Fahamu jinsi wahandisi wa vyombo vya angani wanavyommezea mate bundi

101 East

JF-Expert Member
Feb 25, 2015
1,040
2,118
Kwa miaka mingi mainjinia na maprofesa wa ubunifu wa miundo ya ndege wamekuwa wakimmezea mate bundi arukaye usiku.

Je ni kwanini Bundi amekuwa akimezewa mate kutokana na uwezo wake wa ajabu wa mbawa zake.
Hii ni kwasababu mbawa zake hazipigi kelele pale anaporuka.

Wataalam kutoka national geographic wanasema hakuna ndege yeyote duniani anayeruka kimya kimya hivyo. Ndege wengi wanaporuka wao hutokeza kelele wakati upepo unapopita juu ya manyoya yao. Lakini manyoya ya bundi hayafanyi hivyo.

Manyoya yake ya nyuma yana miisho ya kipekee ambayo hutawanya mawimbi ya sauti yanayotokeza pindi upepo unapopita juu ya manyoya yao.

Anapopiga mbawa zake chini wakati wa kuruka. Manyoya mengine husaidia kufyonza kelele yoyote inayotokea.

Mainjinia wa vyombo vya angani bado wanaendelea kutafiti uwezo huo wa kuruka bila kelele ili hatimaye watengeneze ndege yenye uwezo huo wa kuruka bila kelele.

Kuwa na ndege za aina hiyo vitasaidia viwanja vya ndege vilivyo na sheria kali kuhusu kelele nyingi viruhusu ndege kutua usiku sana na mapema sana asubuhi.

Profesa Geofrey Lilley ambaye ni profesa aliyestaafu wa vyombo vya angani chuo kikuu cha Southampton Uingereza anasema "tumeanza sasa kuboresha ndege kwenye njia hiyo na huenda ikachukua miongo kadhaa kabla ya ndege inayo ruka kimya kimya kutengenezwa.

View attachment 1588802View attachment 1588801
IMG_20201003_083148.jpg
 
Hata wakati Dr.Cooper anatangaza uvumbuzi wa simu ya kwanza ya mkononi mwanzoni mwa miaka ya 80 watu wengi walimshangaa maana walizoea simu ni ya kukaa mezani itakuwaje kuanza kutembea nayo ,tena ilikuwa na uzito wa 1kg

Dr akawaambia watu, sasa ivi mnaniona Mimi chizi Ila siku moja nitawajibu...ilipofika mwaka 90 nusu ya wakazi wa New York walikuwa wanamiliki simu ya mkononi
Ndipo alipowajibu naona sasa hivi ,watu wote wamekuwa machizi kwa kuongea wenyewe barabarani...

Mara nyingi jicho la kawaida haliwezi kuona bali linaangalia
 
Wacha wanunue sisi tutapanda na kununua

TANZANIA ya viwanda
Cause ata hiyo ya makelele hatujui kutengeneza
 
Hata wakati Dr.Cooper anatangaza uvumbuzi wa simu ya kwanza ya mkononi mwanzoni mwa miaka ya 80 watu wengi walimshangaa maana walizoea simu ni ya kukaa mezani itakuwaje kuanza kutembea nayo ,tena ilikuwa na uzito wa 1kg

Dr akawaambia watu, sasa ivi mnaniona Mimi chizi Ila siku moja nitawajibu...ilipofika mwaka 90 nusu ya wakazi wa New York walikuwa wanamiliki simu ya mkononi
Ndipo alipowajibu naona sasa hivi ,watu wote wamekuwa machizi kwa kuongea wenyewe barabarani...

Mara nyingi jicho la kawaida haliwezi kuona bali linaangalia
Unahabari kuwa bila kuwepo sisi wachambia wima hao watafiti wasingekuwa wanajisumbua kiivyo!.. tupo ndio maana wanatumia nguvu kubwa kutuprove wrong!.. tunasubiri silent ndege.
 
Kwa miaka mingi mainjinia na maprofesa wa ubunifu wa miundo ya ndege wamekuwa wakimmezea mate bundi arukaye usiku.

Je ni kwanini Bundi amekuwa akimezewa mate kutokana na uwezo wake wa ajabu wa mbawa zake.
Hii ni kwasababu mbawa zake hazipigi kelele pale anaporuka.

Wataalam kutoka national geographic wanasema hakuna ndege yeyote duniani anayeruka kimya kimya hivyo. Ndege wengi wanaporuka wao hutokeza kelele wakati upepo unapopita juu ya manyoya yao. Lakini manyoya ya bundi hayafanyi hivyo.

Manyoya yake ya nyuma yana miisho ya kipekee ambayo hutawanya mawimbi ya sauti yanayotokeza pindi upepo unapopita juu ya manyoya yao.

Anapopiga mbawa zake chini wakati wa kuruka. Manyoya mengine husaidia kufyonza kelele yoyote inayotokea.

Mainjinia wa vyombo vya angani bado wanaendelea kutafiti uwezo huo wa kuruka bila kelele ili hatimaye watengeneze ndege yenye uwezo huo wa kuruka bila kelele.

Kuwa na ndege za aina hiyo vitasaidia viwanja vya ndege vilivyo na sheria kali kuhusu kelele nyingi viruhusu ndege kutua usiku sana na mapema sana asubuhi.

Profesa Geofrey Lilley ambaye ni profesa aliyestaafu wa vyombo vya angani chuo kikuu cha Southampton Uingereza anasema "tumeanza sasa kuboresha ndege kwenye njia hiyo na huenda ikachukua miongo kadhaa kabla ya ndege inayo ruka kimya kimya kutengenezwa.

View attachment 1588802View attachment 1588801View attachment 1588803
Kwanza sizani Kama ni wazo zuri Sana maana upo zako gheto unakula Mambo au umetulia tu from no where bombardier hiyo imetua juu ya paa lako inakupeleka kwa baba bila taarifa na unakuta unamidhambi mpk shetani anasikitika..😂

We don't need silent ndege Labda watengeneze zakijeshi huku au za maspy.. kwanza wanahangaika na sauti badala ya kuratibu zaidi kwenye upungufu wa ajali.. najua ajali za ndege ni ndogo lkn ikianguka chance ya kupona ni finyu,so wadili na kuongeza chances za mtu kutoka akiwa hai kwenye ndege kuliko kuhangaika na u silent.
 
Unahabari kuwa bila kuwepo sisi wachambia wima hao watafiti wasingekuwa wanajisumbua kiivyo!.. tupo ndio maana wanatumia nguvu kubwa kutuprove wrong!.. tunasubiri silent ndege.
Habari hiyo ninayo...maana duniani Kuna aina mbili za watu ,watu wanaosababisha vitu kutokea na watu wanaosubiri vitu kutokea
 
Back
Top Bottom