nyumbamungu
JF-Expert Member
- Mar 3, 2017
- 994
- 821
Nami naomba nichangie kiduchu ingawa mleta uzi amajibu kwaa usahihi na kwa ufupi unaoleweka.
Kung'atana kitaalamu wanaita "cannibalism" hii ni moja ya tabia mbaya kwa kuku wanaofugwa muda mwingi wakiwa ndani.
Hii hutokana na baadhi ya haya yafuatayo:
1. Kukosa madini lishe kama fosiforasi na kalisiam, madini haya hupatikani kwa wingi kwenye unga wa mifupa na chokaa ya mifugo.
2. Msongo(Stress), hii hutokana na Msongamano ama mrundikano wa kuku (kuku wengi eneo dogo).
3. Kuweka kuku wa umri tofauti ndani ya banda moja, hii usababisha kuku wakubwa kupiga na kuwadonoa kuku wadogo.
Tiba na kinga.
1. Kuwapa chakula chenye uwiano sahihi wa chokaa na unga wa mifupa.
2. Kuwaongezea nafasi ili wawe na eneo pana la kucheza kuepusha kusongamana.
3. Wapatie mchanganyiko wa maji na vitamini(Anti-stress) kwa kipindi kilichoelekezwa katika mfuko ama kibandiko.
3. Kuwafungia majani ama mboga za majani ili wapate sehemu ya kupunguzia msongo kwa kula majani yaliyo ning'inia.
4. Kuwatenga walioathirika haraka sana maana kuku anapoona damu ile sehemu itashambuliwa sana, kwa hiyo unapomtenga muathirika unaokoa maisha yake.
5. Mpe huduma ya kwanza kuku aliyeathirika kwa kumpaka "iodine tincture" na kumpa mchanganyiko wa maji na vitamini (kipunguza msongo ama "anti-stress").
Habari ya asubuhi ndugu kwa mawasiliano zaidi unaweza kutoa elimu kwa anaehitaji?