Fahamu jinsi ya kutengeneza chakula chako cha kuku ili kupata faida

Nami naomba nichangie kiduchu ingawa mleta uzi amajibu kwaa usahihi na kwa ufupi unaoleweka.
Kung'atana kitaalamu wanaita "cannibalism" hii ni moja ya tabia mbaya kwa kuku wanaofugwa muda mwingi wakiwa ndani.

Hii hutokana na baadhi ya haya yafuatayo:

1. Kukosa madini lishe kama fosiforasi na kalisiam, madini haya hupatikani kwa wingi kwenye unga wa mifupa na chokaa ya mifugo.
2. Msongo(Stress), hii hutokana na Msongamano ama mrundikano wa kuku (kuku wengi eneo dogo).
3. Kuweka kuku wa umri tofauti ndani ya banda moja, hii usababisha kuku wakubwa kupiga na kuwadonoa kuku wadogo.
Tiba na kinga.
1. Kuwapa chakula chenye uwiano sahihi wa chokaa na unga wa mifupa.
2. Kuwaongezea nafasi ili wawe na eneo pana la kucheza kuepusha kusongamana.
3. Wapatie mchanganyiko wa maji na vitamini(Anti-stress) kwa kipindi kilichoelekezwa katika mfuko ama kibandiko.
3. Kuwafungia majani ama mboga za majani ili wapate sehemu ya kupunguzia msongo kwa kula majani yaliyo ning'inia.
4. Kuwatenga walioathirika haraka sana maana kuku anapoona damu ile sehemu itashambuliwa sana, kwa hiyo unapomtenga muathirika unaokoa maisha yake.
5. Mpe huduma ya kwanza kuku aliyeathirika kwa kumpaka "iodine tincture" na kumpa mchanganyiko wa maji na vitamini (kipunguza msongo ama "anti-stress").

Habari ya asubuhi ndugu kwa mawasiliano zaidi unaweza kutoa elimu kwa anaehitaji?
 
@OS Cordis,

Au ni ugeni wa kutumia JF, au kutoelewa inanijibu sitoweza kuunganishwa ww ndio umeweka zuio. Mashikholhomaghenhi Mamma.
 
Mahindi= 40 kg
Dagaa = 12 kg
Maharage ya soya = 14 kg
Chokaa = 4 kg
Mkuu hii ina tofauti gani na kununua chakula dukani kilichotengenezwa tayari
nimejaribu kujumulisha naona kama bei zinafanana na pia muda wa kununua na kuandaasi ni ghali zaidi?
 
JINSI YA KUJITENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWA AJILI YA KUONGEZA UZALISHAJI

Kutokana na kuongezeka kwa gharama za chakula cha kuku iwewawia vigumu wafugaji wa kuku kupata faida kupitia ufugaji wa kuku. N akwa jinsi utengenezaji wa chakula cha kuku hasa hasa kuku wa kisasa kama broiler na layers kwa wafugaji ni ngumu leo nakuja na somo jepesi la jinsi ya kutengeneza chakula kwa kuku chotara (hybrid) or kuku wa kienyeji wanaofugwa ndani ya banda kwa kutumia Pearson Square method nah ii yote yawezekana kama mkulima atakuwa na raw materials zinazohitajika katika utengenezaji wa chakula.

Njia HII ya pearson square mara nyingi ina base sana katika Digestable crude protein (DCP) ya malighafi husika katika utengenezaji wa chakula. Na malighafi zinazotahitajika hapa ni kama vile Mahindi, mashudu ya pamba, mashudu ya alzeti, maharage ya soya na dagaa.

Jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku wa mayai (70kg) (chotara) unahitaji vifuatavyo;

34 kg Mahindi
12 kg Soya beans
8 kg Dagaa
10 kg pumba za mahindi
6 kg Chokaa (kwa ajili ya calcium)

Jinsi ya kutengeneza chakula(70kg) kwa ajili ya kuku wa nyama

Mahindi= 40 kg
Dagaa = 12 kg
Maharage ya soya = 14 kg
Chokaa = 4 kg

NB: Hakikisha unaongeza chumvi 250g katika kila mfuko wa 70kg wa chakula chako

Ndondoo muhimu ya jinsi ya kuwalisha kuku wako Nyumbani

Kuku anaetaga mayai anahitaji kula angalau 130g za chakula kwa siku. Kumbuka kuwapa maji masafi muda wote.

Kifaranga kimoja anahitaji 2.2 kg za chakula kwa wiki 8 (hivyo basi vifaranga 100 = 2.2 kg x 100=220 kg. Vifaranga wanahitaji kula muda wote na pia suala la maji ni muhimu kwao pia na unakumbushwa kuwapa mboga mboga baada ya mlo wao kuisha.

Kuku mdogo anayekaribia kutaga anatakiwa kula 4.5 kg ya chakula kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka watakapoanza kutaga yai kwa mara ya kwanza. Baada ya hapo wanabadilishiwa chakula na kupewa chakula cha utagaji (layer diet).

