Fahamu kuhusu Hayati Mzee Moi na fimbo yake maarufu kama “Fimbo ya Nyayo”

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
603
1,760
Moi.jpg

Fimbo ya Rais wa zamani wa Kenya, Hayati Daniel Toroitich Arap Moi ilijulikana sana kama ishara ya nguvu, uongozi na mshikamano wa kitaifa.

Fimbo hiyo liyotengenezwa kwa pembe za ndovu na dhahabu, ilibatizwa jina la 'Fimbo ya Nyayo'.

Wachambuzi wanasema fimbo hiyo ilikuwa ishara ya nguvu na mamlaka aliyopewa kutoka kwa jamii yake.

Huenda fimbo ikawa ni miongoni mwa fimbo zilizowahi kusafiri zaidi nchini Kenya, kwani aliibeba kila mahali alipokwenda. Mzee Moi hakuwahi kutokea katika kazi yoyote ndani na nje ya nchi bila fimbo yake. Mara baada ya kupanda jukwaani, aliitumia kupungia umati wa watu ambao waliitikia kwa shangwe.

Mzee Moi aliithamini sana fimbo hiyo kiasi kwamba wakati mmoja mnamo mwaka 1981, alikataa kuonekana kwenye hafla ya Malkia huko Australia bila fimbo yake ambayo kwa wakati huo ilikuwa imevunjika.

Akiongea katika mahojiano mnamo Agosti 22, 2018, Msaidizi wa Mzee Moi, Lee Njiru alikumbuka jinsi ambavyo fimbo mpya ilibidi isafirishwe kwenda Australia kabla ya Mkutano wa Wakuu wa Jumuiya ya Serikali huko Melbourne.

Fimbo hiyo ilivunjika huko Los Angeles, USA, ambapo Moi alikuwa amehudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa jijini New York.

Bwana Njiru alisema walilazimika kukaa Honolulu, Hawaii, kumngojea msaidizi binafsi wa Moi, Peter Rotich, kusafirisha nyingine kabla ya mkuu huyo nchi kufika mkutanoni.

"Rotich alilazimika kuwa hapo kabla Moi hajafika Australia kwani Mzee alitaka kuwasalimia watu kwa kuwapungia na fimbo hiyo, ambayo ilikuwa sawa na mkia alioutumia Rais (Jomo) Kenyatta," Njiru aliongezea.

Hadi wakati walipofika Australia, Rotich alikuwa tayari ameshawasilisha fimbo nyingine kwa Rais Moi.

"Isingewezekana Mzee Moi kujitokeza mbele ya umma bila fimbo yake," Njiru alikumbuka.

Fimbo ya Nyayo ilijitengenezea alama yake katika historia, na nyimbo za kizalendo ziliimbwa juu yake.

fimbo.jpg

Kwaya ya Kariokor Friends waliimba wimbo uitwao Fimbo ya Nyayo, wakipongeza fimbo hiyo kumsaidia Moi kuongoza nchi. Fimbo ilikuwa ni ishara ya uongozi wa Moi kuiendesha nchi katika mwelekeo sahihi.

"Wakenya, tujali utamaduni wetu na tuungane. Wacha tusonge mbele kwani tumeunganishwa na Fimbo ya Nyayo. Umoja ndio silaha kubwa dhidi ya ukabila na ugaidi, ”yalikuwa baadhi ya mashairi ya wimbo huo.

Wimbo huo pia ulimpongeza Moi kwa kuanzisha Wizara ya Sayansi na Teknolojia iliyowezesha Wakenya wawe huru na kukuza maarifa yao ya kiteknolojia.

Wimbo huo pia uliwahimiza viongozi kufuata njia ya Moi katika kuwa mfano wa kuigwa na kuongoza nchi vizuri.

Fimbo ilikuwa maarufu sana kiasi kwamba iliwekwa nyuma ya noti za Sh20 na Sh100, ambazo zilikuwa na picha ya Moi mbele.

Sanamu kubwa kwa heshima ya rais ilijengwa katika eneo la Uhuru Park kuashiria nguvu yake, uongozi na umoja wa kitaifa.

Fimbo hiyo pia inaaminika kuashiria maono ambayo Moi alikuwa nayo kwa Kenya changa miaka ya 1970 na 80.

moi's fimbo.jpg

Fimbo moi.jpg

Kenya-20.jpg

Chanzo: The Standard
 
Harambeeeeeeeee............................nyayoooooooooo
Harambeeeeeeeee............................nyayoooooooooo

Na maziwa jee?......................ya wototo wa nyayooooo
 
Mzee amefariki bila kutoa siri nani alimuua DR. Auko, Waziri wake wa mambo ya nje.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom