kubkeed kwa mda mrefu(menorrhagia),kupata hedhi inayoambatana na maumivu ya tumbo na kiuno(dismenorrhea),kukosa hedhi(amenorrhea)
.kizunguzungu
.kukosa hamu ya tendo LA ndoa
.kichefuchefu

Haya ni baadhi ya maudhi ambayo mtumiaji anaweza kuayapata.

Ahsante kwa muda wako wa kusoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwanamke anapokosa hedhi kwa muda mrefu sana baada ya matumizi ya P2 anapaswa kufanya nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom