RESEARCHER 1
Member
- Nov 30, 2016
- 16
- 15
Kutokana na wadau wengi kutaka kujua hasa gharama za uzalishaji wa mkonge na muda gani unaaza kupata faida ikanilazimu niwaandalie hii bajeti ambayo tunaitumia kwa mkoa wa Tanga ila inaweza kubadilika kutokana na upatikanaji wa mahitaji na hali ya shamba ilivyo.
================== Ufafanuzi kutoka kwa wadau mbalimbali==============
KILIMO CHA MKONGE TANZANIA
Mkonge au Katani ni moja kati ya zao la biashara Jina la kisanyansi inaitwa Agave sisalana. Asili ya zao hili ni Mexico na baadae likasambaa katika nchi nyingine, kwa mara ya kwanza lilitambushwa katika nchi za kitropikia na subtropikia India,Tanzania, Brazil, Kenya south Africa, Angola, Mozambique Morocco Uganda, Zimbabwe na Mauritius.
Zao la mkonge liliingizwa nchini mwaka 1892 na mtaalamu wa kijerumani Dr. Richard Hindorff ambaye alikuwa ni mtafiti wa mimea na udongo. Mtaalamu huyo alichukua miche 1000 kutoka Pwani ya Mexico kwenye jimbo la Yuctan na kuisafisha kwa kupitia Frolida, Marekani na Humburg Ujerumani. Kati ya miche 1000, ni miche 62 tu ndiyo iliyofika Tanganyika na ilipandwa sehemu iitwayo Kikokwe huko Pangani Tanga.
Mkonge ulisambaa maeneo mengi ya Tanganyika mpaka kufikia mwanzoni mwa miaka 1960 Tanganyika ilikuwa inaongoza kwa uzalishaji wa mkonge ikifatiwa na Brazil na mexico kwa mauzo ya tani 230,000 kwa mwaka nje ya nchi. Kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza miaka ya 1970 uzalishaji ulipungua toka tani 230,000 hadi tani 19,700 kwa mwaka 1997.
Hata ivyo mageuzi ya kiuchumi yaliyoanza miaka 1980 ambayo yalilenga katika ubinafisishaji na biashara huria , uhuru wa taasisi za kifedha za ndani na nje ya nchi yalifufua kilimo cha mkonge na hasa kukamilika kwa ubinafishaji mwaka 2005 uzalishaji umepanda hadi kufikia tani 40,000 mwaka 2015 hii inatokana na kuongezeka kwa mahitaji ya mkonge na bidhaa zake pamoja na kupanda bei kwenye soko la dunia pamoja na ndani.
Soko kuu la mkonge wa Tanzania ni china, Saudi Arabia , India, Uhispania, Ujerumani, Uingereza, Kenya, Uganda na Nigeria.
ZAO LA MKONGE
Kutokana na mabadiliko makubwa ya hali ya hewa kwa sasa wakulima wengi wamekuwa wakikosa mavuno kutokana na kutegemea mvua ambazo kwa sasa mtiririko wake siyo mzuri ivyo wataafiti wa mkonge wanahamasisha kilimo cha mkonge kwa wakulima wadogo nchi nzima ili zao litumike katika kuwaongezea wananchi kipato kutokana na sifa za mkonge kama zifuatazo;
- Zao la mkonge linavumilia sana ukame
- Ni zao ambalo halina msimu maalumu wa kupanda hivyo kupelekea kuweza kupandwa wakati wowote na pia halina wakati maalumu wa kuvunwa pale linapokuwa tayari kuvunwa
- Zao la mkonge linaweza kuchanganywa na mazao mengine ya msimu kama kunde, mahindi, maharage , alizeti, njegere na karanga.
- Ni zao ambalo halina uhaba wa vipando.
- Bidhaa zitokanazo na mkonge zinaweza kutumika katika tasnia ya kilimo, nishati, ujenzi, famasia, magari, meli, majumbani,ofisini na mazingira
- Mmea wa mkonge unaweza kuishi kwa kipindi cha miaka 10-25 hivyo kumuhakikishia mkulima kipato cha uhakika
- Mkonge ni zao linalo staimil magonjwa, wadudu na maguu na hata upungufu wa rutuba kwenye udongo.
UZALISHAJI WA MKONGE
Mambo yafuatayo ni yakuzingatia katika uzalishaji wa mkonge;
- Maandalizi ya miche bora ya mkonge
- Utunzaji wa vitalu vya mkonge
- Upandaji wa mkonge shambani
- Utunzaji wa mkonge shambani
- Kilimo mseto cha mkonge na mazao mengine yachakula
i) MAANDALIZI YA VITALU VYA MKONGE
Uchaguzi sahihi wa miche ya mkonge na maadalizi ya mazuri ya kitalu kwa ajili ya upandaji wa miche ya mkonge ni muhimu kwa ukuaji haraka na hatimaye utoaji wa mavuno bora na mengi ya zao la mkonge.
Kuna aina nne ya vipando vya mkonge;
• Vikonyo (bulbils) huota kwenye mlingoti baada ya maua ya mkonge kupukutika
• Machipukizi (suckers) huchipua kutoka kwenye mmea wa mkonge
• Miche inayozalishwe ndani ya maabara kwa njia ya tissue culture (mtc lab)
• Miche inayotokana na mizizi au tumba za mkonge huitwa rhizomes japo aina hii ya miche sasa hivi haitumiki sana hapa nchini.
II) UTUNZAJI WA VITALU VYA MKONGE
• Palizi – upaliliaji kwa jembe la mkono kwa kawaida palizi linaweza kufanyika mara 4-8 kutegemea na udongo.
- Upaliliaji kwa kutumia dawa za magugu mfano hy-varax hutumika sana kuzuia magugu katika bustani za mkonge huzuia uotaji wa magugu kwa muda wa miezi sita mfululizo ambayo utumika kwa kiasi cha kilo 4.5/ha nah ii dawa inashauriwa inyunyiziwe bustanini wakati udongo una unyevunyevu.
• Namna ya kurutubisha vitalu
- Taka za mkonge ( sisal waste)
- Mbolea ya chunvichunvi zenye kirutubisho cha nitrogen 30kg /ha kama CAN, SA, and UREA kwa kukuzia
- Mbolea aina ya potash kama MOP na DAP
- Wadudu na magonjwa ya mkonge kama tembo wa mkonge ( sisal weevil) na scale na magonjwa kama kuoza kwa mashina (bole rot) , ugonjwa wa pundamilia (zebra leaf rot) na ugonjwa wa mabaka kwenye majani (korogwe leaf sport)
iii) UPANDAJI WA MKONGE SHAMBANI
• Uchaguzi na upandaji wa miche ya kupanda (grading) ukubwa wa miche ya kupanda ni bora iwe na urefu kati ya sentimita 50 -70 na uzito kati ya kilo 2-4 miche ipangwe katika madaraja kufuatana na ukubwa
- Uchimbaji wa miche huchimbwa kwa kutumia jembe au sululu ili kitunguu (bole) kisikatwe ili kuepusha kushambuliwa na wadudu.
- Kutayarisha miche kwa kukata mizizi bila kuaribu shina na majani yaliyonyauka yaondolewe
- Upandaji wa kutumia machipukizi (suckers) ikusanywe kutoka katika mashamba yenye mkonge mdogo si zaidi ya mikato 2
- Kuligawa shamba katika maboma kwa ajili ya kupanda mkonge shambani
• Mifumo ya kupanda mkonge shambani
- Mstari mmoja (single row) kwa nafasi ya 3.5 x 0.75 mita
- Upandaji wa mistari miwili (double row ) upandaji huu miraba miwili huwekwa karibu ili kutoa nafasi pana kati ya miraba hiyo. Nafasi ya upandaji utegemea aina ya mkonge
iv) UTUNZAJI WA MKONGE SHAMBANI
Ili kupata mavuno mengi ni vyema kuzingatia yafuatayo
- Matumizi ya taka za mkonge (sisal waste) ili kuifadhi unyevunyevu na kurutubisha udongo.
- Matumizi ya chokaa (agriculture lime) ili kuongeza chachu pH mpaka 5.5-5.8 inayotakiwa na mkonge.
- Kuweka mbolea za chunvichunvi zenye kirutubisha cha nitrogeni mfano CAN UREA, potasiam na phosphorus kama MOP, TSP NA DAP.
- Udhibiti wa magugu ili kuepusha kutumia maji na virutubisho vinavyotakiwa kutumiwa na mmea. Kwakutumia njia zifuatazo;- kutumia jembe au nyengo, kutumia madawa mfano bromacil, kutumia jamii ya mikunde (cover crop) mfano tropical kudzu.
v) KILIMO MSETO CHA MKONGE NA MAZAO MENGINE YA CHAKULA
Eneo linalotumiwa kwa mkonge ni asilimia 60 na kiasi kilichosalia asilimia 40 hubaki tupu ivyo ni bora Kulima na mazao mengine faida za Kilimo mseto
- Kutumia ardhi kwa ufanisi
- Kuzalisha mazao Zaidi ya moja katika eneo hilo na kwa Gharama ndogo.
- Kwa kupanda mazao jamii ya kunde husaidia kuongeza rutuba ya udongo.
- Kupata Chakula hasa kwa wakulima wadogo na kwa mazao yanayofunika ardhi na kupunguza mmomonyoko wa ardhi kwa njia ya upepo na maji.
• Mazao yanayofaa kuchanganywa na mkonge maharage, kunde, karanga, soya, choroko alizeti, ufuta, mahindi nk
• Mazao yasiyofaa kuchanganywa na mkonge ni mazao ya kudumu kama migomba, minazi, mikorosho na michungwa mtama uwele viazi vitamu na mihogo
2. UVUNAJI WA MKONGE
i) Ukataji wa mkonge ili kupata singe mkonge uvunwa majani kwa kuzingatia yafuatayo
- Jani linalovunwa ni lazima liwe na urefu unaozidi sentimeta 90
- Ni lazima jani liwe na mwanguko usiozidi digrii 45%
- Ni lazima likatwe kwenye shingo yake
- Ni marufuku kukata kitunguu au mape
ii) Usombaji wa majani yaliyokatwa
iii) Usindikaji
iv) Kulainisha singa (brushing)
v) Kufunga mizingo kwenye press (pressing machine)
vi) Kupanga madaraja ya singa (grading) kwa kuangalia urefu wa singa narangi ya singa
Tanzania ni miongoni mwa zenye hali ya hewa na mazingira bora, kwa uzalishaji wa mkonge ambao ni zao la biashara.
Kwa wastani, mkonge unaweza kuishi wastani wa kati ya miaka 13 hadi 14, majani yake yanaweza kufikia urefu wa futi 200 hadi 300 hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile kamba nene, magunia, heleni na mazuria.
Kadri miaka inavyosonga mbele, ndivyo zao hilo linakuwa linavyozidi kuongezeka thamani, kutokana na mahitaji yake kuongezeka kadri siku zinavyoongezeka, kulingana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Linazidi kuwa na thamani katika soko la kimataifa. Historia ya nchi inaonyesha kuwa mkonge umekuwa ukimwa kwa sehemu kubwa ta mikoa ya Morogoro na Tanga.
Wakati bado haijatoweka kabisa katika mikoa hiyo miwili, imeanza kuibuka tena kwa kasi katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, ambako kuna kilimo kilichopamba moto.
Kasi yake imefika hatua ya kuchukua sura ya kuchuana na pamba inayolimwa kwa wingi huko kama zao la biashara.
KUTOKA KWA WAKULIMA
Suzan Jinyange (53), ni mkulima wa katani na msindikaji wa zao hilo kutoka wilayani Kishapu.
Anasema mkonge umewaongezea mafanikio wakulima wilayani humo na anatoa mfano binafsi kwamba akiwa mama aliyeolewa na mwenye watoto sita, amejikita katika kilimo hicho tangu mwaka 2013.
“Nilikuwa nalima mazao ya kawaida, lakini nilipoanza kulima zao la mkonge na kusindika, nimepata mafanikio makubwa,” anasema.
Jinyange anasema kuwa amepanda robo tatu ya ekari za zao hilo na ananunua mkonge kwa wakulima wengine kiasi cha ekari mbili kwa ajili ya kusindika.
Anasema kwa mwaka ana uwezo wa kusindika tani 10 anazoziuza kwa kampuni za mkonge na bei yake kwa kilo ni kati ya Sh. 800 hadi Sh. 1,000 na uliosindikwa unafikia bei zaidi ya Sh. 1,200 hadi Sh. 1,300.
“Nalishukuru shirika la Oxfam kupitia miradi yao, kwani limetupatia elimu juu ya zao hili, kwa sababu ardhi yetu ni kame mno. Tulikuwa tunapata hasara na kujikuta maendeleo ya kiuchumi yanarudi nyuma kila siku,” anasema.
Mkulima huyo anasema utaratibu wa sasa, wanapopanda mikonge kati eneo la kati, huchanganya na mazao mengine kama vile mahindi, choroko na karanga. Jinyange anasema shirika hilo kupitia wataalamu wake, imembadilisha maisha kwa kumpatia mashine ya kusindika mkonge na elimu kuhusu kilimo hicho.
“Nimefanikiwa kununua mashamba, kusomesha watoto pamoja na kumuuguza mtoto wangu anayesumbuliwa na saratani ya mguu. “Nilikuwa sina meno yaling’oka, ila nilipata fedha za kununua meno bandia. Pia nimewaajiri vijana ambao wananisaidia shughuli zangu za kusindika mkonge,” anasema Jinyange.
Mshauri wa Mradi wa Mnyororo wa Zao la Mkonge kutoka shirika la Oxfam, Azimio Mbegu, anasema wamefanya uchambuzi wa chanzo cha mabadiliko ya tabianchi na zao la biashara litakalohimili hali hiyo.
Wakulima kwa kushirikiana na shirika hilo, wamekubaliana zao pekee linalohimili ukame ni mkonge, kwani halishambuliwi na magonjwa.
Kaimu Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wilayani Kishapu,Godwin Evarist, anasema Oxfam lilianza kazi katika wilaya hiyo mwaka 2009. Anasema ilianza shughuli zake katika vijiji 10 na baadaye ikavifikia vijiji 30, kwa lengo la kuelimisha jamii matumizi ya mkonge.
Evarist anasema mwanzoni walitumia mmea wa mkonge kuweka mpaka baina ya mashamba na sasa imepiga hatua na kuwa na hadhi ya zao la biashara. Hivi sasa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, imehamasika na imelichukua kuwa sehemu ya uchumi wa wilaya.
MIKAKATI YA MABORESHO
Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17, Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu imeingiza mkonge kwenye mpango mkakati wake, ikiwa ni hanzo cha ndani na imetenga bajeti ya Sh. milioni 200 kwa ajili ya kuendeleza zao hilo.
Kiasi hicho cha fedha kimedhamiriwa kuviwezesha vikundi vya kinamama kupata pembejeo na mitaji ya kuendeleza biashara zao. Changamoto inayotajwa kuwapo ni ubaba wa miche ya m ikonge na hivyo, imeanzishwa kitalu chenye miche 25 ya zao hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Hawa Ng’umbi anasema wilaya itahakikisha zao hilo linapewa kipaumbele, baada ya wakulima kubaini umuhimu wake katika kuwaongezea kipato.
Hawa anasema kupitia mikutano ya hadhara, wamekuwa wakihamasisha kulima mazao mengine, bila ya kusahau mkonge kwa kuwa linastahimili ukame.
“Kampeni ya uhamasishaji imeanza katika shule, kaya na kata kupanda mikonge ekari mbili. Lakini nilishukuru shirika la Oxfam, kwa kutoa elimu kwa wakulima ambao hivi sasa wamepata mafanikio ,”anasema.
================== Ufafanuzi kutoka kwa wadau mbalimbali==============
KILIMO CHA MKONGE TANZANIA
Mkonge au Katani ni moja kati ya zao la biashara Jina la kisanyansi inaitwa Agave sisalana. Asili ya zao hili ni Mexico na baadae likasambaa katika nchi nyingine, kwa mara ya kwanza lilitambushwa katika nchi za kitropikia na subtropikia India,Tanzania, Brazil, Kenya south Africa, Angola, Mozambique Morocco Uganda, Zimbabwe na Mauritius.
Zao la mkonge liliingizwa nchini mwaka 1892 na mtaalamu wa kijerumani Dr. Richard Hindorff ambaye alikuwa ni mtafiti wa mimea na udongo. Mtaalamu huyo alichukua miche 1000 kutoka Pwani ya Mexico kwenye jimbo la Yuctan na kuisafisha kwa kupitia Frolida, Marekani na Humburg Ujerumani. Kati ya miche 1000, ni miche 62 tu ndiyo iliyofika Tanganyika na ilipandwa sehemu iitwayo Kikokwe huko Pangani Tanga.
Mkonge ulisambaa maeneo mengi ya Tanganyika mpaka kufikia mwanzoni mwa miaka 1960 Tanganyika ilikuwa inaongoza kwa uzalishaji wa mkonge ikifatiwa na Brazil na mexico kwa mauzo ya tani 230,000 kwa mwaka nje ya nchi. Kutokana na sababu mbalimbali zilizojitokeza miaka ya 1970 uzalishaji ulipungua toka tani 230,000 hadi tani 19,700 kwa mwaka 1997.
Hata ivyo mageuzi ya kiuchumi yaliyoanza miaka 1980 ambayo yalilenga katika ubinafisishaji na biashara huria , uhuru wa taasisi za kifedha za ndani na nje ya nchi yalifufua kilimo cha mkonge na hasa kukamilika kwa ubinafishaji mwaka 2005 uzalishaji umepanda hadi kufikia tani 40,000 mwaka 2015 hii inatokana na kuongezeka kwa mahitaji ya mkonge na bidhaa zake pamoja na kupanda bei kwenye soko la dunia pamoja na ndani.
Soko kuu la mkonge wa Tanzania ni china, Saudi Arabia , India, Uhispania, Ujerumani, Uingereza, Kenya, Uganda na Nigeria.
ZAO LA MKONGE
Kutokana na mabadiliko makubwa ya hali ya hewa kwa sasa wakulima wengi wamekuwa wakikosa mavuno kutokana na kutegemea mvua ambazo kwa sasa mtiririko wake siyo mzuri ivyo wataafiti wa mkonge wanahamasisha kilimo cha mkonge kwa wakulima wadogo nchi nzima ili zao litumike katika kuwaongezea wananchi kipato kutokana na sifa za mkonge kama zifuatazo;
- Zao la mkonge linavumilia sana ukame
- Ni zao ambalo halina msimu maalumu wa kupanda hivyo kupelekea kuweza kupandwa wakati wowote na pia halina wakati maalumu wa kuvunwa pale linapokuwa tayari kuvunwa
- Zao la mkonge linaweza kuchanganywa na mazao mengine ya msimu kama kunde, mahindi, maharage , alizeti, njegere na karanga.
- Ni zao ambalo halina uhaba wa vipando.
- Bidhaa zitokanazo na mkonge zinaweza kutumika katika tasnia ya kilimo, nishati, ujenzi, famasia, magari, meli, majumbani,ofisini na mazingira
- Mmea wa mkonge unaweza kuishi kwa kipindi cha miaka 10-25 hivyo kumuhakikishia mkulima kipato cha uhakika
- Mkonge ni zao linalo staimil magonjwa, wadudu na maguu na hata upungufu wa rutuba kwenye udongo.
UZALISHAJI WA MKONGE
Mambo yafuatayo ni yakuzingatia katika uzalishaji wa mkonge;
- Maandalizi ya miche bora ya mkonge
- Utunzaji wa vitalu vya mkonge
- Upandaji wa mkonge shambani
- Utunzaji wa mkonge shambani
- Kilimo mseto cha mkonge na mazao mengine yachakula
i) MAANDALIZI YA VITALU VYA MKONGE
Uchaguzi sahihi wa miche ya mkonge na maadalizi ya mazuri ya kitalu kwa ajili ya upandaji wa miche ya mkonge ni muhimu kwa ukuaji haraka na hatimaye utoaji wa mavuno bora na mengi ya zao la mkonge.
Kuna aina nne ya vipando vya mkonge;
• Vikonyo (bulbils) huota kwenye mlingoti baada ya maua ya mkonge kupukutika
• Machipukizi (suckers) huchipua kutoka kwenye mmea wa mkonge
• Miche inayozalishwe ndani ya maabara kwa njia ya tissue culture (mtc lab)
• Miche inayotokana na mizizi au tumba za mkonge huitwa rhizomes japo aina hii ya miche sasa hivi haitumiki sana hapa nchini.
II) UTUNZAJI WA VITALU VYA MKONGE
• Palizi – upaliliaji kwa jembe la mkono kwa kawaida palizi linaweza kufanyika mara 4-8 kutegemea na udongo.
- Upaliliaji kwa kutumia dawa za magugu mfano hy-varax hutumika sana kuzuia magugu katika bustani za mkonge huzuia uotaji wa magugu kwa muda wa miezi sita mfululizo ambayo utumika kwa kiasi cha kilo 4.5/ha nah ii dawa inashauriwa inyunyiziwe bustanini wakati udongo una unyevunyevu.
• Namna ya kurutubisha vitalu
- Taka za mkonge ( sisal waste)
- Mbolea ya chunvichunvi zenye kirutubisho cha nitrogen 30kg /ha kama CAN, SA, and UREA kwa kukuzia
- Mbolea aina ya potash kama MOP na DAP
- Wadudu na magonjwa ya mkonge kama tembo wa mkonge ( sisal weevil) na scale na magonjwa kama kuoza kwa mashina (bole rot) , ugonjwa wa pundamilia (zebra leaf rot) na ugonjwa wa mabaka kwenye majani (korogwe leaf sport)
iii) UPANDAJI WA MKONGE SHAMBANI
• Uchaguzi na upandaji wa miche ya kupanda (grading) ukubwa wa miche ya kupanda ni bora iwe na urefu kati ya sentimita 50 -70 na uzito kati ya kilo 2-4 miche ipangwe katika madaraja kufuatana na ukubwa
- Uchimbaji wa miche huchimbwa kwa kutumia jembe au sululu ili kitunguu (bole) kisikatwe ili kuepusha kushambuliwa na wadudu.
- Kutayarisha miche kwa kukata mizizi bila kuaribu shina na majani yaliyonyauka yaondolewe
- Upandaji wa kutumia machipukizi (suckers) ikusanywe kutoka katika mashamba yenye mkonge mdogo si zaidi ya mikato 2
- Kuligawa shamba katika maboma kwa ajili ya kupanda mkonge shambani
• Mifumo ya kupanda mkonge shambani
- Mstari mmoja (single row) kwa nafasi ya 3.5 x 0.75 mita
- Upandaji wa mistari miwili (double row ) upandaji huu miraba miwili huwekwa karibu ili kutoa nafasi pana kati ya miraba hiyo. Nafasi ya upandaji utegemea aina ya mkonge
- Mkonge aina ya sisalana nafasi pana ni mita 3.5 na nafasi kati ya mistari miwili iliyo karibu ni mita 1 wakati nafasi kati ya mmea mmoja na mwingine ni setimita 90 (3.5 +1 x 0.9) mita. Hutoa mimea 5,000 kwa hekta.
- Mkonge chotara (H.11648) nafasi pana ni mita 4 na nafasi kati ya mistari iliyo karibu ni 1 pia nafasi kati ya mmea mmoja na mwingine ni mita 1 (4 +1 x 1) mita. Upandaji huu utoa mimea 4,000 kwa hekta.
iv) UTUNZAJI WA MKONGE SHAMBANI
Ili kupata mavuno mengi ni vyema kuzingatia yafuatayo
- Matumizi ya taka za mkonge (sisal waste) ili kuifadhi unyevunyevu na kurutubisha udongo.
- Matumizi ya chokaa (agriculture lime) ili kuongeza chachu pH mpaka 5.5-5.8 inayotakiwa na mkonge.
- Kuweka mbolea za chunvichunvi zenye kirutubisha cha nitrogeni mfano CAN UREA, potasiam na phosphorus kama MOP, TSP NA DAP.
- Udhibiti wa magugu ili kuepusha kutumia maji na virutubisho vinavyotakiwa kutumiwa na mmea. Kwakutumia njia zifuatazo;- kutumia jembe au nyengo, kutumia madawa mfano bromacil, kutumia jamii ya mikunde (cover crop) mfano tropical kudzu.
v) KILIMO MSETO CHA MKONGE NA MAZAO MENGINE YA CHAKULA
Eneo linalotumiwa kwa mkonge ni asilimia 60 na kiasi kilichosalia asilimia 40 hubaki tupu ivyo ni bora Kulima na mazao mengine faida za Kilimo mseto
- Kutumia ardhi kwa ufanisi
- Kuzalisha mazao Zaidi ya moja katika eneo hilo na kwa Gharama ndogo.
- Kwa kupanda mazao jamii ya kunde husaidia kuongeza rutuba ya udongo.
- Kupata Chakula hasa kwa wakulima wadogo na kwa mazao yanayofunika ardhi na kupunguza mmomonyoko wa ardhi kwa njia ya upepo na maji.
• Mazao yanayofaa kuchanganywa na mkonge maharage, kunde, karanga, soya, choroko alizeti, ufuta, mahindi nk
• Mazao yasiyofaa kuchanganywa na mkonge ni mazao ya kudumu kama migomba, minazi, mikorosho na michungwa mtama uwele viazi vitamu na mihogo
2. UVUNAJI WA MKONGE
i) Ukataji wa mkonge ili kupata singe mkonge uvunwa majani kwa kuzingatia yafuatayo
- Jani linalovunwa ni lazima liwe na urefu unaozidi sentimeta 90
- Ni lazima jani liwe na mwanguko usiozidi digrii 45%
- Ni lazima likatwe kwenye shingo yake
- Ni marufuku kukata kitunguu au mape
ii) Usombaji wa majani yaliyokatwa
iii) Usindikaji
iv) Kulainisha singa (brushing)
v) Kufunga mizingo kwenye press (pressing machine)
vi) Kupanga madaraja ya singa (grading) kwa kuangalia urefu wa singa narangi ya singa
==================Shukrani ka muandaaji MR. MBARAKA BATARE, MTAFITI WA MKONGE, ARI-MLINGANO TANGA TANZANI
Tanzania ni miongoni mwa zenye hali ya hewa na mazingira bora, kwa uzalishaji wa mkonge ambao ni zao la biashara.
Kwa wastani, mkonge unaweza kuishi wastani wa kati ya miaka 13 hadi 14, majani yake yanaweza kufikia urefu wa futi 200 hadi 300 hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile kamba nene, magunia, heleni na mazuria.
Kadri miaka inavyosonga mbele, ndivyo zao hilo linakuwa linavyozidi kuongezeka thamani, kutokana na mahitaji yake kuongezeka kadri siku zinavyoongezeka, kulingana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Linazidi kuwa na thamani katika soko la kimataifa. Historia ya nchi inaonyesha kuwa mkonge umekuwa ukimwa kwa sehemu kubwa ta mikoa ya Morogoro na Tanga.
Wakati bado haijatoweka kabisa katika mikoa hiyo miwili, imeanza kuibuka tena kwa kasi katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, ambako kuna kilimo kilichopamba moto.
Kasi yake imefika hatua ya kuchukua sura ya kuchuana na pamba inayolimwa kwa wingi huko kama zao la biashara.
KUTOKA KWA WAKULIMA
Suzan Jinyange (53), ni mkulima wa katani na msindikaji wa zao hilo kutoka wilayani Kishapu.
Anasema mkonge umewaongezea mafanikio wakulima wilayani humo na anatoa mfano binafsi kwamba akiwa mama aliyeolewa na mwenye watoto sita, amejikita katika kilimo hicho tangu mwaka 2013.
“Nilikuwa nalima mazao ya kawaida, lakini nilipoanza kulima zao la mkonge na kusindika, nimepata mafanikio makubwa,” anasema.
Jinyange anasema kuwa amepanda robo tatu ya ekari za zao hilo na ananunua mkonge kwa wakulima wengine kiasi cha ekari mbili kwa ajili ya kusindika.
Anasema kwa mwaka ana uwezo wa kusindika tani 10 anazoziuza kwa kampuni za mkonge na bei yake kwa kilo ni kati ya Sh. 800 hadi Sh. 1,000 na uliosindikwa unafikia bei zaidi ya Sh. 1,200 hadi Sh. 1,300.
“Nalishukuru shirika la Oxfam kupitia miradi yao, kwani limetupatia elimu juu ya zao hili, kwa sababu ardhi yetu ni kame mno. Tulikuwa tunapata hasara na kujikuta maendeleo ya kiuchumi yanarudi nyuma kila siku,” anasema.
Mkulima huyo anasema utaratibu wa sasa, wanapopanda mikonge kati eneo la kati, huchanganya na mazao mengine kama vile mahindi, choroko na karanga. Jinyange anasema shirika hilo kupitia wataalamu wake, imembadilisha maisha kwa kumpatia mashine ya kusindika mkonge na elimu kuhusu kilimo hicho.
“Nimefanikiwa kununua mashamba, kusomesha watoto pamoja na kumuuguza mtoto wangu anayesumbuliwa na saratani ya mguu. “Nilikuwa sina meno yaling’oka, ila nilipata fedha za kununua meno bandia. Pia nimewaajiri vijana ambao wananisaidia shughuli zangu za kusindika mkonge,” anasema Jinyange.
Mshauri wa Mradi wa Mnyororo wa Zao la Mkonge kutoka shirika la Oxfam, Azimio Mbegu, anasema wamefanya uchambuzi wa chanzo cha mabadiliko ya tabianchi na zao la biashara litakalohimili hali hiyo.
Wakulima kwa kushirikiana na shirika hilo, wamekubaliana zao pekee linalohimili ukame ni mkonge, kwani halishambuliwi na magonjwa.
Kaimu Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wilayani Kishapu,Godwin Evarist, anasema Oxfam lilianza kazi katika wilaya hiyo mwaka 2009. Anasema ilianza shughuli zake katika vijiji 10 na baadaye ikavifikia vijiji 30, kwa lengo la kuelimisha jamii matumizi ya mkonge.
Evarist anasema mwanzoni walitumia mmea wa mkonge kuweka mpaka baina ya mashamba na sasa imepiga hatua na kuwa na hadhi ya zao la biashara. Hivi sasa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, imehamasika na imelichukua kuwa sehemu ya uchumi wa wilaya.
MIKAKATI YA MABORESHO
Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/17, Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu imeingiza mkonge kwenye mpango mkakati wake, ikiwa ni hanzo cha ndani na imetenga bajeti ya Sh. milioni 200 kwa ajili ya kuendeleza zao hilo.
Kiasi hicho cha fedha kimedhamiriwa kuviwezesha vikundi vya kinamama kupata pembejeo na mitaji ya kuendeleza biashara zao. Changamoto inayotajwa kuwapo ni ubaba wa miche ya m ikonge na hivyo, imeanzishwa kitalu chenye miche 25 ya zao hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Hawa Ng’umbi anasema wilaya itahakikisha zao hilo linapewa kipaumbele, baada ya wakulima kubaini umuhimu wake katika kuwaongezea kipato.
Hawa anasema kupitia mikutano ya hadhara, wamekuwa wakihamasisha kulima mazao mengine, bila ya kusahau mkonge kwa kuwa linastahimili ukame.
“Kampeni ya uhamasishaji imeanza katika shule, kaya na kata kupanda mikonge ekari mbili. Lakini nilishukuru shirika la Oxfam, kwa kutoa elimu kwa wakulima ambao hivi sasa wamepata mafanikio ,”anasema.