Huo usaidizi ama kwa kitaalamu 'Supportive care' unafanyika kwa wagonjwa wenye dalili za COVID-19 na hujumuisha mambo yafuatayo;

1. Uongezwaji wa maji ndani ya mwili ili kukabiliana na upungufu wa maji mwilini.

2. Usaidizi wa kupumua kwa kutumia vifaa maalumu (oksijeni).

3. Usaidizi katika viungo ama ogani za mwili (vital organs) zenye dalili za kushindwa kufanya kazi; mapafu, figo, ini, moyo n.k. kwa kutumia vifaa maalumu vya kitabibu.

4. Mchanganyiko wa dawa mbalimbali ili kutibu hizo dalili. Dawa zinazotumika ni zile zitumikazo kutibu maradhi mengine kama vile Ebola n.k.

Kinachotibiwa ni dalili tu ila kirusi kinaendelea kuwepo ndani ya mwili maana bado hakuna dawa ya kuweza kukiangamiza kabisa isipokuwa ni uwezo wa mwili wa mgonjwa kuweza kuvithibiti virusi hivyo ili visishambulie mwili na kuleta tena dalili.

Pia, kuna wanaopona dalili hizo lakini kwa mujibu wa tafiti zilizopo, wanaweza kubakia na matatizo mengine ya kudumu katika mifumo yao ya mwili ama ogani zao kutokana na madhara yaliyosababishwa na virusi hivyo isitoshe pia kuna visa vya watu kuambukizwa tena ama kwa mara nyingine.

Bado utafiti zaidi unaendelea kuhusiana na kirusi hiki pamoja na tabia zake maana kuna mambo mengi yahusuyo kirusi hiki bado hayajafahamika kitaalamu.
Asante sana mkuu. Nimeshiba sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chinese foreign ministry spokesman tweets claim US military brought coronavirus to Wuhan
 

Attachments

  • Screenshot_20200314-184301.png
    Screenshot_20200314-184301.png
    55.3 KB · Views: 1
Sources nyingi zilisema mwanzo china anadanganya data maana wakazi na report ya serikali zilikuwa haziendani, na kimahesabu wakasema kutokana na serikali ya china kuwa ya kicomunist, basi lazima wapike data
Ila wakasema italy na nchi nyingi za kidemokrasia hawanaga kupika data kutokana na ukweli na uwazi
Kwa kigezo kipi mkuu? Tupe Madini brother

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moja kwa moja kwenye mada:

Majirani zetu Kenya, Rwanda na DRC tayari wamesha ripoti kuwapo kwa wagonjwa wa corona katika nchi zao. Kwa hali hii ni wazi kuwa hapa kwetu ni suala la muda tu sasa.

Wenzetu, katika nchi nyingi kutegemeana na ukubwa wa tatizo wame kuwa wakichukua hatua kadhaa katika kusaidia udhibiti wa ugonjwa huu. Baadhi ya hatua zilizoishachukuliwa ni:

1. Kuwekwa quarantine kwa wageni wote toke nchi zenye kufahamika kuwa wagonjwa kwa takribani siku 14 kabla ya kuruhusiwa kuingia katika nchi nyingine.

2. Ndege za moja kwa moja tokea nchi zenye wagonjwa zimesitishwa kuelekea nchi zingine.

3. Mikusanyiko ya watu: kwenye mashindano ya mpira, matamasha, makanisani, misikitini nk imesimamishwa.

4. Taratibu za mambo ya kodi kwa wananchi zimecheleweshwa kuwapa wananchi ahueni kwenye kujikimu kuhusiana na mdororo wa uchumi kwani takribani shughuli zote za uzalishaji mali zimesita.

5. Sehemu za wazi kwa ajili kunawa kujiweka salama zimewekwa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu.

6. Namba za simu za kupiga mtu anapojishuku kuwa na dalili za ugonjwa zimewekwa wazi.

7. Nk

Hapa kwetu ninaamini pamoja na #4 serikali ingepanga kusimamisha kwanza shughuli zote za miradii mikubwa hasa ya SGR na Stigglers Gorge.

Hatua hii itatupa nafasi kutambua udharura uliopo kuhusiana na ugonjwa huu.

Tuachane na makesi kesi, chuki na magomvi yasiyokuwa na vichwa wala miguu.

Ni heri tukawa hai bila ya SGR au stigglers gorge kuliko kuwa navyo hali tumeangamia sote na Corona.

Nawasilisha.
 
China kapika data kwa ajili ya biashara. Akasahau ugonjwa umeenea dunia nzima. Alitaka aendelee uza ila sasa hawezi
Sources nyingi zilisema mwanzo china anadanganya data maana wakazi na report ya serikali zilikuwa haziendani, na kimahesabu wakasema kutokana na serikali ya china kuwa ya kicomunist, basi lazima wapike data
Ila wakasema italy na nchi nyingi za kidemokrasia hawanaga kupika data kutokana na ukweli na uwazi

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi yule kiongozi wa Iran aliyesema kuwa atajiuzuru kama vifo kutokana na Corona vitafika 25(sijui nipo sahihi).Je,amejiuzuru?
 
Huo usaidizi ama kwa kitaalamu 'Supportive care' unafanyika kwa wagonjwa wenye dalili za COVID-19 na hujumuisha mambo yafuatayo;

1. Uongezwaji wa maji ndani ya mwili ili kukabiliana na upungufu wa maji mwilini.

2. Usaidizi wa kupumua kwa kutumia vifaa maalumu (oksijeni).

3. Usaidizi katika viungo ama ogani za mwili (vital organs) zenye dalili za kushindwa kufanya kazi; mapafu, figo, ini, moyo n.k. kwa kutumia vifaa maalumu vya kitabibu.

4. Mchanganyiko wa dawa mbalimbali ili kutibu hizo dalili. Dawa zinazotumika ni zile zitumikazo kutibu maradhi mengine kama vile Ebola n.k.

Kinachotibiwa ni dalili tu ila kirusi kinaendelea kuwepo ndani ya mwili maana bado hakuna dawa ya kuweza kukiangamiza kabisa isipokuwa ni uwezo wa mwili wa mgonjwa kuweza kuvithibiti virusi hivyo ili visishambulie mwili na kuleta tena dalili.

Pia, kuna wanaopona dalili hizo lakini kwa mujibu wa tafiti zilizopo, wanaweza kubakia na matatizo mengine ya kudumu katika mifumo yao ya mwili ama ogani zao kutokana na madhara yaliyosababishwa na virusi hivyo isitoshe pia kuna visa vya watu kuambukizwa tena ama kwa mara nyingine.

Bado utafiti zaidi unaendelea kuhusiana na kirusi hiki pamoja na tabia zake maana kuna mambo mengi yahusuyo kirusi hiki bado hayajafahamika kitaalamu.
Asante kwa taarifa mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UPDATE: Uingereza

Visa vipya 342 pamoja na vifo vipya 10 vimeripotiwa.

Ongezeko hilo linaifanya Uingereza kufikisha jumla ya visa 1,140 hadi sasa vikiwemo vifo 21 nchi nzima.

Mpaka kufikia sasa, wagonjwa 18 wamekwisha tibiwa na kupata ahueni huku wengine 20 wakiwa katika hali mbaya zaidi.
 
NEWS ALERT: Wife of Spain's prime minister confirmed to have coronavirus

Begona Gomez, the wife of Spanish Prime Minister Pedro Sanchez, was diagnosed with coronavirus shortly after her husband announced sweeping new measures designed to keep people off the streets and contain the spread of the virus. [Al Jazeera]
 
NEWS ALERT: US president tests NEGATIVE for coronavirus

US President Donald Trump was tested for the coronavirus and the result was negative. [White House]

1584259249250.png
 
UPDATE: Kamisheni ya afya ya China imeripoti visa vipya 20 sanjari na vifo vipya 10 nchini humo.

Visa vinne (4) pamoja na vifo vyote 10 ni kutokea Hubei pekee.

Mpaka sasa, idadi kamili ya visa vyote nchi nzima ni 80,844 vikiwemo vifo 3,199.

Waliotibiwa na kupata ahueni wafikia 66,911 huku wengine 3,226 wangali wakiwa katika hali mbaya zaidi.
 
UPDATE: Korea Kusini

Visa vipya 76 pamoja na vifo vipya vitatu (3) vimeripotiwa nchini humo.

Mpaka kufikia sasa, jumla ya visa 8,162 vimeripotiwa nchi nzima vikiwemo vifo 75.

Wagonjwa wapatao 834 mpaka sasa wameripotiwa kupata ahueni huku wengine 36 wangali wakiwa katika hali mbaya zaidi.

Nchi hiyo imeweka kizuizi kwa watu wanaoingia kutokea mataifa yaliyoathirika zaidi ambapo watahitajika kufanyiwa vipimo na kutoa taarifa zao za kiafya kupitia 'app' maalumu iliyoundwa nchini humo.
 
Back
Top Bottom