Malighafi zinazotakiwa katika utengenezaji wa chakula zinatakiwa zile za kiwango cha juu kabisa usitumie mahindi yenye uozo maana utafanya kuku wako kupata ugonjwa wa aflatoxins poisoning.

Ukitumia dagaa hakikisha ni wasafi na hawana mchanga ama shells wa aina yoyote.

Na mwisho hakikisha chakula hicho unakichanganya vizuri kabisa ili kuleta uwiano au mchanganyo ulio sahihi.

Hitimisho
Kwa formular za Chakula za Kuku wa kisasa kama Broiler na Layer tunaweza wasiliana kwa namba zangu hapo chini na hakika zitakuongezea uzalishaji maradufu ya chakula cha kununua.

Imeandaliwa na Dr of Veterinary Medicine
Kutokana na gharama ya soya wengi hutumia mashudu kwa kuwa hayana kazi nyingine
 
Mkuu Dr. Of Veterinary Kuna mahali nlipita nikakuta wanachimba udongo Wana uchanganya na pumba kwa chakula Cha kuku je hiyo waiongeleaje Mkuu
 
Tafuteni Azola.... Mtapenda.
Makuku yatanenepa, yatashusha mayai hadi udate....
Then zingatieni kuwapatia NEOCHICK.
 
Swali. Hivi mtu ukiacha kuweka Dagaa ukaweka Uduvi ni sawa?au Ukaweka Chokaa badala ya Mifupa ni sawa? Na ayo mahindi niyale yaliyo vunjwa vunjwa au mazima?.zaidi ya yote tunasema Asante mtaalam kwa Elimu hii nzuri Mungu akubari.

Sent from my TECNO K8 using JamiiForums mobile app
 
JINSI YA KUJITENGENEZA CHAKULA CHA KUKU NYUMBANI KWA AJILI YA KUONGEZA UZALISHAJI

Kutokana na kuongezeka kwa gharama za chakula cha kuku iwewawia vigumu wafugaji wa kuku kupata faida kupitia ufugaji wa kuku. N akwa jinsi utengenezaji wa chakula cha kuku hasa hasa kuku wa kisasa kama broiler na layers kwa wafugaji ni ngumu leo nakuja na somo jepesi la jinsi ya kutengeneza chakula kwa kuku chotara (hybrid) or kuku wa kienyeji wanaofugwa ndani ya banda kwa kutumia Pearson Square method nah ii yote yawezekana kama mkulima atakuwa na raw materials zinazohitajika katika utengenezaji wa chakula.

Njia HII ya pearson square mara nyingi ina base sana katika Digestable crude protein (DCP) ya malighafi husika katika utengenezaji wa chakula. Na malighafi zinazotahitajika hapa ni kama vile Mahindi, mashudu ya pamba, mashudu ya alzeti, maharage ya soya na dagaa.

Jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku wa mayai (70kg) (chotara) unahitaji vifuatavyo;

34 kg Mahindi
12 kg Soya beans
8 kg Dagaa
10 kg pumba za mahindi
6 kg Chokaa (kwa ajili ya calcium)

Jinsi ya kutengeneza chakula(70kg) kwa ajili ya kuku wa nyama

Mahindi= 40 kg
Dagaa = 12 kg
Maharage ya soya = 14 kg
Chokaa = 4 kg

NB: Hakikisha unaongeza chumvi 250g katika kila mfuko wa 70kg wa chakula chako

Ndondoo muhimu ya jinsi ya kuwalisha kuku wako Nyumbani

Kuku anaetaga mayai anahitaji kula angalau 130g za chakula kwa siku. Kumbuka kuwapa maji masafi muda wote.

Kifaranga kimoja anahitaji 2.2 kg za chakula kwa wiki 8 (hivyo basi vifaranga 100 = 2.2 kg x 100=220 kg. Vifaranga wanahitaji kula muda wote na pia suala la maji ni muhimu kwao pia na unakumbushwa kuwapa mboga mboga baada ya mlo wao kuisha.

Kuku mdogo anayekaribia kutaga anatakiwa kula 4.5 kg ya chakula kwa muda wa miezi miwili na nusu mpaka watakapoanza kutaga yai kwa mara ya kwanza. Baada ya hapo wanabadilishiwa chakula na kupewa chakula cha utagaji (layer diet).

Malighafi zinazotakiwa katika utengenezaji wa chakula zinatakiwa zile za kiwango cha juu kabisa usitumie mahindi yenye uozo maana utafanya kuku wako kupata ugonjwa wa aflatoxins poisoning.

Ukitumia dagaa hakikisha ni wasafi na hawana mchanga ama shells wa aina yoyote.

Na mwisho hakikisha chakula hicho unakichanganya vizuri kabisa ili kuleta uwiano au mchanganyo ulio sahihi.

Hitimisho
Kwa formular za Chakula za Kuku wa kisasa kama Broiler na Layer tunaweza wasiliana kwa namba zangu hapo chini na hakika zitakuongezea uzalishaji maradufu ya chakula cha kununua.

Imeandaliwa na Dr of Veterinary Medicine
Naomba mawasiliano yako mkuu.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom